Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/07/10
“Wengi kati yetu hawajue jambo la kusema wanapokuwa mbele ya rafiki aliye mgonjwa sana ao anayekaribia kufa. Unafikiri nini kuhusu shauri hili? [Soma Yakobo 1:19. Kisha acha mutu ajibu.] Habari hii inatoa mawazo fulani yanayotegemea kanuni za Biblia.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Amkeni! Mwezi wa 7
“Je, wanawake wanapaswa kuwa watumishi katika kanisa? [Acha mutu ajibu.] Ona yale Biblia inayosema kuhusu mwanamuke mmoja. [Soma Waroma 16:1.] Lakini, andiko lingine linasema kwamba wanawake wanapaswa kubaki kimya katika kutaniko. Kwa hiyo basi, maoni ya Biblia ni nini kuhusu jambo hilo? Mafasirio yanapatikana katika habari hii.” Onyesha habari iliyo kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi 01/08/10
“Watu wengi wanaogopa kwamba vita ya nyukilia ao mabadiliko ya hali ya hewa vitaharibu dunia. Wewe unawaza jambo hilo litatokea? [Acha mutu ajibu.] Ona yale Biblia inayosema kuhusu jambo hilo. [Soma Ufunuo 11:18.] Gazeti hili linajibu maulizo 4 ambayo watu wanajiuliza mara nyingi kuhusu mwisho wa dunia.”
Amkeni! Mwezi wa 8
“Labda umewahi kuzungumza na Mashahidi wa Yehova. Umekwisha kujiuliza kwa nini tunahubiri mlango kwa mlango, hata ikiwa watu wengi hawapendezwi? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Mathayo 24:14.] Watu wengi hawajue vizuri Mashahidi wa Yehova. Gazeti hili litakusaidia ujuwe ikiwa wao ni nani.”