Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/01/10
“Je, unafikiri kwamba ulimwengu ungekuwa mahali pazuri ikiwa kila mutu angetii kanuni hii ya Biblia? [Soma Waroma 12:18. Kisha acha mutu ajibu.] Hivyo basi, je, umekwisha kujiuliza kwa nini nyakati fulani Mungu aliwaongoza watu wake wapigane vita katika nyakati za zamani? Habari hii inaonyesha jibu la Biblia lililo wazi.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 13.
Amkeni! Mwezi wa 1
Soma Matendo 17:31a. Kisha useme: “Wazo la Siku ya Hukumu linaogopesha watu wengi. Unafikiri nini kuhusu Siku ya Hukumu? [Acha mutu ajibu.] Biblia inafundisha kwamba Siku ya Hukumu italeta baraka nyingi duniani. Habari hii inaeleza jambo hilo.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi 01/02/10
“Watu wengi wanatumaini kwamba wataenda mbinguni wanapokufa. Je, tumaini hilo linakupendeza? [Acha mutu ajibu.] Ona zawadi ambayo Biblia inasema watu wazuri wengi watapokea. [Soma Zaburi 37:29.] Gazeti hili linazungumzia mawazo ya Biblia kuhusu wale watakaoenda mbinguni na kile ambacho watafanya huko.”
Amkeni! Mwezi wa 2
“Watu wengi wanavunja ndoa leo. Je, unafikiri kwamba waume na wake wengi wanafikiria matokeo mabaya ya jambo hilo mbele ya kuamua kuvunja ndoa? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Methali 14:15.] Gazeti hili linazungumzia mambo mane ambayo watu waliooana wanapaswa kuchunguza wanapofikiria kuvunja ndoa.”