Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 4
“Tunawatia moyo majirani wetu wasome Biblia zao. Lakini watu wengi wanaona kwamba ni vigumu kuielewa Biblia. Wewe pia umeona hilo? [Acha mutu ajibu.] Ona jambo tunalosoma hapa.” Umuonyeshe habari iliyo kwenye ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 4, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja lililo hapo. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/04/13
“Kila mutu tunayezungumuza naye ana magumu. Hilo linafanya watu fulani wafikiri juu ya kusudi la maisha. Wewe unawaza ni jambo gani hasa linalofanya watu wakose furaha leo? [Acha mutu ajibu.] Biblia inatuahidi kwamba karibuni Mungu atamaliza magumu tunayopata leo. [Soma Ufunuo 21:4.] Gazeti hili linazungumuzia mambo tunayongojea wakati ujao na namna tunavyoweza kuishi maisha yenye kusudi leo.”
Amkeni! Mwezi wa 4
“Duniani pote, watu wanatendewa vibaya nyumbani. Wengine wanasema kwamba ikiwa mutu anatendea wengine vibaya nyumbani hilo linatokana na desturi ya jamii yake, malezi aliyopata, na mambo ya jeuri anayotazama kwenye televizyo. Wewe unawaza ni nini hasa kinachofanya watu watendewe vibaya nyumbani? [Acha mutu ajibu.] Biblia inaonyesha uhusiano unaofaa unaopaswa kuwa kati ya bibi na bwana. [Soma Waefeso 5:33.] Gazeti hili linaonyesha namna ndoa fulani zimeokoka kwa sababu ya kutumia kanuni za Biblia.”