Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuzoeza Mwanafunzi wa Biblia Ili Akuwe na Programu Nzuri ya Kujifunza
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Ili wafikie kukomaa kiroho, wanafunzi wa Biblia wanapaswa kujaza akili na mioyo yao mafundisho mengine zaidi ya mafundisho ya musingi ya Neno la Mungu. (Ebr. 5:12–6:1) Unapaswa kujikaza sana ili kujifunza, ni kusema unapaswa kulinganisha habari yenye unasoma na habari zenye tayari unajua, na kuona namna gani unaweza kutumikisha habari hiyo. (Met. 2:1-6) Kufundisha wanafunzi namna wao wenyewe wanaweza kutafuta habari kutawasaidia kupata majibu ya Biblia kwa kutumia vichapo vyetu. Kujikaza sana kutumikisha mambo yenye wanajifunza kutawasaidia kushindana na majaribu yenye watapata katika maisha yao ya Kikristo.—Lu. 6:47, 48.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Wakati munamaliza kichwa kidogo ao sura fulani, umuulize mwanafunzi wako wa Biblia aeleze kwa kifupi mambo yenye amejifunza. Kama hauna funzo ya kuongoza, soma andiko fulani ao fungu fulani la Munara wa Mulinzi, kisha ueleze kwa kifupi katika maneno yako mwenyewe ili kukomalisha uwezo wako wa kuelewa mambo.