Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp20 na. 3 uku. 14-15
  • Unaweza Kupata Baraka za Milele za Muumbaji Wetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unaweza Kupata Baraka za Milele za Muumbaji Wetu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Miujiza ya Yesu Inaweza Kutufundisha Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Aliwapenda Watu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mambo Yenye Manabii Wanatufundisha Kumuhusu Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Kristo—Nguvu za Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
wp20 na. 3 uku. 14-15
Watu wa kila desturi na kabila wanafurahia kuwa pamoja mu dunia paradiso.

“Dunia itatoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, atatubariki.”​—ZABURI 67:6

Unaweza Kupata Baraka za Milele za Muumbaji Wetu

Mungu aliahidi nabii Abrahamu kama mumoja wa wazao wake ataletea baraka “mataifa yote ya dunia.” (Mwanzo 22:18) Ule muzao ni nani?

Miaka karibu 2 000 yenye imepita, Mungu alipatia Yesu, mwenye alikuwa muzao wa Abrahamu, uwezo wa kufanya miujiza ya ajabu. Ile miujiza ilionyesha kama Yesu njo mwenye Mungu angetumia ili kubariki mataifa yote, kama vile alimuahidi Abrahamu.​—Wagalatia 3:14.

Miujiza yenye Yesu alifanya ilionyesha kama ni yeye njo Mungu amechagua ili kubariki wanadamu, na ilionyesha pia namna Mungu atamutumia ili kubariki wanadamu milele. Ona namna miujiza ya Yesu inaonyesha sifa fulani za Yesu zenye kupendeza.

Upole​—Yesu aliponyesha wagonjwa.

Siku moja, mutu mwenye ukoma alimulilia Yesu amuponyeshe. Yesu alimugusa na kumuambia: “Ninataka!” Mara moja, ukoma wake ukaisha.​—Marko 1:40-42.

Ukarimu​—Yesu alikulisha wenye njaa.

Yesu hakupenda watu waende na njaa. Mara mingi Yesu alikulisha kimuujiza maelfu ya watu kwa kufanya mikate na samaki kidogo ikuwe mingi. (Matayo 14:17-21; 15:32-38) Kisha kula, wote walishiba na chakula mingi ilibakia.

Huruma​—Yesu alifufua wafu.

Kwa sababu ‘alimusikilia huruma,’ Yesu alifufua mutoto mumoja tu wa mujane mwenye hakukuwa na mutu mwingine yeyote wa kumuhangaikia.​—Luka 7:12-15.

BARAKA ZA MILELE KU DUNIA

Tayari Yesu ameonyesha kama Mungu iko na uwezo wa kuletea wanadamu baraka. Hivi karibuni, wakati Yesu atarudia, sawa vile aliahidi, Mweza-Yote atamutumia ili afanye miujiza ya ajabu hata zaidi mu dunia yote!

Maisha itakuwa namna gani ku dunia wakati Mungu atatimiza ahadi yenye alimutolea Abrahamu? Wale wenye wanamupenda na kumuheshimia Mungu “watariti dunia” na watapata “furaha nyingi sana katika wingi wa amani.” (Zaburi 37:11) “Kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—Ufunuo 21:4.

Itafurahisha sana kuishi milele ku dunia na tena kwa amani! Tunakutia moyo ujifunze zaidi kuhusu baraka zenye utawala wa Mungu utaleta hivi karibuni kwa kufungua www.jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine