Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp20 na. 3 uku. 13
  • Tunapaswa Kusaidia Wenye Wako na Lazima ya Musaada juu Tupate Baraka

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tunapaswa Kusaidia Wenye Wako na Lazima ya Musaada juu Tupate Baraka
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAMBO YENYE MAANDIKO MATAKATIFU INASEMA
  • NAMNA GANI TUNAWEZA KUSAIDIA MUTU MWENYE IKO NA LAZIMA YA MUSAADA?
  • Mufano wa Musamaria Mwema
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • ‘Utaendelea Kukesha’?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Umasikini
    Amuka!—2015
  • Habari Njema Kwa Maskini
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
wp20 na. 3 uku. 13
Mwanaume mumoja anatumia karte juu ya kuonyesha mwanaume mwingine adresi.

Unaweza kusaidia wengine bila kuangalia miaka, inchi, ao dini yao?

Tunapaswa Kusaidia Wenye Wako na Lazima ya Musaada juu Tupate Baraka

Watu wengi mu dunia wako na lazima ya chakula na nyumba. Wamoja wako tu na lazima ya tumaini la wakati wenye kuja. Namna gani bidii yetu ya kusaidia wale watu inaweza kufanya Mungu atukubali na kutubariki?

MAMBO YENYE MAANDIKO MATAKATIFU INASEMA

“Mwenye anaonyesha mutu wa hali ya chini wema anamukopesha Yehova, na Yeye atamulipa kwa sababu ya mambo yenye anatenda.”​—MEZALI 19:17.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUSAIDIA MUTU MWENYE IKO NA LAZIMA YA MUSAADA?

Yesu alitoa mufano wa mwanaume mwenye alishambuliwa na wanyanganyi na wakamuacha karibu kufa. (Luka 10:29-37) Mutu fulani wa roho muzuri mwenye alikuwa hamujue alisimama na kusaidia ule mwanaume mwenye alikuwa ameumizwa mubaya. Alimusaidia hata kama hakukuwa wa kabila yake.

Ule mwanaume wa roho muzuri hakumutolea tu matunzo ya kwanza-kwanza na musaada wa kimwili lakini pia alimufariji na kumutuliza.

Ule mufano unatufundisha nini? Yesu alipenda kutufundisha kama tunapaswa kufanya yote yenye tunaweza ili kusaidia wale wenye wako na lazima ya musaada. (Mezali 14:31) Maandiko Matakatifu inafundisha kama hivi karibuni Mungu atamaliza umaskini na mateso. Lakini, tunaweza kujiuliza: Mungu atafanya vile namna gani na wakati gani? Habari yenye kufuata itazungumuzia baraka zenye Muumbaji wako mwenye upendo amekutayarishia.

“MUNGU HAJANIACHAKA”!

Maelezo ya mutu mwenye alitoka Gambia na kuhamia Ulaya

“Wakati nilifika Ulaya, sikukuwa na kitu. Sikukuwa na kazi, feza, na nyumba. Mafundisho ya Maandiko Matakatifu imenisaidia nikuwe na hekima, nikuwe na bidii mu kazi, na nisaidie wengine kuliko tu kuwaomba musaada. Mungu hajaniachaka, na nimejionea baraka yake!”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine