UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | LUKA 10-11
Mufano wa Musamaria Mwema
Yesu alitoa mufano huo ili kujibu ulizo hili: “Kwa kweli jirani yangu ni nani?” (Lu 10:25-29) Alijua kama kutaniko la Kikristo lingefikia kuwa na watu wa “namna zote,” hata Wasamaria na Watu wa Mataifa. (Yoh 12:32) Mufano huo ulifundisha wafuasi wa Yesu kama walipaswa kujikaza sana ili kuonyesha wengine upendo, hata wale wenye walikuwa tofauti kabisa nao.
UJIULIZE:
‘Ninaona namna gani ndugu na dada wa desturi zingine?’
‘Ninapitisha zaidi wakati pamoja na wale tu wenye kupenda mambo yenye ninapendaka?’
‘Ninaweza kupanuka tena zaidi kwa kufanya urafiki pamoja na ndugu na dada wenye kuwa na desturi tofauti na zangu?’ (2Kor 6:13)
Ninapanga kualika . . .
ahubiri pamoja na miye
akuje kwangu ili tukule pamoja
ajiunge na familia yangu kwa ajili ya Ibada yetu ya Familia ya mangaribi