Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 5-11/03
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 20-21
“Kila Mutu Mwenye Anataka Kuwa Mukubwa Katikati Yenu Anapaswa Kuwa Mutumishi Wenu”
nwtsty picha na video
Soko
Soko fulani, kama ile yenye kuonyeshwa katika Buku la Mukutano, zilikuwa pembeni ya barabara. Mara nyingi watu wenye kuuzisha walitandika kwenye barabara vitu vingi vya kuuzisha; hilo lilizuia watu kutembea. Wakaaji wa mahali hapo walikuwa wanauza vitu vya kutumia nyumbani, vyombo vya udongo, na bilauri vya bei sana; waliuza pia vitu vyenye vilitoka kuvunwa. Kwa sababu wakati huo frigo haikukuwa, kila siku watu walipaswa kuenda kwenye soko kuuza vitu. Huko, watu wenye kuuzisha walikuwa wanasikia habari zenye wafanyabiashara ao wageni wengine walileta, watoto walikuwa wanacheza, na watu wenye hawakukuwa na kazi walichunga mutu fulani awapatie kazi. Yesu aliponyesha mugonjwa fulani kwenye soko, na Paulo alihubiri katika soko. (Mdo 17:17) Lakini, Waandishi na Mafarisayo wenye kiburi walipenda watu wawaone na kuwasalimia mahali penye watu wengi kama hapo.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 20:20, 21
mama ya wana wa Zebedayo: Ni kusema, mama ya mitume Yakobo na Yohana. Kulingana na Injili ya Marko, ni Yakobo na Yohana ndio walimuendea Yesu. Ni wazi kama ni wao walifanya ombi, lakini kupitia mama yao, Salome, mwenye pengine alikuwa shangazi ya Yesu.—Mt 27:55, 56; Mk 15:40, 41; Yoh 19:25.
mumoja kwenye mukono wako wa kuume na mwingine kwenye mukono wako wa kushoto: Hapa, kushoto na kuume kunamaanisha heshima na mamlaka, lakini mukono wa kuume ndio wenye heshima kubwa zaidi.—Zab 110:1; Mdo 7:55, 56; Rom 8:34.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 20:26, 28
mutumishi: Ao “mutumwa.” Kila mara Biblia inatumia neno la Kigiriki di·aʹko·nos ili kumaanisha mutu mwenye anaendelea kujinyenyekeza ili kutumikia wengine. Neno hilo linatumiwa kwa Kristo (Rom 15:8), watumishi ao watumwa wa Kristo (1Kor 3:5-7; Kol 1:23), watumishi wa huduma (Flp 1:1; 1Tim 3:8), na pia wafanyakazi wa nyumbani (Yoh 2:5, 9) na wakubwa wa serikali (Rom 13:4).
hakukuja ili watu wamutumikie, lakini ili yeye atumikie wengine: Ao “hakukuja ili kutumikiwa, lakini ili atumikie.”
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 21:9
Okoa, tunaomba: Neno kwa neno, “Hosanna.” Neno hilo la Kigiriki linatokana na maneno ya Kiebrania yenye kumaanisha “okoa, tunaomba” ao “okoa, tafazali.” Hapa neno hilo linatumiwa kama ombi kwa Mungu kwa ajili ya wokovu ao ushindi; linaweza pia kutafsiriwa “tafazali, toa wokovu kwa.” Kisha muda, neno hilo lilianza kumaanisha mambo mawili: sala na sifa. Neno hilo la Kiebrania linapatikana katika Zaburi 118:25, yenye ilikuwa sehemu ya Zaburi za Haleli zenye watu walizoea kuimba kila mwaka wakati wa Pasaka. Kwa hiyo, wakati huo, watu walikuwa wanakumbuka mara moja maneno hayo. Njia moja yenye Mungu alitumia ili kujibia sala hiyo ya kuokoa Mwana wa Daudi ilikuwa kumufufua kutoka kwa wafu. Kwenye Mathayo 21:42, Yesu mwenyewe anataja Zaburi 118:22, 23 na anasema kama inatimia juu ya Masiya.
Mwana wa Daudi: Hapa, maneno haya inaonyesha kama watu wanatambua kizazi cha Yesu na daraka lake la kuwa Masiya mwenye aliahidiwa.
Anatumia Muti wa Tini ili Kufundisha Somo Fulani Kuhusu Imani
Lakini, sababu gani Yesu alifanya ule muti ukauke? Anafunua sababu katika jibu lake: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, kama muko na imani na hamuna mashaka, hamutafanya tu jambo lenye nilifanyia muti wa tini, lakini hata mukiambia mulima huu, ‘Ondoka na utupwe katika bahari,’ jambo hilo litatendeka. Na mambo yote yenye munaomba katika sala, kama muko na imani, mutayapokea.” (Mathayo 21:21, 22) Kwa hiyo anarudilia jambo lenye alikuwa amesema kuhusu uwezo wa imani wa kuhamisha mulima.—Mathayo 17:20.
Kwa hiyo kwa kufanya muti ukauke,Yesu anaonyesha kuwa ni jambo la maana kumuamini Mungu. Anasema hivi: “Mambo yote yenye munaomba katika sala, mukuwe na imani kwamba mumekwisha kuyapokea, na mutayapata.” (Marko 11:24) Ni somo la maana kabisa kwa wanafunzi wote wa Yesu! Jambo hilo linafaa kabisa kwa mitume kwa sababu ya majaribu makali yenye watapata hivi karibuni. Kuko uhusiano mwengine kati ya muti wa tini kukauka na sifa ya imani.
Kama muti huo wa tini, taifa la Israeli liko na sura yenye kudanganya. Watu wa taifa hili wako katika agano pamoja na Mungu, na kwa inje wanaonekana kuwa wenye kushika Sheria yake. Lakini, wanashindwa kuzaa matunda mazuri na wanamukataa hata Mwana wa Mungu! Kwa hiyo, kwa kufanya muti wa tini ukauke, Yesu anaonyesha namna mwisho utakuwa kwa taifa hilo lenye kushindwa kuzaa matunda na lenye kukosa imani.
TAREHE 12-18/03
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 22-23
“Tii Zile Amri Mbili Kubwa Zaidi”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 22:37
moyo: Kwa kawaida, wakati neno hilo linatumiwa kwa njia ya mufano, linamaanisha mutu wote wa ndani. Lakini, wakati linatajwa pamoja na neno “nafsi” na “akili,” linachukua maana ingine kabisa na zaidi sana linamaanisha hisia za mutu, mambo yenye anatamani, na namna anajisikia. Maneno tatu yenye kutumiwa hapa (moyo, nafsi, na akili) inaweza kumaanisha jambo moja; inafanana, inakazia katika njia kubwa zaidi lazima ya kuwa na upendo kamili kwa Mungu.
nafsi: Ao “mutu wote muzima.”
akili: Ni kusema, uwezo wote wa kufikiri. Mutu anapaswa kutumia akili yake ili afikie kumujua Mungu na kuwa na upendo mukubwa kwake. (Yoh 17:3; Rom 12:1) Katika maneno haya ya Kumbukumbu la Torati 6:5, maandishi ya zamani ya Kiebrania inatumia maneno tatu, ‘moyo, nafsi, na nguvu.’ Lakini, kulingana na Injili ya Mathayo namna inaandikwa katika Kigiriki, neno lenye kutafsiriwa “akili” linatumiwa mahali pa neno “nguvu.” Kunaweza kuwa sababu mbalimbali zenye zilifanya maneno tofauti itumiwe. Kwanza, hata kama Kiebrania cha zamani hakikukuwa na neno lenye kumaanisha “akili,” neno “moyo” lilimaanisha pia “akili.” Wakati neno hilo linatumiwa kwa njia ya mufano, linamaanisha mutu wote wa ndani, ni kusema mawazo ya mutu, namna anajisikia, mielekeo, na makusudio. (Kum 29:4; Zab 26:2; 64:6; ona kwa ajili ya funzo kuhusu neno moyo katika andiko hili.) Ndiyo maana, mahali maandishi ya Kiebrania inatumia neno “moyo,” tafsiri ya Kigiriki ya Septante inatumia kila mara neno la Kigiriki lenye kumaanisha “akili.” (Mwa 8:21; 17:17; Met 2:10; Isa 14:13) Sababu ingine yenye pengine ilimusukuma Mathayo atumie neno la Kigiriki lenye kumaanisha “akili” kuliko kumaanisha “nguvu” wakati alikuwa anataja Kumbukumbu la Torati 6:5 ni kwamba, neno la Kiebrania lenye kumaanisha “nguvu [ao, “nguvu za uzima,”]” lilikuwa linamaanisha nguvu za kimwili na pia uwezo wa kufikiri ao akili. Hata ikuwe namna gani, kuingiana kwa mawazo kati ya maneno ya Kiebrania na Kigiriki kunaweza kusaidia kueleza sababu gani wakati walitaja Kumbukumbu la Torati, waandikaji wa Injili hawakutumia kabisa-kabisa maneno ileile.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 22:39
Ya pili: Kwenye Mathayo 22:37, kuko jibu la moja kwa moja lenye Yesu alitolea Mufarisayo; lakini sasa Yesu anaenda mbali zaidi ya ulizo lenye liliulizwa na anataja amri ya pili (Law 19:18); alipenda kufundisha kama amri hizo mbili haziwezi kubadilishwa na kama zinategemeza Sheria yote na Manabii.—Mt 22:40.
jirani: Neno hili la Kigiriki lenye kutafsiriwa “jirani” (neno kwa neno, “mutu wa karibu”) halimaanishe tu watu wenye tunaishi nao karibu. Linaweza pia kumaanisha mutu yeyote mwenye tuko naye uhusiano.—Lu 10:29-37; Rom 13:8-10.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 22:40
Sheria . . . Manabii: “Sheria” maana yake, vitabu vya Biblia kuanzia Mwanzo mupaka Kumbukumbu la Torati. “Manabii” maana yake, vitabu vya unabii vyenye kupatikana katika Maandiko ya Kiebrania. Hata hivyo, wakati maneno hayo inatajwa pamoja, inaweza kumaanisha Maandiko yote ya Kiebrania.—Mt 7:12; 22:40; Lu 16:16.
vinategemea: Tendo la Kigiriki lenye kumaanisha neno kwa neno “kushikilia juu ya” linatumiwa hapa kwa njia ya mufano ili kumaanisha “kutegemea; kuwa na musingi juu ya.” Yesu hakupenda kumaanisha tu Sheria pamoja na Amri Kumi, lakini pia Maandiko yote ya Kiebrania yenye kutegemea upendo.—Rom 13:9.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 22:21
Kaisari vitu vya Kaisari: Jibu la Yesu hapa, na pia katika habari yenye kufanana na hii, yenye kuzungumuziwa katika Marko 12:17 na Luka 20:25, ndiyo mahali moja tu kwenye Yesu anataja mutawala Muroma. Kati ya “vitu vya Kaisari” kuko kulipa kodi kwa sababu ya kazi mbalimbali zenye serikali inatimiza, na pia kuheshimia na kujitiisha kwa kadiri kwa wakubwa wa serikali.—Rom 13:1-7.
Mungu vitu vya Mungu: Kati ya vitu hivi kuko kumuabudu Mungu kwa moyo wetu wote, kumupenda kwa nafsi yetu yote, na kumutii kabisa na kwa ushikamanifu.—Mt 4:10; 22:37, 38; Mdo 5:29; Rom 14:8.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 23:24
wenye kuchuya imbu lakini munameza ngamia: Waisraeli walijua kama imbu alikuwa kati ya wanyama wadogo sana wenye hawakuwa safi, na ngamia alikuwa kati ya wanyama wakubwa sana wenye hawakuwa safi. (Law 11:4, 21-24) Yesu alitumia usemi wa kutia chumvi, pamoja na zihaka fulani, kwa kusema kama viongozi wa dini walichuya vinywaji vyao ili imbu zisiwafanye wakose kuwa safi, lakini walizarau kabisa mambo mazito ya Sheria, tendo lenye kufananishwa na kumeza ngamia.
TAREHE 19-25/03
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 24
“Endelea Kuwa Macho Kiroho Katika Siku za Mwisho”
it-1 uku. 112 fu. 10
Upendo
Upendo unaweza kupoa. Wakati Yesu Kristo alifasiria wanafunzi wake mambo yenye itatokea wakati wenye kuja, alisema waziwazi kama upendo (a·gaʹpe) wa watu wengi wenye kusema kama wanamuamini Mungu ungepoa. (Mt 24:3, 12) Mutume Paulo alitabiri kama watu watakuwa “wenye kupenda pesa;” hilo lingekuwa alama yenye kuonyesha nyakati za hatari zenye kuja (2 Tim 3:1, 2) Inaonekana wazi kama, mutu anaweza kuacha kanuni za muzuri, na kama upendo wa kweli wenye alikuwa nao unaweza kupoa. Hilo linaonyesha wazi kama ni lazima kuendelea kuwa na upendo na kuendelea kuukomalisha kwa kufikiri sana juu ya Neno la Mungu na kwa kutumikisha kanuni za Mungu katika maisha yetu.—Efe 4:15, 22-24.
w99 15/11 uku. 19 fu. 5
Je, Unatimiza Mambo Yote Yenye Mungu Anakuomba?
Yesu Kristo alisema hivi juu ya nyakati zetu zenye hatari: ‘Kama vile siku za Noa zilivyokuwa, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa. Kwa maana kama vile walivyokuwa katika siku hizo kabla ya garika, wakikula na kunywa, wanaume wakioa na wanawake wakiolewa, mupaka siku ambayo Noa aliingia ndani ya safina; nao hawakujali mupaka garika ikakuja na kuwafagilia mbali wote, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.’ (Mathayo 24:37-39) Kula na kunywa haiko mubaya kama tunafanya hivyo kwa kiasi, na ndoa ni mupango wenye ulianzishwa na Mungu mwenyewe. (Mwanzo 2:20-24) Lakini tukitambua kama hangaiko yetu kubwa imekuwa kufuatia mambo ya kawaida ya maisha, juu ya nini tusisali juu ya jambo hilo? Yehova anaweza kutusaidia tutangulize mambo ya Ufalme, tufanye mambo yenye kuwa sawa, na kutimiza mambo yenye anatuomba.—Mathayo 6:33; Waroma 12:12; 2 Wakorintho 13:7.
Mitume Wanaomba Alama
Anasema kama wanafunzi wake wanapaswa kuendelea kuwa macho, wenye kukesha, na kuwa tayari. Anakazia wazo hilo kupitia mufano huu mwengine: “Mujue jambo hili: Kama mwenye nyumba angejua ni wakati gani usiku mwizi atakuja, angekaa macho na hangeruhusu nyumba yake ivunjwe. Kwa hiyo ninyi pia mukuwe tayari, kwa sababu Mwana wa binadamu atakuja katika saa yenye hamuwazie.”—Mathayo 24:43, 44.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 24:8
maumivu ya taabu: Neno la Kigiriki linamaanisha neno kwa neno maumivu makali sana ya wakati wa kuzaa. Wakati linatumiwa hapa ili kumaanisha taabu, maumivu, na mateso kwa ujumla, linaweza kumaanisha kwamba, sawa na maumivu ya kuzaa, matatizo ya ulimwengu itaongezeka, itaendelea kuwa makali mupaka itafikia mwisho kwenye ziki kubwa yenye kutajwa katika Mathayo 24:21.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 24:20
kipindi cha baridi: Mvua kali, mafuriko, na baridi kali katika kipindi hiki vingefanya ikuwe nguvu sana kusafiri na kupata chakula na mahali pa kujificha.—Ezra 10:9, 13.
siku ya Sabato: Katika maeneo kama vile Yudea, vizuizi kuhusu sheria ya Sabato vilifanya ikuwe nguvu mutu asafiri mbali na kubeba mizigo; pia, milango ya miji haikufunguliwa siku ya Sabato.—Ona Matendo 1:12 na Nyongeza B12.
TAREHE 26/03–1/04
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 25
“Endelea Kukesha”
(Mathayo 25:1-6) “Basi Ufalme wa mbinguni unaweza kufananishwa na mabikira kumi (10) wenye walikamata taa zao na kuenda kumupokea bwana-arusi. 2 Watano (5) kati yao walikuwa wapumbavu, na watano walikuwa wenye busara. 3 Kwa maana wale wapumbavu walibeba taa zao lakini hawakubeba mafuta ya kuongeza, 4 lakini wale wenye busara walibeba taa zao pamoja na mafuta katika chupa zao. 5 Wakati bwana-arusi alikawia kuja, wote walisinzia na kuanza kulala. 6 Katikati ya usiku kukatokea sauti kubwa: ‘Bwana-arusi anafika! Muende mumupokee.’
(Mathayo 25:7-10) Kisha wale mabikira wote wakasimama na kutayarisha taa zao. 8 Wale wapumbavu wakaambia wale wenye busara, ‘Mutupatie sehemu kidogo ya mafuta yenu, kwa sababu taa zetu zinakaribia kuzimika.’ 9 Wale wenye busara wakawajibu, na kusema: ‘Pengine hakutakuwa ya kutuenea sisi na ninyi. Lakini muende kwa wenye kuyauzisha, na mujinunulie yenu.’ 10 Wakati walikuwa wanaenda kununua mafuta, bwana-arusi akafika. Wale mabikira wenye walikuwa tayari wakaingia pamoja naye kwenye karamu ya ndoa, na mulango ukafungwa.
(Mathayo 25:11, 12) Kisha, wale mabikira wengine pia wakakuja, na kusema, ‘Bwana, Bwana, tufungulie!’ 12 Akawajibu, ‘Ninawaambia kweli, siwajue ninyi.’
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
Uendelee Kutegemeza Ndugu za Kristo kwa Uaminifu
Leo, tunaelewa muzuri zaidi mufano wa kondoo na mbuzi. Kuhusu ulizo ni nani wenye kuzungumuziwa katika mufano huo, Yesu ndiye “Mwana wa binadamu,” ni kusema, Mufalme. Wale wenye Yesu anaita “ndugu zangu,” ni wanaume na wanamuke wenye walitiwa mafuta kwa roho ili watawale pamoja na Kristo huko mbinguni. (Rom. 8:16, 17) “Kondoo” na “mbuzi,” wanafananisha watu wa mataifa yote. Watu hao hawakutiwa mafuta kwa roho takatifu. Hukumu itafanywa wakati gani? Hukumu hiyo itafanywa mbele ziki kubwa imalizike. Na sababu gani watu fulani watahukumiwa kuwa kondoo ao mbuzi? Watahukumiwa kulingana na namna watakuwa wamewatendea ndugu watiwa-mafuta wa Kristo wenye walikuwa wangali duniani. Kwa sababu mwisho wa ulimwengu huu unakaribia sana, tunashukuru sana kuona namna Yehova ametusaidia hatua kwa hatua kuelewa mufano wa kondoo na mbuzi, na mifano ingine yenye kupatikana katika Mathayo sura ya 24 na 25!
w09 15/10 uku. 16 fu. 16-18
“Ninyi Ni Rafiki Zangu”
Kama uko na tumaini la kuishi duniani chini ya Ufalme wa Mungu, namna gani unaweza kuonyesha urafiki wako kwa ndugu za Kristo? Tuchunguze njia tatu tu. Kwanza, kwa kushiriki kwa moyo wote katika kazi ya kuhubiri. Kristo alitolea ndugu zake amri ya kuhubiri habari njema katika ulimwengu wote. (Mt. 24:14) Lakini, ingekuwa nguvu sana kwa ndugu za Kristo wenye kuwa katika dunia leo kutimiza daraka hilo bila musaada wa wafanyakazi wenzao, ni kusema, kondoo wengine. Kila mara, wakati kondoo wengine wanashiriki katika kazi ya kuhubiri, wanasaidia ndugu za Kristo kutimiza kazi yao takatifu. Kristo na mutumwa mwaminifu na mwenye busara wanapendezwa sana na tendo hilo la urafiki.
Njia ya pili yenye kupitia hiyo kondoo wengine wanaweza kusaidia ndugu za Kristo ni kutegemeza kazi ya kuhubiri kwa kutoa feza zao. Yesu aliwatia moyo wafuasi wake wajifanyie marafiki na “mali zisizo za uadilifu.” (Luka 16:9) Haimaanishe kama tunaweza kununua kwa feza urafiki wa Yesu ao wa Yehova. Lakini, wakati tunatumia vitu vyetu vya kimwili ili kutegemeza kazi ya Ufalme, tunaonyesha urafiki na upendo wetu, hapana kwa maneno tu, lakini pia “kwa tendo na kweli.” (1 Yohana 3:16-18) Tunategemeza namna hiyo kwa kushiriki katika kazi ya kuhubiri, kwa kutoa michango ya feza ili kujenga na kutengeneza mahali petu pa ibada, na pia wakati tunatoa michango ya feza kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ya ulimwenguni pote. Hata kama tunatoa feza kidogo ao nyingi, tunajua kama Yehova na Yesu wanapendezwa sana wakati tunatoa kwa uchangamufu.—2 Kor. 9:7.
Njia ya tatu yenye sisi wote tunaweza kuonyesha kama tuko marafiki wa Kristo ni kutii muongozo wenye wazee wa kutaniko wanatutolea. Wanaume hao wamewekwa na roho takatifu chini ya muongozo wa Kristo. (Efe. 5:23) Mutume Paulo aliandika hivi: ‘Muwatii wale wanaongoza katikati yenu na munyenyekee.’ (Ebr. 13:17) Wakati mwengine, pengine tunaweza kuona kama ni jambo ngumu kutii muongozo wenye kutegemea Biblia wenye wazee wa kutaniko letu wanatutolea. Pengine tunajua uzaifu wao, na hilo linafanya tukuwe na mawazo ya mubaya kuhusu mashauri yao. Lakini, tukumbuke kama, Kristo, Kichwa cha kutaniko, anaendelea kupendezwa kutumia wanaume hao wenye hawakamilike. Kwa hiyo, urafiki wetu pamoja na Kristo unategemea namna tunaitikia mamlaka yao. Wakati tunafuata muongozo wa wazee kwa furaha kuliko kukazia makosa yao, tunaonyesha kama tunamupenda Kristo.