Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 6-12/08
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | LUKA 17-18
“Onyesha Shukrani”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Lu 17:12, 14
wanaume kumi wenye ukoma: Wakati wa zamani, inaonekana watu wenye walikuwa na ukoma walikuwa wanakutana pamoja ao walikuwa wanaishi katika vikundi ili waweze kusaidiana. (2Fal 7:3-5) Sheria ya Mungu ilisema kama watu wenye walikuwa na ukoma walipaswa kutengwa na wengine. Mutu mwenye alikuwa na ukoma alipaswa pia kuwaonya wengine kwa kulalamika: “Siko safi, siko safi” (Law 13:45, 46) Ili kuheshimia sheria, watu hao wenye walikuwa na ukoma walisimama mbali na Yesu. Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 8:2.
mujionyeshe kwa makuhani: Wakati Yesu alikuwa katika dunia, alikuwa pia chini ya Sheria. Kwa hiyo, alikubali kama ukuhani wa Haruni ulikuwa ungali unafanya kazi, na aliambia watu wenye aliponyesha ukoma waende kujionyesha kwa kuhani. (Mt 8:4; Mk 1:44) Kulingana na Sheria ya Musa, kuhani alikuwa na daraka la kuchunguza kama mutu fulani mwenye alikuwa na ukoma amepona. Kisha kupona, mutu huyo alipaswa kuenda kwenye hekalu na kutoa sadaka, ao zawadi ya ndege wawili wenye kuwa safi wenye ni wazima, muti wa mwerezi, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na hisopo.—Law 14:2-32.
w08 1/8 uku. 14-15 fu. 8-9
Sababu Gani Uonyeshe Shukrani?
Yesu, alipuuza kwamba wale wengine hawakuonyesha shukrani? Habari inaendelea hivi: “Yesu akajibu akasema: ‘Wote kumi walitakaswa, haiko vile? Basi, wale wengine kenda wako wapi? Je, hakuna mwingine mwenye alirudia ili kumutukuza Mungu isipokuwa mutu huyu wa taifa lingine?’”—Luka 17:17, 18.
Wale watu wengine kenda wenye walikuwa na ukoma hawakukuwa watu wabaya. Walionyesha waziwazi kama walikuwa na imani katika Yesu na walikuwa tayari kutii maagizo yake, na pia kusafiri kuenda Yerusalemu ili kujionyesha kwa makuhani. Lakini, hata kama walisamini sana tendo la Yesu la wema, hawakumuonyesha shukrani. Kristo hakufurahia jambo hilo. Halafu sisi? Tunazoea kusema aksanti wakati mutu anatutendea jambo la muzuri, na, wakati inafaa, tunaonyesha kama tunasamini jambo alitufanyia kwa kumutumia ujumbe mufupi wa shukrani?
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Lu 17:10
hawana mafaa yoyote: Neno kwa neno, “wenye hawako wa maana, wa bure.” Mufano huu wa Yesu haumaanishe kama watumwa, ni kusema wanafunzi wa Yesu, wanajiona kuwa watu wa bure, wenye hawana faida. Katika andiko hii maneno “hawana maana yoyote” inamaanisha kama watumwa walikuwa wanajishusha, hawakuwaza kama wanastahili pongezi ya pekee, ao kusifiwa. Wataalamu fulani wa Biblia wanasema kama maneno hayo, kulingana na namna inatumiwa katika andiko hii, inaweza kutafsiriwa “sisi ni watumwa tu wenye hawastahili sifa ya pekee.”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Lu 18:8
imani hii: Ao “imani ya namna hii.” Neno kwa neno “imani.” Neno la Kigiriki linatambulisha wazi kama Yesu hakuwa anazungumuzia imani kwa ujumla, lakini aina fulani ya imani ya pekee, kama ile ya mujane mwenye kuzungumuziwa katika mufano wa Yesu. Hilo lilimaanisha kuwa na imani katika uwezo wa sala, na kama Mungu atafanya haki itendewe kwa wachaguliwa wake. Pengine Yesu hakujibia ulizo kuhusu imani ili wanafunzi wake waendelee kufikiri juu ya aina ya imani yao. Mufano juu ya sala na imani ulikuwa wenye kufaa kabisa kwa sababu Yesu alikuwa amezungumuzia mateso yenye wanafunzi wake watapata.—Lu 17:22-37.
TAREHE 13-19/08
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | LUKA 19-20
“Tujifunze Kupitia Mufano wa Mina Kumi”
Mufano Wake wa Mina Kumi
Anasema: “Mutu fulani wa familia ya kifalme alisafiri kuenda inchi ya mbali ili afanywe kuwa mufalme na kisha arudie.” (Luka 19:12) Safari kama hiyo ilipaswa kuchukua wakati murefu. Bila shaka, Yesu ndiye ule “mutu wa familia ya kifalme” mwenye anasafiri kuenda “inchi ya mbali,” ni kusema, mbinguni, kwenye Baba yake atamupatia mamlaka ya ufalme.
Katika mufano huu, mbele aende, “mutu wa familia ya kifalme” anaita watumwa kumi na anapatia kila mumoja wao mina ya feza, na kuwaambia: “Mufanye nazo biashara mupaka wakati nitakuja.” (Luka 19:13) Mina ya feza iko na samani kubwa. Mina moja inalingana na mushahara wa miezi tatu wa mufanyakazi katika shamba.
Pengine wanafunzi wanatambua kwamba wanafananishwa na watumwa kumi hao wa mufano huo, kwa sababu Yesu amekwisha kuwafananisha na wafanyakazi katika mavuno. (Matayo 9:35-38) Bila shaka hakuwaomba walete mavuno ya nafaka. Lakini, mavuno hayo ni kuleta wanafunzi wengine wenye wanaweza kupata fasi katika Ufalme wa Mungu. Wanafunzi wanatumia kila kitu chenye wako nacho ili kutokeza wariti wengi wa Ufalme.
Mufano Wake wa Mina Kumi
Kama wanafunzi wanaelewa kwamba wako kama watumwa wenye walitumia kabisa kila kitu chenye wako nacho ili kufanya wanafunzi wengi zaidi, wanaweza kuendelea kuwa hakika kwamba Yesu atafurahi. Na wanaweza kutumainia kupata zawabu kwa sababu ya bidii ya namna hiyo. Bila shaka, wanafunzi wote wa Yesu hawako katika hali ileile ya maisha, ao hawana nafasi ao uwezo uleule. Lakini Yesu, mwenye alipewa ‘ufalme,’ atatambua na kubariki bidii yao ya kufanya wanafunzi—Matayo 28:19, 20.
Mufano Wake wa Mina Kumi
Kwa kushindwa kuongeza mali ya ufalme ya bwana wake, mutumwa huyo anapata shida. Mitume wanangojea kwa hamu wakati Yesu atatawala katika Ufalme wa Mungu. Kwa hiyo kupitia mambo yenye anasema kuhusu mutumwa huyo wa mwisho, pengine wanaelewa kwamba ikiwa hawatumike kwa bidii, hawatapata nafasi katika Ufalme huo.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Lu 19:43
ngome ya miti yenye kuchongwa: Ao “lupango ya miti.” Neno la Kigiriki khaʹrax linapatikana tu hapa katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Inasemekana kama ilikuwa “fimbo yenye kuchongoka ao nguzo yenye walitumia ili kujenga lupango katika eneo fulani; muti” na tena “kambi ao eneo la maaskari lenye wamejenga na miti; lupango ya miti.” Maneno ya Yesu ilitimia katika mwaka wa 70, wakati maaskari Waroma wenye kuongozwa na Titus, walijenga ukuta ao lupango ya miti ili kuzunguka muji wa Yerusalemu kwa ajili ya vita. Titus alikuwa na kusudi tatu: Kuzuia Wayahudi ili wasikimbie, kuwachochea wasipiganie muji wao, na kuwazuia ili wasipate chakula. Ili kupata vyombo kwa ajili ya kujenga ukuta huo, maaskari Waroma walikata miti yote ya pembeni-pembeni ya Muji wa Yerusalemu.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Lu 20:38
kwa maana kwake wote ni wazima: Ao “kwa maoni yake, wote wangali wazima.” Biblia inasema kama watu wenye wanaishi bila kumujua Mungu, kwa maoni yake wamekufa. Lakini, watumishi wake wenye wanakufa, kwa maoni yake wangali wazima, kwa sababu mupango wake wa kuwafufua utatimia kweli kweli.—Rom 4:16, 17.
TAREHE 20-26/08
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | LUKA 21-22
“Ukombozi Wenu Unakaribia”
Ufalme wa Mungu Unaondoa Maadui Wake
Mambo ya ajabu yataonekana katika mbingu. Yesu alitabiri hivi: “Jua litatiwa giza, nao mwezi hautatoa nuru yake, nazo nyota zitaanguka kutoka mbinguni.” Bila shaka, watu hawatatafuta tena nuru kutoka kwa viongozi wa dini, kwa sababu hawatakuwa tena viongozi. Yesu alikuwa anazungumuzia pia mambo fulani ya ajabu ambayo yatatukia katika mbingu? Pengine. (Isa. 13:9-11; Yoe. 2:1, 30, 31) Watu watafanya nini wakati wataona mambo hayo? Watapatwa na “maumivu makali” kwa sababu ‘hawatajua njia ya kutokea.’ (Lu. 21:25; Sef. 1:17) Bila shaka, maadui wa Ufalme wa Mungu, kuanzia kwa wafalme mupaka watumwa, ‘watazimia kwa woga na tarajio la mambo yanayokuja’ na watakimbia ili kuenda kutafuta mahali pa kujificha. Lakini hawatapata mahali penye usalama pa kujificha ili waepuke hasira ya Mufalme wetu.—Luka 21:26; 23:30; Ufu. 6:15-17.
Muazimie Kuendeleza “Upendo Wenu wa Kindugu”!
“Mukuwe hodari.” (Soma Waebrania 13:6.) Kumutegemea Yehova kunatupatia uhodari ao nguvu ya kuvumilia majaribu. Nguvu hiyo inatusaidia kuwa na maoni ya muzuri. Na wakati tunakuwa na maoni ya muzuri, tunaweza kuonyesha upendo wa kindugu kwa kutia moyo na kufariji ndugu na dada zetu. (1 Tes 5:14, 15) Hata wakati wa ziki kubwa, tunaweza kuwa na ujasiri, kwa sababu tunajua kama wokovu wetu unakaribia—Luka 21:25-28.
“Ukombozi Wenu Unakaribia”!
13 Wale wenye kufananishwa na mbuzi watafanya nini wakati watatambua kama wataharibiwa? ‘Watajipiga-piga kwa huzuni.’ (Mt 24:30) Lakini, Wakristo watiwa-mafuta na wale wenye kuwaunga mukono watafanya nini? Watafanya kulingana na maneno haya ya Yesu: ‘Wakati mambo haya yataanza kutokea, musimame wima na kuinua vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu unakaribia.’—Luka 21:28.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Lu 21:33
Mbingu na dunia zitapita: Maandiko ingine inasema kama mbingu na dunia zitaendelea kuwa milele. (Mwa 9:16; Zab 104:5; Mhu 1:4) Kwa hiyo pengine Yesu alitumia maneno ya kutia chumvi, yenye kumaanisha kwamba hata kama mbingu na dunia zinapita, jambo lenye haliwezi kutendeka, maneno yake inapaswa kutimia. (Linganisha na Mt 5:18.) Lakini, pengine katika andiko hii, mbingu na dunia zinaweza pia kumaanisha mbingu na dunia za mufano zenye katika Ufunuo 21:1 zinaitwa “mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza.”
maneno yangu hayatapita hata kidogo: Ao “kwa kweli maneno yangu hayatapita.” Kutumia maneno mbili ya Kigiriki yenye kuonyesha kukataa, hilo linaonyesha wazi kama wazo linakataliwa kabisa na kama maneno ya Yesu itatimia kabisa kabisa.
w14 15/10 uku. 16-17 fu. 15-16
Mutakuwa “Ufalme wa Makuhani”
Kisha kuanzisha tukio lenye linaitwa Chakula cha Mangaribi cha Bwana, Yesu alifanya agano pamoja na mitume wake waaminifu. Agano hilo linaitwa agano la Ufalme. (Soma Luka 22:28-30.) Maagano yenye tumezungumuzia ilifanywa na Yehova. Lakini agano la Ufalme ni agano lenye Yesu anafanya pamoja na wafuasi wake watiwa-mafuta. Wakati Yesu alisema, “kama vile Baba yangu alifanya agano pamoja na mimi,” inawezekana alikuwa anazungumuzia agano lenye Yehova alifanya pamoja naye ili kuwa ‘kuhani milele kwa mufano wa Melkisedeki.’—Ebr. 5:5, 6.
Mitume waaminifu 11 ‘walishikamana na Yesu katika majaribu yake.’ Agano la Ufalme liliwahakikishia kama watakuwa pamoja naye huko mbinguni na kama watakaa kwenye viti vya ufalme ili kuwa wafalme na makuhani. Hata hivyo, haiko wale 11 tu ndio watapewa pendeleo hilo. Wakati Yesu mwenye utukufu alimutokea mutume Yohana katika maono, alimuambia hivi: ‘Ule mwenye atashinda nitamupatia ruhusa ya kukaa pamoja na mimi kwenye kiti changu cha ufalme, kama vile nilipata ushindi na nikakaa pamoja na Baba yangu kwenye kiti chake cha ufalme.’ (Ufu. 3:21) Kwa hiyo, Yesu anafanya agano la Ufalme pamoja na Wakristo watiwa-mafuta 144000 tu. (Ufu. 5:9, 10; 7:4) Agano hilo ni musingi wa kisheria wenye unawaruhusu kutawala pamoja na Yesu mbinguni. Ni kama bibi arusi mwenye anatoka katika familia tajiri na kuolewa na mufalme mwenye anatawala. Kisha kuolewa, ule bibi arusi anakuwa na mamlaka katika utawala wa ule mufalme. Kwa mufano, Biblia inaita Wakristo watiwa-mafuta “bibi-arusi” wa Kristo, “bikira mwenye kuwa na mwenendo safi” mwenye anachumbiwa na Kristo.—Ufu. 19:7, 8; 21:9; 2 Kor. 11:2.
TAREHE 27/08–2/09
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | LUKA 23-24
“Ukuwe Tayari Kusamehe Wengine”
cl uku. 297 fu. 16
“Kuujua Upendo wa Kristo”
Yesu aliiga kabisa upendo wa Baba yake katika njia ingine ya maana: alikuwa “tayari kusamehe.” (Zaburi 86:5) Jambo hilo lilionekana wazi hata wakati alikuwa kwenye muti wa mateso. Mbele akufe kifo cha haya, wakati alipigiliwa misumari kwenye mikono na miguu, Yesu alisema nini? Alimulilia Yehova awape malipizi wale wenye walikuwa wanamutesa? Hapana, hata kidogo! Maneno haya ni kati ya maneno yake ya mwisho: “Baba, uwasamehe, kwa maana hawajue jambo lenye wanafanya.”—Luka 23:34.
g 2/08 uku. 11 fu. 5-6
Je, Mungu Anasamehe Zambi Nzito?
Yehova haangalie tu zambi yenye ilifanywa, lakini anaangalia pia mutazamo wa mutenda-zambi. (Isaya 1:16-19) Wazia kidogo watenda-maovu wawili wenye walitundikwa pembeni ya Yesu. Ni wazi kama wote wawili walikuwa wamefanya makosa makubwa, kwa sababu mumoja wao alisema: “Sisi tunastahili kutendewa hivi, kwa maana tunapewa azabu kupatana na makosa yenye tulifanya; lakini mutu huyu [Yesu] hakufanya jambo lolote la mubaya.” Maneno ya huyo mutenda-maovu inaonyesha kama alijua jambo fulani kuhusu Yesu. Pengine ujuzi huo ulibadilisha namna yake ya kuona mambo. Jambo hilo linaonyeshwa katika maneno yake yenye kufuata, wakati alimusihi Yesu hivi: “Unikumbuke wakati utaingia katika Ufalme wako.” Yesu alifanya nini kuhusu ombi hilo lenye lilitoka katika moyo? Yesu alimuambia, “Kwa kweli ninakuambia leo, utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.”—Luka 23:41-43.
Fikiria kidogo jambo hilo: Maneno ya mwisho ya Yesu ilikuwa pia kuonyesha rehema mutu mwenye alikubali kama amefanya jambo lenye lilifanya astahili kifo. Hilo linatia moyo kabisa! Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama Yesu Kristo na Baba yake, Yehova, wataonyesha rehema wote wenye wanatubu kwelikweli hata kama wamefanya makosa gani wakati wenye ulipita.—Waroma 4:7.
cl uku. 297-298 fu. 17-18
“Kujua Upendo wa Kristo”
Pengine hali ya mutume Petro inaonyesha kwa njia yenye kugusa moyo hata zaidi namna Yesu alikuwa mwenye kusamehe. Ni wazi kama Petro alimupenda sana Yesu. Siku ya Nisani 14, usiku wa mwisho mbele wamuue Yesu, Petro alimuambia hivi: “Bwana, niko tayari kuenda na wewe katika gereza na katika kifo.” Lakini, kisha wakati kidogo tu, Petro alikana mara tatu kumujua Yesu! Biblia inaonyesha jambo lenye lilitokea wakati Petro alikuwa anamukana mara ya tatu: “Bwana akageuka na kumuangalia Petro moja kwa moja.” Petro alisikitika sana kwa sababu ya zambi yake, mupaka “akaenda inje na kulia kwa uchungu.” Kisha, siku hiyo wakati Yesu alikufa, pengine mutume Petro alijiuliza hivi: ‘Bwana wangu alinisamehe kabisa?’—Luka 22:33, 61, 62.
Petro hakukawia kupata jibu. Yesu alifufuliwa asubuhi ya Nisani 16, na inaonekana kama alimutembelea Petro siku ileile. (Luka 24:34; 1 Wakorinto 15:4-8) Sababu gani Yesu aliendelea kushikamana na huyo mutume mwenye alikuwa amemukana kabisa? Pengine Yesu alitaka kumuhakikishia Petro mwenye alitubu kama angali anamupenda na kumuona kuwa wa lazima. Lakini Yesu alimuhakikishia jambo hilo kwa njia ingine.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Lu 23:31
wakati muti ni mubichi, . . . wakati utakuwa umekauka: Pengine Yesu anazungumuzia taifa la Wayahudi. Taifa hilo lilikuwa kama muti wenye kufa wenye ulikuwa ungali na sehemu fulani zenye kuwa mubichi, kwa sababu Yesu alikuwa pale na kulikuwa Wayahudi fulani wenye walimuamini. Lakini, karibuni wangemuua, na Wayahudi waaminifu wangetiwa mafuta na roho takatifu na kuwa sehemu ya Israeli ya kiroho. (Rom 2:28, 29; Gal 6:16) Wakati huo, taifa la Israeli ya kimwili lingekufa kiroho, kama vile muti wenye kukauka.—Mt 21:43.
nwtsty picha na video
Musumari Ndani ya Mufupa wa Kisingino
Picha ya mufupa wa kisingino cha mutu wenye kutobolewa na musumari wa chuma wenye urefu wa santimetre 11.5. Mufupa wenye ulivumbuliwa katika mwaka wa 1968, wakati walikuwa wanatafuta vitu vya zamani katika udongo huko Yerusalemu, ni wa wakati wa Waroma. Kuvumbula mufupa huo kunaonyesha kama pengine wakati walitundika mutu kwenye muti walitumia misumari. Pengine musumari huo unafanana na ule wenye maaskari walitumia ili kumutundika Yesu Kristo kwenye muti. Waliupata katika sanduku moja la majiwe lenye kuitwa sanduku la mifupa, mwenye walikuwa wanaweka mifupa ya mutu kisha mwili wake kuoza. Jambo hilo linaonyesha kama mutu mwenye alitundikwa kwenye muti alikuwa anazikwa katika kaburi.