Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 1-7/10
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOHANA 9-10
“Yesu Anahangaikia Kondoo Wake”
nwtsty picha na video
Zizi la kondoo
Zizi la kondoo ilikuwa lupango yenye ilijengwa ili kulinda kondoo wasiibwe ao wasishambuliwe na wanyama wa makali. Usiku, wachungaji walikuwa wanaingiza makundi yao katika zizi la kondoo ili kuwalinda. Wakati wa zamani, mazizi ya kondoo haikufunikwa juu, na ilikuwa na umbo na ukubwa mbalimbali, kwa kawaida ilijengwa kwa majiwe na ilikuwa tu na mulango moja. (Hes 32:16; 1Sa 24:3; Sef 2:6) Yohana anazungumuzia kuingia katika zizi la kondoo “kupitia kwenye mulango,” wenye ulilindwa na “mulinzi wa mulango.” (Yoh 10:1, 3) Mahali kwenye kulikuwa wachungaji wengi, usiku makundi mingi ililindwa pamoja, na mulinzi wa mulango alikuwa anakesha ili kulinda kondoo. Asubui, mulinzi wa mulango alikuwa anafungulia wachungaji mulango. Kila muchungaji alikuwa anakusanya kundi lake kwa kuita kondoo wake, na kondoo walikuwa wanatambua sauti ya muchungaji wao na kumufuata. (Yoh 10:3-5) Yesu alizungumuzia zoezi hilo ili kuonyesha namna alihangaikia wanafunzi wake.—Yoh 10:7-14.
Familia za Kikristo—‘Mukae Macho’
5 Kwa njia ya mufano, uhusiano kati ya muchungaji na kondoo wake unategemea ujuzi na kuaminiana. Muchungaji anajua kila jambo juu ya kondoo wake, na kondoo wanamujua na kumuamini muchungaji wao. Wanatambua sauti yake na kuitii. Yesu alisema hivi: “Ninawajua kondoo wangu na kondoo wangu wananijua.” Yesu hana ujuzi wa juu-juu tu kuhusu kutaniko. Neno la Kigiriki lenye limetafsiriwa ‘kujua’ liko na maana ya “ujuzi wa ndani sana juu ya mutu kipekee.” Ndiyo, ule Muchungaji Mwema anajua kondoo wake kipekee. Anajua mahitaji, uzaifu, na sifa za muzuri za kila mumoja wao. Yesu, mwenye ni Mufano wetu, anaona kila jambo juu ya kondoo wake. Na kondoo wake wanamujua muzuri kabisa muchungaji wao na wanaamini uongozi wake.
cf uku. 124-125 fu. 17
“Hakukuwa Anasema Nao Bila Mufano”
17 Kulingana na mambo yenye alijionea, George A. Smith aliandika hivi mu kitabu chake The Historical Geography of the Holy Land: “Mara kwa mara tulifurahia kupumuzika muchana pembeni ya kisima kimoja kati ya visima vya Yudea, kwenye wachungaji tatu ao ine walikuwa wanaleta kondoo wao. Kondoo wao walichangana-changana; kwa hiyo tulijiuliza kama kila muchungaji angetambua namna gani kondoo wake. Lakini wakati kondoo walimaliza kunywa maji na kucheza, kila muchungaji alienda upande tofauti wa bonde hilo, na kila mumoja aliita kondoo wake kwa sauti yenye wangetambua; kisha kondoo walijitenga na kondoo wengine na wakaanza kufuata wachungaji wao kwa utaratibu kulingana na namna walikuja.” Yesu alichagua mufano wenye kufaa zaidi ili kukazia wazo lake, ni kusema, kama tunatambua mafundisho yake na kuitii, na kama tunafuata mwongozo wake, tutatunzwa na “muchungaji mwema.”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 10:16
niwalete: Ao “niwaongoze.” Neno la Kigiriki aʹgo lenye kutumiwa hapa linaweza kuwa na maana ya “kuleta (ndani)” ao “kuongoza,” kulingana na habari yenye kuzungumuziwa. Maandishi fulani ya Kigiriki ya miaka ya 200 hivi Kisha Kuzaliwa kwa Yesu inatumia neno lingine la Kigiriki (sy·naʹgo) lenye mara mingi linatafsiriwa “kukusanya.” Kwa sababu Yesu ni Muchungaji Mwema, anakusanya, anaongoza, analinda, na analisha kondoo wa zizi hili (wenye kuitwa pia “kundi ndogo” mu Lu 12:32) na pia kondoo wengine wake. Kondoo hao wanakuwa kundi moja yenye kuongozwa na muchungaji mumoja. Hii maneno ya mufano inakazia umoja wenye wanafunzi wa Yesu wangekuwa nao.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 9:38
akainama mbele yake: Ao “akamuinamia; akaanguka mbele ya miguu yake; akamupatia heshima.” Wakati neno la Kigiriki pro·sky·neʹo linatumiwa katika maana ya kutolea ibada mungu fulani, linatafsiriwa “kuabudu.” (Mt 4:10; Lu 4:8) Lakini, hapa, mwanaume mwenye aliponyeshwa, mwenye alizaliwa kipofu, alitambua kama ni Mungu alimutuma Yesu na akainama mbele yake. Hakumuona kama Mungu, lakini kama “Mwana wa binadamu,” mwenye alitabiriwa, Masiya mwenye Mungu alipatia mamlaka. (Yoh 9:35) Wakati aliinama mbele ya Yesu, pengine aliiga watu wenye kutajwa mu Maandiko ya Kiebrania. Waliinama wakati walikutana na manabii, wafalme, ao watumishi wengine wa Mungu. (1Sa 25:23, 24; 2Sa 14:4-7; 1Fa 1:16; 2Fa 4:36, 37) Mara mingi, watu wenye waliinama mbele ya Yesu walionyesha shukrani kwa sababu waliona nguvu ya Mungu ao kwa sababu aliwakubali.—Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 2:2; 8:2; 14:33; 15:25.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 10:22
Sikukuu ya Kumutolea Mungu Hekalu: Jina la Kiebrania la sikukuu hiyo ni Hanukkah (chanuk·kahʹ), maana yake “Kuzinduliwa (Inauguration); Kutolea.” Ilikuwa inafanya siku 8, kuanzia siku ya 25 ya mwezi wa Kislevu, karibu na wakati muchana unaanza kuwa murefu, (ona kwa ajili ya funzo kuhusu wakati wa majira ya baridi kali mu Yoh 10:22 na Nyongeza B15) ili kukumbuka kutolewa tena kwa hekalu ya Yerusalemu kwa Mungu mu mwaka wa 165 Mbele ya Kuzaliwa kwa Yesu. Mufalme wa Siria Antiochus IV Épiphane alionyesha kama anamuzarau Yehova, Mungu wa Wayahudi, kwa kuchafua hekalu Yake. Kwa mufano, alijenga mazabahu yake juu ya mazabahu ya Yehova, nafasi kwenye zabihu za kuteketezwa zilikuwa zinatolewa. Siku ya 25, mwezi wa Kislevu, mwaka wa 168 Mbele ya Kuzaliwa kwa Yesu, ili kuchafua kabisa hekalu ya Yehova, Antiochus alitoa nguruwe kwenye ile mazabahu na aliomba muchuzi ya nyama ya nguruwe isambazwe fasi yote katika hekalu. Alilunguza milango ya hekalu, alibomoa vyumba vya makuhani, na alibeba mazabahu ya zahabu, meza ya mukate wa wonyesho, na kinara cha taa cha zahabu. Kisha akakamata hekalu ya Yehova na akaitolea Zeu, mungu mupagani wa Olympe. Kisha miaka mbili, Judas Maccabée akakamata tena muji na hekalu. Kisha kusafisha hekalu, ikatolewa tena kwa Mungu siku ya 25, mwezi wa Kislevu, mwaka wa 165 Mbele ya Kuzaliwa kwa Yesu, miaka tatu kisha Antiochus kufanya toleo lenye kuchukiza kwenye mazabahu hiyo kwa ajili ya Zeu. Kisha wakaanza tena kumutolea Yehova zabihu za kuteketezwa kwenye ile mazabahu kila siku. Katika Maandiko yenye iliongozwa na roho, hakuna hata fasi moja kwenye inaandikwa kama Yehova alimupatia Judas Maccabée ushindi na alimuongoza ili ajenge upya hekalu. Lakini, Yehova alikuwa ametumia watu wa mataifa ingine, kama vile Cyrus wa Perse, ili kutimiza mipango yake fulani juu ya ibada Yake. (Isa 45:1) Kwa hiyo, ni jambo lenye kufaa tuseme kama Yehova anaweza kutumia mumoja kati ya watu wenye kujitoa kwake ili kutimiza mapenzi Yake. Maandiko inaonyesha kama hekalu ilipaswa kusimama na kutumika ili unabii mbalimbali juu ya Masiya, kazi yake ya kuhubiri, na namna angetoa uzima wake utimie. Tena, zabihu zenye kuzungumuziwa mu kitabu cha Mambo ya Walawi zilipaswa kutolewa mupaka wakati Masiya angetoa zabihu kubwa zaidi, ni kusema, uzima wake kwa ajili ya wanadamu. (Da 9:27; Yoh 2:17; Ebr 9:11-14) Wanafunzi wa Yesu hawakukuwa wanafanya Sikukuu ya Kumutolea Mungu Hekalu. (Kol 2:16, 17) Lakini, hakuna fasi hata moja kwenye kunaandikwa kama Yesu ao wanafunzi wake walihukumu wale wenye walifanya Sikukuu hiyo.
TAREHE 8-14/10
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOHANA 11-12
“Uige Sifa ya Yesu ya Kusikilia Wengine Huruma”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 11:24, 25
Ninajua atafufuka: Marta aliwaza kama Yesu alikuwa anazungumuzia ufufuo wa wakati wenye kuja, wa siku ya mwisho. (Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 6:39.) Alikuwa na imani kubwa sana katika fundisho la ufufuo. Viongozi fulani wa dini wa wakati wake, wenye waliitwa Masadukayo, hawakuamini kama kutakuwa ufufuo, hata kama jambo hilo linaonyeshwa wazi mu Maandiko. (Da 12:13; Mr 12:18) Kwa upande mwingine, Mafarisayo waliamini kama wakati mutu anakufa nafsi yake inaendelea kuishi. Lakini, Marta alijua kama Yesu alifundisha tumaini la ufufuo na kama alifikia hata kufufua watu, hata kama kati ya watu hao wote hakuna mwenye alikuwa amefanya siku mingi mu kaburi kama Lazaro.
Mimi ndiye ufufuo na uzima: Kifo cha Yesu mwenyewe na ufufuo wake ulitolea watu wenye kufa nafasi ya kuishi tena. Kisha Yesu kufufuliwa, Yehova alimupatia uwezo wa kufufua watu wenye wamekufa na pia kuwapatia uzima wa milele. (Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 5:26.) Kwenye Ufu 1:18, Yesu anajiita “mwenye kuishi,” mwenye iko na “funguo za kifo na za Kaburi.” Kwa hiyo, Yesu ni tumaini kwa ajili ya wazima na wale wamekufa. Aliahidi kufungua makaburi na kupatia uzima wale wamekufa, iwe mbinguni ili watawale pamoja naye ao mu dunia hii yenye itatawaliwa na guvernema yake ya mbinguni.—Yoh 5:28, 29; 2Pe 3:13.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 11:33-35
akilia: Ao “kumwanga machozi.” Neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa “akilia” mara mingi liko na maana ya kulia kwa sauti. Neno hilohilo linatumiwa juu ya Yesu wakati alitabiri kuharibiwa kwa Yerusalemu kwenye kungetokea.—Lu 19:41.
akilia . . . akasumbuka sana: Kutumiwa pamoja kwa hii maneno mbili kunaonyesha namna Yesu anajisikia mubaya sana wakati huo. Tendo la Kigiriki lenye kutafsiriwa “akilia” (em·bri·maʹo·mai) linaonyesha mara mingi hisia kubwa, lakini hapa linaonyesha kama Yesu alisumbuka sana mupaka akalia. Maneno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “akasumbuka sana” (ta·rasʹso) inamaanisha neno kwa neno kuwa na wasiwasi. Kulingana na mutu moja mwenye elimu ya Biblia, hapa hii maneno iko na maana ya “kuvurugika sana katika roho; maumivu makubwa ao huzuni nyingi.” Tendo lilelile linatumiwa kwenye Yoh 13:21 ili kuzungumuzia namna Yesu anajisikia wakati anawazia namna Yuda atamutoa.—Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 11:35.
ndani yake: Neno kwa neno, “katika roho.” Neno la Kigiriki pneuʹma linatumiwa hapa pengine katika maana ya nguvu yenye kuchochea yenye kutoka mu moyo wa mufano wa mutu na inamufanya aseme ao afanye mambo kwa njia fulani.—Ona Maana ya Maneno, “Roho.”
akatokwa na machozi: Neno lenye kutumiwa hapa (da·kryʹo) ni tendo la neno la Kigiriki lenye kuwa na maana ya “machozi” lenye kutumiwa mu Maandiko kama vile Lu 7:38; Mdo 20:19, 31; Ebr 5:7; Ufu 7:17; 21:4. Inaonekana wanakazia zaidi sana kumwanga machozi kuliko kulia kwa sauti. Mu Maandiko yote ya Kigiriki ya Kikristo, ni hapa tu tendo hili la Kigiriki linatumiwa, na liko tofauti na lile lenye kutumiwa mu Yoh 11:33 (ona kwa ajili ya funzo) ili kuzungumuzia namna Maria na Wayahudi walilia. Yesu alijua kama atamufufua Lazaro, lakini kuona marafiki wake wanalia kulimuletea huzuni mingi. Kwa sababu alipenda sana marafiki wake, alimwanga machozi waziwazi. Habari hii inaonyesha wazi kama alihangaikia sana wale wenye walipoteza wapendwa wao kwa sababu ya zambi ya Adamu.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 11:49
kuhani mukubwa: Wakati Israeli ilikuwa taifa huru, kuhani mukubwa alitumikia cheo hicho maisha yake yote. (Hes 35:25) Lakini, wakati Waroma walitawala Israeli, watawala Waroma walikuwa na mamlaka ya kuweka ao kuondoa kuhani mukubwa. (Ona Maana ya Maneno, “Kuhani Mukubwa.”) Kayafa, mwenye Waroma waliweka, alijua sana kufanyiza uhusiano muzuri na watu wengine, na aliendelea kuwa kuhani mukubwa wakati murefu zaidi kuliko makuhani wakubwa wengine wote wenye waliwekwa kisha yeye. Aliwekwa mu mwaka wa 18 hivi Kisha Kuzaliwa kwa Yesu na alitumikia cheo hicho mupaka mwaka wa 36 hivi Kisha Kuzaliwa kwa Yesu. Wakati anasema kama Kayafa alikuwa kuhani mukubwa mwaka huo, ni kusema mwaka wa 33 kisha kuzaliwa kwa Yesu, pengine Yohana alipenda kusema kama miaka ya Kayafa ya kuwa kuhani mukubwa ilitia ndani mwaka wenye walimuua Yesu.—Ona Nyongeza B12 ili kujua mahali kwenye pengine nyumba ya Kayafa ilikuwa.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 12:42
watawala: Hapa, inaonekana neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa “watawala” linahusu washiriki wa tribinali kubwa ya Wayahudi, ni kusema, Sanhedrini. Neno hilo linatumiwa mu Yoh 3:1 ili kuzungumuzia Nikodemo, mumoja wa washiriki wa tribinali hiyo.—Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 3:1.
wasifukuzwe katika sinagogi: Ao “wasitengwe; wasiwakatalie kuingia katika sinagogi.” Neno la Kigiriki a·po·sy·naʹgo·gos linatumiwa tu hapa na mu Yoh 12:42 na 16:2. Watu walikuwa wanamuzarau na kumuepuka mutu mwenye alifukuzwa katika sinagogi. Kutenga mutu na Wayahudi wengine kulipaswa kuletea mutu huyo na familia yake magumu makubwa ya feza. Sinagogi, zenye zilitumiwa zaidi sana ili kufundisha watu, zilitumiwa pia kwa kiasi fulani kama tribinali ndogo zenye zilikuwa na mamlaka ya kuhukumu mutu apigwe fimbo na kutengwa na wengine.—Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 10:17.
TAREHE 15-21/10
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOHANA 13-14
“Niliwawekea Ninyi Mufano”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 13:5
kunawisha wanafunzi miguu: Mu Israeli ya zamani, watu wengi walivaa sapatu (sandale), ni kusema, viatu vyenye vilikuwa na sehemu ya chini na kamba za kufungia kwenye muguu na kwenye kifundo cha muguu (cheville). Kwa sababu barabara na mashamba ilikuwa na vumbi ao matope, miguu ya watu ilichafuka. Kwa hiyo, watu walikuwa wanatosha viatu hivyo mbele ya kuingia ndani ya nyumba, na wenye-nyumba wenye walikuwa wakaribishaji wazuri walikuwa wananawisha miguu ya wageni wao. Biblia inataja mara mingi zoezi hiyo. (Mwa 18:4, 5; 24:32; 1Sa 25:41; Lu 7:37, 38, 44) Wakati Yesu alinawisha miguu ya wanafunzi wake, alitumia zoezi hiyo ili kuwafundisha wakuwe wanyenyekevu na watumikiane.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 13:12-14
munapaswa: Ao “lazima mufanye hivyo.” Tendo la Kigiriki lenye kutumiwa hapa linatumiwa mara mingi katika mambo ya feza, na kwa kawaida liko na maana ya “kuwa na deni ya mutu fulani; deni ya kupatia mutu kitu fulani.” (Mt 18:28, 30, 34; Lu 16:5, 7) Hapa na mahali pengine, linatumiwa katika maana pana ya kulazimika ao kulazimishwa kufanya jambo fulani.—1Yo 3:16; 4:11; 3Yo 8.
w99 1/3 uku. 31 fu. 1
Ule Mutu Mukubwa Zaidi Anafanya Kazi ya Unyenyekevu
Kwa kunawisha miguu ya wanafunzi wake, Yesu alifundisha somo ya lazima sana juu ya unyenyekevu. Ni wazi kama Wakristo hawapaswe kufikiri kama wao ni wa maana sana na kwa hiyo wengine wanapaswa kuwatumikia sikuzote, wala hawapaswe kutafuta sifa na kujulikana sana. Lakini, wanapaswa kufuata mufano wa Yesu, mwenye “hakukuja ili watu wamutumikie, lakini ili yeye atumikie wengine na atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.” (Matayo 20:28) Kwa hiyo, wanafunzi wa Yesu wanapaswa kuwa tayari kufanyiana kazi za hali ya chini zaidi.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 14:6
Mimi ndiye njia na kweli na uzima: Yesu ni njia kwa sababu ni kupitia yeye tu ndiyo tunaweza kumukaribia Mungu katika sala. Ni “njia” pia ili wanadamu waunganishwe tena na Mungu. (Yoh 16:23; Ro 5:8) Yesu ni kweli kwa sababu alisema na kuishi kulingana na kweli. Alitimiza pia unabii mbalimbali wenye ulionyesha daraka lake kubwa katika kutimizwa kwa mipango ya Mungu. (Yoh 1:14; Ufu 19:10) Unabii huo umekuwa “‘ndiyo’ [ao ulitimia] kupitia yeye.” (2Ko 1:20) Yesu ni uzima kwa sababu kupitia zabihu ya ukombozi, aliwezesha wanadamu wapate “uzima wa kwelikweli,” ni kusema, “uzima wa milele.” (1Ti 6:12, 19; Efe 1:7; 1Yo 1:7) Atajionyesha pia kuwa “uzima” kwa mamilioni ya watu wenye watafufuliwa na tumaini la kuishi milele mu Paradiso.—Yoh 5:28, 29.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 14:12
kazi kubwa kuliko hizi: Yesu haseme kama miujiza yenye wanafunzi wake wangefanya ingekuwa ya mukubwa zaidi kuliko miujiza yenye yeye alifanya. Lakini, anatambua kwa unyenyekevu kama kazi ya kuhubiri na kufundisha yenye wanafunzi wake wangefanya ingekuwa kubwa zaidi kuliko yake. Wanafunzi wake wangehubiri katika eneo kubwa zaidi, wangepata watu wengi zaidi, na wangehubiri wakati murefu zaidi kuliko yeye. Maneno ya Yesu inaonyesha wazi kama alipenda wanafunzi wake waendeleshe kazi yenye alianzisha.
TAREHE 22-28/10
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOHANA 15-17
“Ninyi Hamuko Sehemu ya Ulimwengu”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 15:19
ulimwengu: Hapa, neno la Kigiriki koʹsmos liko na maana ya ulimwengu wa wanadamu wenye hawamutumikie Mungu, wanadamu wenye kukosa haki wenye wamejitenga na Mungu. Kati ya waandikaji wa Injili ni Yohana tu ndiye anataja maneno ya Yesu yenye kusema kama wanafunzi wake hawako sehemu ya ulimwengu ao hawako wa ulimwengu. Wazo hilo linapatikana tena mara mbili mu sala ya mwisho ya Yesu yenye alitoa kwa ajili ya mitume wake waaminifu.—Yoh 17:14, 16.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 15:21
kwa sababu ya jina langu: Mu Biblia, wakati fulani neno “jina” liko na maana ya mutu mwenye kuitwa kwa jina hilo, sifa yake, na mambo yote yenye kumuhusu. (Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 6:9.) Kuhusu jina la Yesu, liko pia na maana ya mamlaka na cheo yenye Baba yake amemupatia. (Mt 28:18; Flp 2:9, 10; Ebr 1:3, 4) Hapa Yesu anaeleza sababu gani watu wa ulimwengu wangetesa wanafunzi wake: kwa kuwa hawajue Ule mwenye alimutuma. Kumujua Mungu kungewasaidia kuelewa na kutambua maana ya jina la Yesu. (Mdo 4:12) Hilo lingekuwa pia na maana ya cheo ya Yesu, Mufalme mwenye Mungu amechagua, Mufalme wa wafalme, mwenye watu wote wanapaswa kujitiisha kwake ili wapate uzima wa milele.—Yoh 17:3; Ufu 19:11-16; linganisha na Zb 2:7-12.
it-1 uku. 555
Uhodari
Wakristo wanapaswa kuonyesha uhodari ili wasiige tabia na matendo ya watu wa ulimwengu wenye kujitenga na Mungu na wabakie washikamanifu kwake hata kama ulimwengu unawachukia. Yesu Kristo aliambia wanafunzi wake: “Katika ulimwengu mutapata taabu, lakini musiogope! Mimi nimeshinda ulimwengu.” (Yoh 16:33) Mwana wa Mungu hakuacha ulimwengu umuchochee, lakini alipata ushindi juu ya ulimwengu kwa kukataa kuufanana hata katika hali moja. Mufano mukubwa wa Yesu wa kupata ushindi juu ya ulimwengu na namna yake ya kuishi yenye haikukuwa na makosa inaweza kutupatia uhodari wenye tuko nao lazima ili kumuiga kwa kuendelea kujitenga na ulimwengu na kukataa kuiga tabia na matendo ya watu wa ulimwengu.—Yoh 17:16.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 17:21-23
kitu kimoja: Ao “mu umoja.” Yesu alisali ili wanafunzi wake wakuwe “kitu kimoja,” watumike pamoja kwa umoja kwa kusudi moja, kama vile tu yeye na Baba yake wako “kitu kimoja,” na wako na mawazo yenye kupatana na yenye umoja. (Yoh 17:22) Mu 1Ko 3:6-9, Paulo anataja umoja huo wa Wakristo wa kweli wakati wanatumika kati yao, na pamoja na Mungu.—Ona 1Ko 3:8 na kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 10:30; 17:11.
wakamilishwe katika umoja: Ao “waunganishwe kikamili.” Hapa, Yesu anapatanisha kukamilishwa katika umoja na kupendwa na Baba. Jambo hilo linapatana na Kol 3:14, yenye inasema: “Upendo . . . ni kifungo kikamilifu cha umoja.” Umoja huo uko na mipaka. Ni kusema, sisi wanafunzi wa Yesu tunaendelea kuwa tofauti mu mambo kama vile uwezo, tabia, na zamiri. Lakini tunaungana mu matendo, imani, na mafundisho.—Ro 15:5, 6; 1Ko 1:10; Efe 4:3; Flp 1:27.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 17:24
kuwekwa kwa musingi wa ulimwengu: Neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa “musingi” linatafsiriwa “kupata uzao” mu Ebr 11:11, kwenye linatumiwa kuhusu “uzao.” Hapa, inaonekana wazi kama kwa kutumiwa pamoja na maneno “musingi wa ulimwengu,” pengine liko na maana ya watoto wenye Adamu na Eva walizaa. Yesu anapatanisha “kuwekwa musingi wa ulimwengu” na Abeli, mwenye pengine alikuwa mwanadamu wa kwanza mwenye jina lake ‘liliandikwa katika kitabu cha kukunjwa cha uzima tangu kuwekwa musingi wa ulimwengu.’ (Lu 11:50, 51; Ufu 17:8) Maneno haya ya Yesu katika sala kwa Baba yake inaonyesha pia kama tangu zamani sana, mbele Adamu na Eva wazae watoto, Mungu alimupenda Mwana muzaliwa-pekee wake.
TAREHE 29/10–4/11
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOHANA 18-19
“Yesu Alitoa Ushahidi juu ya ile Kweli”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 18:37
nitoe ushahidi: Kulingana na namna inatumiwa mu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, maneno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “kutoa ushahidi” (mar·ty·reʹo) na “shahidi” (mar·ty·riʹa; marʹtys) iko na maana pana. Hii maneno yote mbili inatumiwa katika maana ya kutoa ushuhuda wa mambo yenye kujulikana, lakini inaweza pia kuwa na wazo la “kutangaza; kuhakikisha; kusema muzuri juu ya.” Yesu alitoa ushuhuda na alitangaza kweli zenye alikuwa nazo hakika, lakini pia maisha yake ilitimiza unabii mbalimbali wa Neno la Mungu na mipango ya Baba yake. (2Ko 1:20) Mipango ya Mungu juu ya Ufalme, na Masiya Mufalme wake ilitabiriwa hata katika mambo madogo-madogo. Maisha yote ya Yesu mu dunia, mupaka wakati alijitoa na kufa, ilitimiza unabii wote juu yake, na pia mambo yote, ao mifano, yenye kupatikana katika agano la Sheria. (Kol 2:16, 17; Ebr 10:1) Kwa hiyo, tunaweza kusema kama kupitia maneno na matendo yake, Yesu ‘alitoa ushahidi juu ya ile kweli.’
ile kweli: Yesu hakukuwa anazungumuzia kweli kwa ujumla, lakini kweli kuhusu mipango ya Mungu. Jambo la musingi kuhusu mipango ya Mungu ni kwamba Yesu, “mwana wa Daudi,” ni Kuhani Mukubwa na Mufalme wa Ufalme wa Mungu. (Mt 1:1) Yesu alieleza kama sababu kubwa ya kuja kwake mu dunia, maisha yake mu dunia, na kazi yake ya kuhubiri ilikuwa kutangaza kweli kuhusu ule Ufalme. Malaika walitangaza ujumbe kama huo mbele Yesu azaliwe, na wakati Yesu alizaliwa katika Betlehemu ya Yudea, muji mwenye Daudi alizaliwa.—Lu 1:32, 33; 2:10-14.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 18:38a
Kweli ni nini?: Pengine ulizo la Pilato lilihusu kweli kwa ujumla, halikuhusu “ile kweli” yenye Yesu alitoka tu kuzungumuzia. (Yoh 18:37) Kama Pilato alipenda kabisa kujua kweli ni nini, bila shaka Yesu alipaswa kumujibia. Lakini pengine ulizo la Pilato halikuomba jibu, aliuliza ulizo hilo ili kuzarau kweli, ni kama vile alisema: “Kweli? Njo kusema nini? Hakuna kweli!” Pilato hakungojea hata apate jibu, lakini aliondoka na kuenda inje kwa Wayahudi.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 19:30
akakata roho: Ao “akakata pumuzi; akaacha kupumua.” Pengine hapa neno “roho” (Kigiriki, pneuʹma) linaweza kuwa na maana ya “pumuzi” ao “nguvu ya uzima.” Hilo linapatana na namna tendo la Kigiriki ek·pneʹo (neno kwa neno “kutoa pumuzi”) linatumiwa katika habari yenye kufanana na hii yenye kupatikana mu Mk 15:37 na Lu 23:46 (kwenye linatafsiriwa “akakata pumuzi” ao, “akatoa pumuzi yake ya mwisho” kulingana na kwa ajili ya funzo kuhusu hii maandiko). Watu fulani wanasema kama matumizi ya maneno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “akakata” maana yake Yesu alijiachilia akufe, kwa sababu mambo yote ilikuwa imetimizwa. Alikubali ‘kumwanga uzima wake hata mupaka kifo.’—Isa 53:12; Yoh 10:11.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 19:31
siku hiyo ya Sabato ilikuwa siku kubwa: Sikuzote, Nisani 15, siku yenye ilifuata Pasaka, ilikuwa sabato, hata kama iliangukia siku gani ya juma. (Law 23:5-7) Wakati Sabato hii ya pekee iliangukia siku ya Sabato ya kawaida (ni kusema, siku ya saba ya juma ya Wayahudi, yenye ilianza Siku ya Tano kisha jua kushuka mupaka Siku ya Posho kisha jua kushuka), ilikuwa Sabato “kubwa.” Sabato kama hiyo ilifuata siku Yesu alikufa, ni kusema Siku ya Tano. Kuanzia mwaka wa 31 mupaka 33, ni katika mwaka wa 33 tu ndiyo tarehe 14 Nisani iliangukia Siku ya Tano. Kwa hiyo, ushuhuda huo unahakikisha wazo la kwamba Yesu alikufa tarehe 14 Nisani, mwaka wa 33.