Vichapo Vyenye Kutajwa katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 4-10/03
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAROMA 12-14
“Namna ya Kuonyesha Upendo wa Kikristo”
it-1-F uku. 53 fu. 2-3
Upendo
Upendo wa kindugu (Kigiriki: phi·la·del·phiʹa, neno kwa neno: “upendo kwa ajili ya ndugu”) unapaswa kuwa kati ya washiriki wote wa kutaniko la Kikristo. (Ro 12:10; Ebr 13:1; ona pia 1Pe 3:8.) Kwa hiyo, uhusiano wenye kuwa kati ya washiriki wa kutaniko unapaswa pia kuwa wa karibu sana, wa nguvu sana na wenye uchangamufu sawa vile uhusiano kati ya watu wa familia moja. Hata kama tayari washiriki wa kutaniko wanaonyeshanaka upendo wa kindugu, wanatiwa moyo waendelee kufanya vile kwa ukamili zaidi.—1Te 4:9, 10.
Neno la Kigiriki phi·loʹstor·gos, lenye kumaanisha “mwenye iko na upendo wenye upole,” linatumiwa kuhusu mutu mwenye iko na uhusiano wa karibu sana na mwingine. Muzizi moja wa ile neno yenye kuundwa na maneno mingi, stérgô, unatumiwaka zaidi sana juu ya kumaanisha upendo wa asili, sawa ule wenye uko kati ya watu wa familia moja. Mutume Paulo alitia moyo Wakristo wakomalishe ile sifa. (Ro 12:10) Tena, alionyesha kama mu siku za mwisho, watu watakosa “upendo wa asili” (Kigiriki: aʹstor·goi) na kama watu wa vile wanastahili kifo.—2Ti 3:3; Ro 1:31, 32.
w09 15/10 uku. 8 fu. 3
“Mukuwe Wenye Kufanya Amani na Watu Wote”
3 Soma Waroma 12:17. Paulo alisema kwamba wakati watu wanatutendea mubaya, hatupaswe kulipiza kisasi. Zaidi sana wale wenye wako mu familia zenye hazina dini moja, wanapaswa kutii ile shauri ya Paulo. Bibi ao bwana Mukristo anapaswa kuepuka kurudisha ubaya kwa ubaya mu maneno ao matendo. ‘Kulipa uovu kwa uovu’ hakuletake faida yoyote. Lakini, kunafanyaka mambo ikuwe mubaya zaidi.
w07 1/7 uku. 24-25 fu. 12-13
“Musimulipe Mutu Yeyote Uovu Kwa Uovu”
12 Kisha, Paulo anatoa shauri kuhusu namna tunapaswa kutendea waamini na watu wenye hawako waamini: “Musimulipe mutu yeyote uovu kwa uovu.” Ile maneno inapatana kabisa na ile yenye alitangulia kusema, nikusema, “Muchukie sana mambo maovu.” Kwa kweli, namna gani mutu anaweza kusema kwamba anachukia kabisa mambo maovu ikiwa analipa wengine uovu? Kufanya vile ni kinyume kabisa cha kuwa na upendo wa “bila unafiki.” Kisha Paulo anasema: “Mufanye mambo ya muzuri mbele ya macho ya watu wote.” (Waroma 12:9, 17) Namna gani tunaweza kutumikisha ile shauri?
13 Ku mwanzo, mu barua yenye aliandikia Wakorinto, Paulo alizungumuzia mateso yenye mitume walipata. Alisema hivi: “Tumekuwa tamasha kwa ulimwengu, na kwa malaika, na kwa wanadamu. . . . Wakati tunatukanwa, tunabariki; wakati tunateswa, tunavumilia kwa subira; wakati tunasingiziwa, tunajibu kwa upole.” (1 Wakorinto 4:9-13) Vilevile, leo Wakristo wa kweli wanatazamwa na watu wa ulimwengu huu. Wakati wale wenye kuwa karibu na sisi wanaona mambo ya muzuri yenye tunafanya hata wakati watu wanatuonea, wanaweza penda kusikiliza ujumbe wenye tuko tunahubiri.—1 Petro 2:12.
Musameheane kwa Kupenda
13 Wakati fulani unaweza penda kusaidia mutu mwenye alikukosea afurahie kanuni za Biblia. Mutume Paulo aliandika: “‘Kama adui yako iko na njaa, mupatie chakula; kama iko na kiu, mupatie kitu akunywe; kwa maana kwa kufanya vile utakusanya makaa yenye moto juu ya kichwa chake.’ Usiache ushindwe na uovu, lakini endelea kushinda uovu kwa wema.” (Ro. 12:20, 21) Kama unatenda kwa adabu wakati watu wanakuchokoza, unaweza kusaidia hata watu wakali zaidi wabadilike na kuanza kutenda mambo ya muzuri. Kama unajikaza kuelewa mutu mwenye alikukosea na kujitia pa nafasi yake, unaweza kumusaidia ajifunze Biblia. Mu hali yoyote, ukitenda kwa upole unaweza kufanya ule mwenye alikukosea ajiulize juu ya nini mwenendo yako iko muzuri.—1 Pe. 2:12; 3:16.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
Namna ya Kuchagua Mambo ya Kujifurahisha
5 Kila kitu chenye tunafanya mu maisha kiko na uhusiano na ibada yetu kwa Yehova. Paulo alieleza jambo hilo wakati alisema hivi: “Mutoe miili yenu ikuwe zabihu yenye uzima, takatifu, na yenye kukubalika kwa Mungu.” (Waroma 12:1) Yesu alisema hivi: “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Marko 12:30) Sikuzote tunapenda kumutolea Yehova kitu cha muzuri zaidi. Katika Israeli ya zamani, wakati watu walitoa zabihu ya munyama kwa Yehova, walipaswa kutoa munyama mwenye kuwa na afya ya muzuri. Ikiwa zabihu ilikuwa na kasoro ao ulemavu fulani, Mungu aliikataa. (Mambo ya Walawi 22:18-20) Vilevile, Yehova anaweza kukataa ibada yetu. Juu ya nini?
6 Yehova anatuambia hivi: “Munapaswa kuwa watakatifu, kwa sababu mimi ni mutakatifu.” (1 Petro 1:14-16; 2 Petro 3:11) Yehova atakubali ibada yetu ikiwa tu iko takatifu, ao safi. (Kumbukumbu la Torati 15:21) Ibada yetu haiwezi kuwa safi kama tunafanya mambo yenye Yehova anachukia, kama vile mambo machafu, yenye jeuri, ao yenye kuwa na uhusiano na pepo wachafu. (Waroma 6:12-14; 8:13) Lakini Yehova anaweza kuchukizwa pia kama tunatumia mambo ya vile ili kujifurahisha. Ile inaweza kufanya ibada yetu isikuwe safi na Yehova hawezi kuikubali. Tena, ile mambo inaweza kuharibu kabisa uhusiano wetu pamoja naye.
w08 15/6 uku. 31 fu. 4
Mambo Makubwa Katika Barua kwa Waroma
13:1—Ni mu maana gani mamlaka zenye kuwa kubwa “zimesimamishwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri”? Mamlaka za serikali “zimesimamishwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri” mu maana ya kwamba Mungu anaziruhusu zitawale, na pia Mungu alionaka mbele ya wakati kama serikali fulani zitatawalaka. Ile inaonekana waziwazi mu mambo yenye Biblia ilitabiri kuhusu zile serikali.
TAREHE 11-17/03
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAROMA 15-16
“Umutegemee Yehova Juu Akupatie Uvumilivu na Faraja”
“Mulie Pamoja na Wale Wenye Kulia”
11 Habari yenye kuzungumuzia huzuni yenye Yesu alikuwa nayo wakati wa kifo cha Lazaro, ni moja tu kati ya maandiko mengi sana yenye kuleta kitulizo yenye kupatikana katika Neno la Mungu lenye kufariji. Ndiyo sababu “mambo yote yenye yaliandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutoka katika Maandiko tukuwe na tumaini.” (Ro. 15:4) Ikiwa umefiwa, wewe pia unaweza kupata maneno yenye kutuliza katika maandiko kama haya:
▪ “Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo; anaokoa wale wenye kupondwa roho.”—Zb. 34:18, 19.
▪ “Wakati mahangaiko yalinilemea, [Yehova] ulinifariji na kunituliza.”—Zb. 94:19.
▪ “Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu mwenye alitupenda na kutupatia faraja ya milele na tumaini la muzuri kupitia fazili zenye hazistahiliwe, wafariji mioyo yenu na kuwafanya ninyi kuwa imara.”—2 Te. 2:16, 17.
“Muache Uvumilivu Ukamilishe Kazi Yake”
5 Umuombe Yehova akupatie nguvu. Yehova ni “Mungu mwenye anatoa uvumilivu na faraja.” (Ro. 15:5) Ni yeye tu ndiye anaelewa muzuri sana hali yetu, namna tunajisikia na namna tulikomaa. Kwa hiyo, anajua muzuri sana mambo yenye tuko nayo lazima ili kuvumilia. Biblia inasema hivi: “Anatimiza tamaa ya wale wenye kumuogopa; anasikia kilio chao cha kuomba musaada, na anawaokoa.” (Zb. 145:19) Lakini, namna gani Mungu atajibia sala zetu za kumuomba nguvu ya kuvumilia?
“Unapaswa Kumupenda Yehova Mungu Wako”
11 Yehova ametutolea tumaini lenye linajaza mioyo yetu shangwe na Amani. (Ro. 15:13) Tumaini lenye Mungu ametutolea linatusaidia tuvumilie majaribu. Wakristo watiwa-mafuta wenye watakuwa ‘waaminifu hata kufikia kifo watapewa taji la uzima’ kule mbinguni. (Ufu. 2:10) Wakristo waaminifu wenye kuwa na tumaini la kuishi ku dunia watapokea baraka za milele mu Paradiso. (Lu. 23:43) Ile matumaini inatufanya tujisikie namna gani? Mioyo yetu inajaa furaha, amani na upendo kwa Mutoaji wa “kila zawadi ya muzuri na kila zawadi kamilifu,” haiko vile?—Yak. 1:17.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w89-F 1/12 uku. 24 fu. 3
“Ili Kuonyesha Kama Upendo Wao Ni wa Kweli Kabisa”
Bila shaka, ndugu zao wenye walikuwa Watu wa Mataifa walipaswa kufikiria namna gani watasaidia ndugu wa Yerusalemu wenye walikuwa mu majaribu. Kusema kweli, walikuwa na “deni” fulani ya Wakristo wa Yerusalemu. Je, haiko Yerusalemu njo kwenye habari njema ilianzia mbele ifike kwenye Watu wa Mataifa walikuwa wanaishi? Paulo anatoa wazo hii: “Kwa maana kama mataifa wameshiriki mambo yao ya kiroho, wao pia wako na deni la kuwatumikia kwa vitu vyao vya kimwili.”—Waroma 15:27.
it-2-F uku. 647 fu. 2
Uwezo wa Kujua Mambo Mbele ya Wakati, Uwezo wa Kupanga Mambo Mbele ya Wakati
Masiya ao Kristo, njo mwenye alipaswa kuwa Uzao wenye uliahidiwa wenye Mungu angetumia ili kubariki watu wote wenye haki wa mu familia zote za dunia. (Gal 3:8, 14) Ule “uzao” ulizungumuziwa mara ya kwanza kisha uasi kutokea mu Edeni, lakini mbele Abeli azaliwe. (Mwa 3:15) Kulipita miaka 4000 hivi mbele ile “siri takatifu” ifunuliwe. Ilifunuliwa wakati ilionekana waziwazi kama ule “uzao” wa Kimasiya ni nani. Kwa kweli, ile siri takatifu “ilikuwa imefichwa tangu nyakati za zamani.”—Ro 16:25-27; Efe 1:8-10; 3:4-11.
TAREHE 18-24/03
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | 1 WAKORINTO 1-3
“Uko Mutu wa Kimwili ao Mutu wa Kiroho?”
Kuwa Mutu wa Kiroho, Maana Yake Nini?
4 Fikiria kwanza mawazo ya mutu wa kimwili. Watu wa ulimwengu huu wanakaza akili zao juu ya tamaa za mwili. Paulo anaeleza jambo hilo kuwa ‘roho ambayo sasa inatenda katika wana wa kutotii.’ (Efe. 2:2) Roho hiyo inachochea watu wengi waige mambo yenye watu wengi zaidi wanafanya. Wanakaza akili zao juu ya mwili. Kwa hiyo, wengi kati yao wanafanya mambo yenye wao wenyewe wanaona kuwa sawa na hawajikaze hata kidogo kuishi kulingana na kanuni za Mungu. Mutu wa kimwili, ao mwenye kukaza akili yake juu ya mwili, mara nyingi anahangaikia sana kusifiwa na kufuatia vitu vya kimwili ao kutetea mambo yenye anaona kuwa ni haki yake.
5 Ni mambo gani mengine yenye yanaweza kutambulisha mutu wa kimwili? Watu wenye kufanya “matendo ya mwili” ya aina yoyote, wao pia ni watu wa kimwili. (Gal. 5:19-21) Barua ya kwanza yenye Paulo aliandikia kutaniko la Korinto inataja tabia zingine zenye kutambulisha watu wa kimwili. Tabia kama vile: kuwa watu wenye kuleta migawanyiko, wenye ubaguzi, wenye hawapendi makubaliano, wenye kupelekana kwenye tribinali, wenye hawaheshimu wale wenye kuongoza, wenye wanapenda sana kula na kunywa. Wakati mutu wa kimwili anapatwa na jaribu, anakuwa zaifu na anaangukia katika jaribu hilo. (Mez. 7:21, 22) Mwanafunzi Yuda alizungumuzia juu ya wale wenye wangekuwa zaifu sana mupaka wangefikia kukosa “hali ya kiroho.”—Yuda 18, 19.
Kuwa Mutu wa Kiroho, Maana Yake Nini?
6 Sasa, kuwa ‘mutu wa kiroho,’ maana yake nini? Tofauti na mutu wa kimwili, mutu wa kiroho anahangaikia sana urafiki wake pamoja na Yehova. Watu wa kiroho wanajikaza kuwa “waigaji wa Mungu.” (Efe. 5:1) Hilo linamaanisha kama wanajikaza kuwa na mawazo ya Yehova juu ya mambo mbalimbali na kuona mambo namna anayaona. Wanaona kuwa Mungu ni mutu wa kweli kabisa. Tofauti na watu wa kimwili, watu wa kiroho wanajikaza kupatanisha njia zao zote na kanuni za Yehova. (Zb. 119:33; 143:10) Kuliko kukaza akili yake juu ya matendo ya mwili, mutu wa kiroho anajikaza kuonyesha sifa za ‘tunda la roho.’ (Gal. 5:22, 23) Ili kueleza zaidi maana ya ‘mutu wa kiroho,’ fikiria ulinganifu huu: Mutu mwenye kujua muzuri kufanya biashara anaweza kuitwa mufanyabiashara, vilevile mutu mwenye kukaza akili yake juu ya mambo ya kiroho anaweza kuitwa mutu wa kiroho.
Kuwa Mutu wa Kiroho, Maana Yake Nini?
15 Namna gani unaweza kuiga Kristo? Andiko la 1 Wakorinto 2:16 linasema kama tunapaswa kuwa na “akili ya Kristo.” Na Waroma 15:5 inasema kama tunapaswa kuwa na ‘mutazamo uleule wa akili ambao Kristo Yesu alikuwa nao.’ Kwa hiyo, ili tukuwe kama Kristo tunapaswa kujua namna anafikiri na sifa zake zote. Kisha tunapaswa kufuata mufano wake. Yesu alikaza akili yake juu ya urafiki wake pamoja na Mungu. Kwa hiyo, kuwa kama Yesu kunafanya tukuwe zaidi kama Yehova. Kwa hiyo, tunaona kuwa ni jambo la maana sana tujifunze kufikiri kama Yesu.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 854 fu. 5
Hekima
Mu hekima yao, watu wa ulimwengu wamekataa zawadi yenye Mungu ametoa kupitia Kristo na wanaiona kuwa upumbavu; hata kama inaonekana wakubwa wa ulimwengu walikuwa na uwezo na hekima fulani ya kuongoza mambo, walifikia ‘kuua Bwana mwenye utukufu ku muti wa mateso.’ (1Ko 1:18; 2:7, 8) Lakini, Mungu alionyesha namna hekima ya watu wenye hekima wa ulimwengu ilikuwa upumbavu, na aliwapatisha haya kwa kutumia kile chenye waliona kuwa “kitu kipumbavu cha Mungu,” na pia watu wenye waliona kuwa ‘wapumbavu, wazaifu, na wenye hawana maana’ ili kutimiza kusudi Lake lenye haliwezi kushindikana. (1Ko 1:19-28) Paulo alikumbusha Wakristo wa Korinto kwamba “hekima ya mupangilio huu wa mambo” na “ile ya watawala wa mupangilio huu wa mambo” itafikia kuwa kitu bure; kwa hiyo, Paulo hakutia ile hekima mu ujumbe wa kiroho wenye alikuwa anatangaza. (1Ko 2:6, 13) Aliambia Wakristo wa Kolosai wafanye angalisho juu wasinaswe mu mutego wa “filozofia [phi·lo·so·phiʹas, neno kwa neno: “upendo wa hekima”] na udanganyifu wa bure kulingana na desturi ya wanadamu.”—Kol 2:8; ona pia mistari ya 20-23.
w08 15/7 uku. 27 fu. 6
Mambo Makubwa Katika Barua kwa Wakorinto
2:3-5. Wakati alikuwa anahubiri kule Korinto, fasi ya maana sana ya elimu na filozofia ya Kigiriki, inawezekana Paulo alijiuliza kama ataweza kushawishi wasikilizaji wake. Lakini, hakuruhusu uzaifu wowote ao woga wenye pengine alikuwa nao umuzuie asitimize kazi yenye Mungu alimupatia. Na siye, hatupaswe kuruhusu hali za mupya zituzuie kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu. Kama Paulo, tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atatusaidia.
TAREHE 25-31/03
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | 1 WAKORINTO 4-6
“Chachu Kidogo Inachachisha Donge Lote”
it-2-F uku. 130 fu. 5
Chachu
Mutume Paulo alitumia ulinganisho wa vile wakati aliambia kutaniko la Kikristo la Korinto litoshe muasherati katikati yao. Alisema: “Je, hamujue kama chachu kidogo inachachisha donge lote? Mutoshe chachu ya zamani ili mukuwe donge mupya, kwa kuwa ninyi hamuna chachu. Kwa maana, kwa kweli, Kristo kondoo wetu wa Pasaka ametolewa kuwa zabihu. ” Kisha alionyesha waziwazi maana ya “chachu” yenye alikuwa anazungumuzia, kwa kusema: “Kwa hiyo, tufanye basi sikukuu, hapana na chachu ya zamani, ao na chachu ya ubaya na uovu, lakini na mikate yenye haina chachu, ya unyoofu na kweli.” (1Ko 5:6-8) Hapa, Paulo alitumia maana ya mufano ya sikukuu ya Wayahudi ya Keki Zenye Hazina Chachu, yenye ilikuwa inafanywa kisha sikukuu ya Pasaka. Kama vile kipande kidogo tu cha donge la unga chenye chachu kinafanyaka donge lote livimbe, vilevile kutaniko lote kwa ujumla lingekuwa muchafu mu macho ya Yehova kama halingetosha katikati yake uvutano wa ule muasherati. Iliomba basi kutosha “chachu” katikati yake, sawa vile Waisraeli hawakupaswa kuwa na chachu yoyote kwao wakati wa ile sikukuu.
it-2-F uku. 903 fu. 6
Shetani
“Kumutoa mutu kwa Shetani kwa ajili ya kuharibiwa kwa mwili” maana yake nini?
Wakati mutume Paulo alikuwa anapatia kutaniko la Korinto maagizo kuhusu hatua za kukamatia mushiriki wa kutaniko mwenye alifanya uasherati na bibi ya baba yake, aliandika: “Munapaswa kumutoa mutu wa namna hiyo kwa Shetani kwa ajili ya kuharibiwa kwa mwili.” (1Ko 5:5) Kwa kusema vile, Paulo aliomba wafukuze ule mutu mu kutaniko, wakate uhusiano wowote wa kindugu naye. (1Ko 5:13) Kumutoa kwa Shetani kulimaanisha kumutosha mu kutaniko na kumutupa mu ulimwengu wenye unatawaliwa na Shetani. Sawa vile “chachu kidogo” mu “donge lote” la unga, ule mutu alikuwa “mwili,” ni kusema mutu wa kimwili mu kutaniko; kwa kutosha ule mutu mwenye alifanya uasherati na bibi ya baba yake, kutaniko lenye kukaza akili juu ya mambo ya kiroho lingekuwa limeharibu “mwili” wenye ulikuwa katikati yake. (1Ko 5:6, 7) Vilevile, Paulo alitoa Himenayo na Aleksanda kwa Shetani juu walikuwa wametupilia mbali imani na zamiri ya muzuri na imani yao ilikuwa imevunjika.—1Ti 1:20.
lvs 241, maelezo ingine
Kutengwa na Kutaniko
Wakati mutu fulani mwenye alifanya zambi nzito hatubu na anakataa kufuata kanuni za Yehova, hawezi tena kuwa mushiriki wa kutaniko. Anapaswa kutengwa na kutaniko. Wakati mutu fulani anatengwa na kutaniko, tunaacha kupitisha wakati pamoja naye na tunaacha kuongea naye. (1 Wakorinto 5:11; 2 Yohana 9-11) Mupango wa kutengwa na kutaniko unafanya jina la Yehova na kutaniko visichafuliwe. (1 Wakorinto 5:6) Pia, kutengwa na kutaniko ni nizamu yenye inaweza kusaidia mutu atubu ili amurudilie Yehova.—Luka 15:17.
▸ Sura ya 3, fungu la 19
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w09 15/5 uku. 24 fu. 16
Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
16 Wakristo wenye wanajaribiwa ni “tamasha kwa malaika.” (1 Ko. 4:9) Malaika wanafurahi wakati wanaona matendo yetu ya uaminifu na hata wanashangilia wakati mutenda-zambi anatubu. (Luka 15:10) Malaika wanaona mwenendo wa wanamuke Wakristo wenye unapendeza Mungu. Biblia inasema kama “mwanamuke anapaswa kuwa na alama ya mamlaka juu ya kichwa chake kwa sababu ya malaika.” (1 Ko. 11:3, 10) Ndiyo, malaika wanafurahi wakati wanaona namna wanamuke Wakristo na watumishi wengine wote wa Mungu ku dunia wanatii ukichwa na kufuata utaratibu wa kiteokrasi. Utii wa watumishi wa Mungu unakumbusha wale wana wa mbinguni wa Mungu kama ni jambo ya lazima kutii utaratibu wa kiteokrasi.
it-2-F uku. 151 fu. 2
Sheria
Sheria kwa ajili ya malaika. Hata kama malaika ni viumbe wa hali ya juu kupita mwanadamu, wanatii sheria na amri za Mungu. (Ebr 1:7, 14; Zb 104:4) Hata Yehova aliwekea Shetani vizuizi. (Yob 1:12; 2:6) Wakati alikuwa anabishana na Shetani, Mikaeli, malaika mukubwa, alionyesha kwamba alitambua na kuheshimia cheo cha Muamuzi Mukubwa Zaidi kwa kusema: “Yehova akukemee.” (Yuda 9; ona pia Zek 3:2.) Yehova ameweka malaika wote chini ya mamlala ya Yesu Kristo mwenye ametukuzwa. (Ebr 1:6; 1Pe 3:22; Mt 13:41; 25:31; Flp 2:9-11) Kwa hiyo, Yesu njo alituma mujumbe, malaika, kwa Yohana. (Ufu 1:1) Mu 1 Wakorinto 6:3, mutume Paulo anaonyesha kama ndugu za kiroho wa Kristo watahukumu malaika, inaonekana anasema vile sababu watasaidia kwa njia fulani kuleta hukumu juu ya roho waovu.