UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 6-8
“Ni Vile Alifanya Kabisa”
Wazia kazi yote yenye Noa na familia yake walipaswa kufanya ili kujenga safina bila kuwa na vyombo mbalimbali vyenye kutumiwa leo na bila kujua njia mbalimbali za kujenga zenye kutumiwa leo.
Jengo hilo lilikuwa kubwa sana—lilikuwa na urefu wa metre 133 hivi, upana wa metre 22 hivi, na urefu kuenda juu wa metre 13 hivi
Noa alipaswa kuangusha miti, kuikata-kata kulingana na vipimo vyenye kufaa, na kuipeleka nafasi ya kazi
Alipaswa kutumia lami ili kufunika ndani na inje ya jengo hilo kubwa
Alipaswa kuweka chakula chenye yeye na familia yake na wanyama wangekula kwa mwaka mumoja
Ile kazi ilikamata miaka 40 ao 50 hivi
Namna gani hii habari inaweza kututia moyo wakati tunaona kama ni nguvu kufanya mamboyenye Yehova anatuomba?