Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Mwezi wa 4 uku. 7
  • “Muondoe Miungu ya Kigeni”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Muondoe Miungu ya Kigeni”
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ukubali Musaada wa Yehova ili Kupinga Pepo Wachafu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kuzungumuza na Mashetani?
    Amuka!—2017
  • Ushikamane na Yehova Tu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Yakobo na Esau Wanasikilizana
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
mwb20 Mwezi wa 4 uku. 7
Mwanaume mumoja anatupa kitu cha kuvaa mu shingo chenye kuwa na upatano na tabia ya kupashana habari na pepo wachafu.

MAISHA YA MUKRISTO

“Muondoe Miungu ya Kigeni”

Yakobo alijua kama Yehova tu njo anapaswa kuabudiwa, hata kama Yehova alikuwa hajatoa sheria yenye kukataza kuabudu sanamu. (Ku 20:3-5) Kwa hiyo, kisha Yehova kumuambia Yakobo arudie Beteli, Yakobo aliambia watu wote wenye walikuwa pamoja naye waondoe sanamu zao. Kisha Yakobo akaharibu zile sanamu, kutia ndani, vitu vya kuvaa kwenye masikio, vyenye pengine watu walivaa ili kujilinda. (Mwa 35:1-4) Kwa kweli Yehova alifurahia mambo yenye Yakobo alifanya.

Leo, namna gani tunaweza kumuabudu Yehova tu? Kwanza, tunapaswa kuepuka jambo lolote lenye kuwa na upatano na ibada ya sanamu na kuepuka kupashana habari na pepo wachafu. Ile inatia ndani kuachana kabisa na vitu vyote vyenye kuwa na uhusiano na pepo wachafu na tunapaswa pia kuchunguza muzuri mambo yenye tunajifurahisha nayo. Kwa mufano, ujiulize hivi: ‘Ninafurahia vitabu ao filme zenye kuonyesha wanyonya-damu, maiti zenye kutembea, na mambo yenye haiko ya kawaida? Mambo yenye ninajifurahisha nayo inafanya uchawi, ulozi, ao laana vionekane kuwa ni mambo ya kujifurahisha yenye haina hatari?’ Tunapaswa kukataa kabisa jambo lolote lenye Yehova anachukia.​—Zb 97:10.

MUANGALIE VIDEO “UMUPINGE IBILISI,” NA KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:

  • Mutoto analala ku kitanda na anavaa kwenye mukono kitu cha kumulinda. Nyuma ya ule mutoto, mama yake iko anazungumuza na bibi na bwana wenye wanajifunzaka naye Biblia.

    Ni tatizo gani lilitokea katika maisha ya mwanafunzi wa Biblia mwenye kuitwa Palesa?

  • Wale bibi na bwana na mwanafunzi wao wa Biblia wanakutana na wazee wawili ili kupata musaada.

    Juu ya nini ni muzuri kutafuta musaada wa wazee katika hali yoyote yenye kuhusisha kupashana habari na pepo wachafu?

  • Ule mwanafunzi wa Biblia anaunguza kitu cha kujilinda chenye mutoto wake alikuwa anavaa.

    Umupinge Ibilisi, na umukaribie Mungu.​—Yak 4:7, 8

    Watu wenye wanapenda Yehova awalinde, wanapaswa kuachana kabisa na mambo gani?

  • Palesa aliamua kufanya nini?

  • Katika eneo lenu, unaweza kufanya mambo gani fulani, ili uepuke uvutano wa pepo wachafu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine