Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g17 na. 2 uku. 4-6
  • Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kuzungumuza na Mashetani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kuzungumuza na Mashetani?
  • Amuka!—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • CHANZO KIBAYA
  • Ukubali Musaada wa Yehova ili Kupinga Pepo Wachafu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Kwa Nini Ni Vibaya Kuwasiliana na Pepo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Viumbe vya Kiroho—Ni Marafiki ao Maadui Wetu?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Pinga Ibilisi na Njia Zake za Kudanganya
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2017
g17 na. 2 uku. 4-6
Bibi na bwana wenye kuangalia matangazo ya biashara kuhusu filme za mambo ya mashetani kwenye televizyo

Hata kama mambo ya kujifurahisha yanaonyesha habari za mashetani kwa njia yenye kuvutia, tunapaswa kujua hatari yenye kutokana na mambo hayo

HABARI KUBWA | HATARI YA KUJIFURAHISHA NA MAMBO YA MASHETANI

Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kuzungumuza na Mashetani?

HATA kama watu wengi wako na mashaka kuhusu mambo yenye kuwa na uhusiano na mashetani, kwa sababu wanayaona kuwa habari za uongo ao mawazo yenye yalitungwa na watu wenye kutayarisha filme, Biblia inaonyesha mawazo yenye kuwa tofauti. Inatuonya waziwazi kuhusu mazoea ya kuzungumuza na mashetani. Kwa mufano, andiko la Kumbukumbu la Torati 18:10-13 linasema hivi: ‘Asipatikane ndani yako . . . yeyote anayefanya uaguzi, mwenye kufanya uchawi ao yeyote anayetafuta ishara za bahati ao mulozi, ao anayefunga wengine kwa kuwatakia maovu ao yeyote anayetafuta shauri kwa mwenye kuwasiliana na pepo ao mujuzi wa kubashiri matukio ao yeyote anayeuliza habari kutoka kwa wafu.’ Sababu gani? Andiko hilo linaongeza hivi: ‘Kila mutu anayefanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova . . . Utajionyesha kuwa hauna kosa kwa Yehova Mungu wako.’

Sababu gani Biblia inakataza kabisa mazoea yote ya kuzungumuza na mashetani?

CHANZO KIBAYA

Biblia inatufundisha kwamba miaka mingi mbele Mungu aumbe dunia, aliumba mamilioni ya viumbe wa roho, ni kusema, malaika. (Ayubu 38:4, 7; Ufunuo 5:11) Kila mumoja wa malaika hao aliumbwa na uhuru wa kuchagua, ni kusema, uwezo wa kuchagua kati ya mema na mabaya. Wamoja kati yao walichagua kumuasi Mungu, na wakaacha makao yao ya mbinguni ili kutesa watu duniani. Matokeo? Dunia “ikajaa jeuri.”—Mwanzo 6:2-5, 11; Yuda 6.

Biblia inasema kwamba malaika hao waovu wako na uvutano mukubwa juu ya wanadamu, wanadanganya mamilioni ya watu. (Ufunuo 12:9) Wanatumia hata tamaa ya wanadamu ya kupenda kujua mambo ya wakati wenye kuja ili kuwadanganya.—1 Samweli 28:5, 7; 1 Timotheo 4:1.

Ni kweli kwamba uwezo fulani wenye hauko wa kawaida unaonekana kuwa unasaidia watu. (2 Wakorintho 11:14) Lakini, kwa kweli, malaika waovu ndio wanajaribu kufunga macho ya watu ili wasijue kweli kuhusu Mungu.—2 Wakorintho 4:4.

Kwa hiyo, kulingana na Biblia, kuna hatari kama mutu anajifurahisha kwa kuzungumuza na roho waovu. Watu wenye walipenda kuwa wanafunzi wa Yesu walifundishwa kweli kuhusu matendo kama hayo. Ndiyo sababu “wale waliozoea kufanya ufundi wa uchawi wakaleta pamoja vitabu vyao wakaviteketeza [ao, wakavichoma],” hata kama kufanya hivyo ilikuwa kupoteza feza nyingi.—Matendo 19:19.

Mwanamuke mumoja anasoma kitabu chenye kuzungumuzia mambo ya mashetani

“Vitabu, filme, na televizyo vinaonyesha wachawi kwa njia yenye kuvutia katika miaka ya hivi karibuni; pengine hilo ndilo linafanya vijana wengi wanawake waendelee kuamini uchawi.” —Gallup Youth Survey, 2014

Leo pia, wengi wameamua kuacha kujifurahisha na mambo yenye kuwa na uhusiano na mashetani. Kwa mufano, wakati Mariaa alikuwa na miaka 12, alionekana kuwa na uwezo wa kutabiri mambo ao hatari fulani yenye kuwa mbele. Alitumia karte ili kutabiri mambo yenye yangepata wanafunzi wenzake, na kwa sababu mambo yenye alikuwa anatabiri yalitokea kabisa, akaanza kupendezwa na uaguzi.

Maria aliwaza kwamba alikuwa na zawadi ya Mungu yenye ilimuwezesha kusaidia watu. Anasema hivi: “Lakini jambo fulani lilinisumbua. Wakati nilitabiri mambo kupitia karte, nilifanya hivyo kwa ajili ya wengine. Sikuwa na uwezo wa kutabiri mambo kupitia karte hizo kwa ajili yangu, hata kama nilipenda kujua mambo yenye yangenifikia.”

Kwa sababu alihangaishwa na maulizo mengi yenye hayakupata majibu, Maria alisali kwa Mungu na kisha alitembelewa na Mashahidi wa Yehova, na akaanza kujifunza Biblia pamoja nao. Maria alijifunza katika Biblia kwamba uwezo wake wa kutabiri mambo yenye kuja haukutoka kwa Mungu. Alijifunza pia kwamba wale wenye wanataka kuwa marafiki wa Mungu wanapaswa kuachana na vitu vyote vyenye kuwa na uhusiano na mashetani. (1 Wakorintho 10:21) Mambo yalifikia kuwa je? Maria alitupa vitabu na vitu vyote vyenye kuhusiana na mashetani. Sasa, anatangazia wengine kweli yenye amejifunza katika Biblia.

Wakati alikuwa kijana, Michael alipenda sana kusoma vitabu vyenye kuzungumuzia hadisi za mambo ya mashetani. Anasema hivi: “Nilipenda kujifananisha na watu wenye kujulikana sana wa miaka yangu ambao walizunguka katika ulimwengu wenye hauko wa kawaida.” Pole kwa pole, Michael alifikia kuzoea kusoma vitabu vyenye kuzungumuzia mambo ya mashetani. Anasema tena hivi: “Tamaa ya kupenda kujua mambo mengi zaidi ilinifanya nifurahie kusoma vitabu na kuangalia filme zenye kuzungumuzia mambo hayo.”

Lakini, kujifunza Biblia kulimusukuma Michael achunguze muzuri mambo yenye alikuwa anasoma. Anamalizia kwa kusema hivi: “Nilifanya liste ya mambo yote yenye kuwa na uhusiano na mashetani na kuachana nayo. Nilijifunza jambo la maana. Katika andiko la 1 Wakorintho 10:31, Biblia inasema hivi: ‘Mufanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu.’ Sasa, ninajiuliza hivi: ‘Mambo yenye ninasoma yanamuletea Mungu utukufu ao hapana?’ Kama hayamuletee utukufu, ninayaepuka.”

Mwanamuke mumoja anaangalia site ya jw.org

Kwa hiyo, ni jambo lenye kufaa wakati Biblia inalinganishwa na taa. Ni Biblia tu ndiyo inatoa mafasirio ya kweli kuhusu kuzungumuza na mashetani. (Zaburi 119:105) Lakini, Biblia inafasiria zaidi ya hayo. Inazungumuzia ahadi nzuri ya ulimwengu ambamo hamutakuwa roho waovu. Hilo litakuwa na matokeo makubwa juu ya wanadamu. Kwa mufano, andiko la Zaburi 37:10, 11 linasema hivi: ‘Na bado muda kidogo tu, na mutu muovu hatakuwako tena; nawe hakika utapaangalia mahali pake, naye hatakuwapo. Bali wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.’

a Majina yamebadilishwa katika habari hii.

Kuzungumuza na Mashetani Ni Nini?

Watu wanapendezwa na mambo ya mashetani kwa kufanya uchawi, uaguzi, na kwa kutafuta kuelewa mambo kupitia nyota. Katika sehemu nyingi za dunia, watu wanajaribu kuzungumuza na roho waovu kupitia muchawi ao mufumu. Watu wengi wanatumia uaguzi ili kujaribu kujua mambo yenye kuja. Wanaangalia nyota, wanatafuta ishara za bahati, wanatazama katika kitu fulani chenye kuwa kama kioo, wanafasiria alama za mikono ya wengine, ao alama za mikono yao.

Vitabu, magazeti, na filme vinaonyesha mambo ya mashetani kwa njia yenye kupendeza na kwamba hayana hatari yoyote. Watu fulani wenye elimu ya mawasiliano (communication) wanasema kwamba namna programu za televizyo na filme zinaonyesha mambo ya mashetani imechochea sana mambo yenye watu wanaamini.

Biblia Inafundisha Kabisa Nini?

Tunakualika ujifunze mengi zaidi kwa kusoma sura ya 10 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Kimechapishwa na Mashahidi wa Yehova na unaweza kukichukua bila kulipa kwenye jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine