UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 42-43
Yosefu Anaonyesha Kabisa Sifa ya Kujizuia
Wazia namna Yosefu alijisikia wakati bila kutazamia alikutana na ndugu zake uso kwa uso? Angependa angejitambulisha mara moja na kuwakumbatia ao kujilipizia kisasi. Lakini hakutenda palepale bila kufikiri. Kama watu wa familia yako ao watu wengine wanakutendea bila haki, utafanya nini? Mufano wa Yosefu unatufundisha kama ni jambo la maana kujizuia na kubakia mwenye kutulia, kuliko kufuata moyo wetu wenye kuwa mudanganyifu wenye unatuchochea kutenda kulingana na hali yetu ya kukosa kukamilika na bila kufikiri.
Namna gani unaweza kumuiga Yosefu katika hali zenye unakutana nazo?