Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb21 Mwezi wa 9 uku. 3-16
  • Tumia mu Mahubiri Broshua na Kitabu Furahia Maisha Milele!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tumia mu Mahubiri Broshua na Kitabu Furahia Maisha Milele!
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kuongoza Funzo ya Biblia kwa Kutumia “Furahia Maisha Milele!”
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Saidia Mwanafunzi Wako wa Biblia Afikie Kubatizwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Namna ya Kutumia Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
mwb21 Mwezi wa 9 uku. 3-16
Bibi na bwana wanatumia broshua “Furahia Maisha Milele!” juu ya kuzungumuza na mwanaume mumoja fasi kwenye bisi inazoea kusimama.

MAISHA YA MUKRISTO

Tumia mu Mahubiri Broshua na Kitabu Furahia Maisha Milele!

Tuko na furaha sana ya kupata broshua na kitabu ya mupya kwa ajili ya kuongoza mafunzo ya Biblia! Tunasali Yehova atubariki juu tuweze kufanya wanafunzi wengi sana. (Mt 28:18-20; 1Ko 3:6-9) Tunaweza kufanya nini ili kutumia muzuri hivi vyombo?

Kulingana na vile Furahia Maisha Milele! inapangwa, ni lazima mwanafunzi na mwalimu wakuwe nachangia mazungumuzo wakati ya funzo. Kwa hiyo, juu muko njia ya mupya ya kufundisha, inaomba kufuata hii maagizo wakati uko najitayarisha na wakati uko naongoza mafunzo ya Biblia.a

  • Kusoma habari na kuzungumuzia maulizo

  • Kusoma maandiko yenye iko na neno “soma” na kusaidia mwanafunzi aelewe namna ya kuitumikisha

  • Kuangalia mavideo na kuizungumuzia kwa kutumia maulizo yenye ilitayarishwa

  • Kujikaza kumaliza somo yote kila mara yenye munajifunza

Wakati uko mu mahubiri, upatie kwanza musikilizaji broshua juu ya kuona kama anapendezwa. (Ona kisanduku, “Namna ya Kutolea Mutu Broshua Furahia Maisha Milele! Wakati Unamutembelea Mara ya Kwanza.”) Kama unamaliza kujifunza broshua pamoja na mwanafunzi na unaona kama anapenda kuendelea, umutolee sasa kitabu na muendeleshe funzo mu somo ya 04. Kama ungali najifunza na mutu mu kitabu Biblia Inatufundisha, ao kitabu Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu, ao kichapo ingine ya kuongozea amo funzo, uache na uanze kujifunza naye kitabu Furahia Maisha Milele! na uamue ni wapi kwenye mutaanzia.

Walewale bibi na bwana wanatumia kitabu “Furahia Maisha Milele!” ili kuongoza funzo ya Biblia ya mwanaume na wako kwake.

MUANGALIE VIDEO TUNAKUKARIBISHA KU MAZUNGUMUZO YETU YA BIBLIA, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Wanafunzi watajifunza mambo gani mu hii kitabu ya mupya?

  • Juu ya nini unapaswa kuonyesha wanafunzi wapya hii video?

  • Ni mambo gani yenye unaweza kuambia mwanafunzi hatua kwa hatua akuwe nafanya? (Ona kisanduku “Wazo Kubwa na Mambo ya Kufanya mu Kila Sehemu.”)

a JAMBO YA KUKUMBUKA: Hata kama wakati ya funzo ni weye kuamua kama mutazungumuzia ao hapana sehemu “Habari Zingine”, wakati ya kujitayarisha inaomba kusoma na kuchunguza kila jambo yenye kuwa ndani. Kufanya vile, itakusaidia ujue ni nini yenye inaweza kufurahisha sana mwanafunzi wako na kumusaidia. Mu kitabu ya kielektroniki muko viunganishi (lien) vyenye vinapeleka ku video na ku habari zingne.

WAZO KUBWA NA MAMBO YA KUFANYA MU KILA SEHEMU

 

MASOMO

WAZO KUBWA

KILE MWANAFUNZI ATAFANYA

1

01-12

Namna Biblia inaweza kukusaidia na namna unaweza kufikia kujua mwenye aliiandikishaka

Utie mwanafunzi moyo akuwe nasoma Biblia, akuwe najitayarisha kwa ajli ya funzo, na aanze kukusanyika

2

13-33

Mambo yenye Mungu alishatufanyia na ibada yenye inamufurahisha

Utie mwanafunzi moyo akuwe naambia wengine mambo yenye iko najifunza na umutie moyo akuwe muhubiri

3

34-47

Mambo yenye Mungu anapenda watumishi wake wafanye

Utie mwanafunzi moyo ajitoe kwa Yehova na abatizwe

4

48-60

Mambo yenye unaweza kufanya juu uendelee kuwa rafiki ya Yehova

Usaidie mwananafunzi ajue kutofautisha mambo ya muzuri na ya mubaya, na umusaidie afanye maendeleo

NAMNA YA KUTOLEA MUTU BROSHUA FURAHIA MAISHA MILELE! WAKATI UNAMUTEMBELEA MARA YA KWANZA

Ukurasa ya mwisho ya hii broshua iko na ulizo, sawa vile tu matrakte yetu inapangwa. Unaweza kufanya hivi:

  • Uliza ulizo yenye kuwa na majibu mbalimbali

  • Soma jibu ya Biblia yenye kuwa mu Zaburi 37:29

  • Muzungumuzie mambo yenye kuwa chini ya sehemu “Baraka Yenye Utapata Wakati ile Maneno Itatimia.” Kama wakati inaruhusu, musome maandiko yenye kuwa pale na kuzungumuzia picha

  • Ku mwisho, uulize hii ulizo: Unaweza Kuamini Mambo Yenye Biblia Inasema?, kisha uanzishe funzo ya Biblia mu somo ya kwanza

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine