Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr25 Mwezi wa 1 uku. 1-13
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2025
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 6-12/1
  • TAREHE 13-19/1
  • TAREHE 20-26/1
  • TAREHE 27/1–2/2
  • TAREHE 3-9/2
  • TAREHE 10-16/2
  • TAREHE 17-23/2
  • TAREHE 24/2–2/3
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2025
mwbr25 Mwezi wa 1 uku. 1-13

Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 6-12/1

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ZABURI 127-134

Bazazi​—Muendelee Kuhangaikia Batoto Yenu

w21.08 uku. 5 fu. 9

Furahia Fasi Yako mu Familia ya Yehova

9 Yehova alipatia watu uwezo wa kuwa na watoto na daraka ya kuwafundisha wamupende na kumutumikia. Kama uko muzazi, uko mwenye shukrani juu ya hii zawadi ya muzuri sana? Hata kama Yehova alipatia malaika uwezo mingi, tusisahau kama malaika hawana uwezo wa kuwa na watoto. Kama wanachunga ile wazo mu akili, wazazi watasamini daraka ya maana sana yenye wako nayo, ni kusema, kukomalisha watoto wao “katika nizamu na maonyo ya Yehova.” (Efe. 6:4; Kum. 6:5-7; Zb. 127:3) Ili kusaidia wazazi, tengenezo ya Mungu inatoa vyombo mbalimbali vyenye kutegemea Biblia, kama vile vichapo, video, muziki na mambo ingine yenye kuwa ku site yetu. Kusema kweli, Baba yetu wa mbinguni na mwana wake wanapenda vijana sana. (Lu. 18:15-17) Wakati wazazi wanamutegemea Yehova na wanafanya yao yote ili kuhangaikia watoto wao, ile inamufurahisha Yehova. Wanasaidia pia watoto wao kuwa mu familia ya Yehova milele!

w19.12 uku. 27 fu. 20

Wazazi, Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova

20 Ujue muzuri watoto wako. Zaburi ya 127 inalinganisha watoto na mishale. (Soma Zaburi 127:4.) Mishale inaweza kufanyizwa na vitu tofauti-tofauti na inaweza kuwa na ukubwa tofauti-tofauti; vilevile kila mutoto iko tofauti kabisa na mwenzake. Njo maana wazazi wanapaswa kujua namna ya kufundisha kila mutoto. Bibi na bwana fulani mu inchi ya Israeli ya leo wenye waliweza kusaidia watoto wao wawili wamutumikie Yehova wanaonyesha jambo lenye liliwasaidia. Wanasema hivi: “Tulikuwa tunajifunza Biblia na kila mutoto kipekee.” Kwa kweli, kila kichwa cha familia ataamua kama ni lazima ao kama inawezekana kujifunza na watoto kwa njia hiyo.

Mali ya Kiroho

it-1 uku. 543

Mimea ya Mu Biblia

Muandikaji moya wa zaburi aliahidi hivi bale benye kumuogopa Yehova: “Wana wako watakuwa kama machipukizi ya muzeituni kuzunguka meza yako.” (Zb 128:1-3) Wakati aliandikaka ile maneno, alikuwa nafikiria namna mizeituni inaotaka. Kwa kuotesha miti ya mupya ya mizeituni banakataka machipukizi ku muti wa zamani. Tena muzeituni wa zamani unaweza kutokeza machipukizi ku mizizi na kisha mizeituni inakuwa ya mingi. Namna ile machipukizi inaotaka njo muandikaji wa zaburi alifananisha na namna batoto bangezunguka baba yabo na kuletea familia furaha.

TAREHE 13-19/1

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ZABURI 135-137

“Bwana Wetu Ni Mukubwa Kuliko Miungu Mingine Yote”

w15 15/6 uku. 6 fu. 15

Kristo Nguvu za Mungu

15 Yehova mwenyewe ndiye alimupatia Yesu nguvu; kwa hiyo, tuko hakika kwamba Mungu Mweza-Yote iko na uwezo mwingi sana wa kuzuia nguvu za asili. Tufikirie mifano fulani. Mbele ya Garika kuanza, Yehova alisema hivi: ‘Baada ya siku 7 nitanyesha mvua duniani siku 40 muchana na usiku.’ (Mwa. 7:4) Vilevile kwenye Kutoka 14:21, tunasoma hivi: “Yehova akaanza kuifanya bahari irudi nyuma kwa upepo wenye nguvu wa mashariki.” Na kwenye Yona 1:4, tunasoma hivi: ‘Yehova mwenyewe akavumisha [akaleta] upepo mukubwa baharini, kukawa na tufani [zoruba] kubwa baharini; nayo meli [mashua] ikawa karibu kuvunjika.’ Ni jambo lenye kutia moyo sana kujua kwamba katika dunia mupya, sikuzote Yehova atazuia nguvu za asili.

w21.11 uku. 6 fu. 16

Upendo Mushikamanifu wa Yehova Uko na Faida Gani Kwako?

16 Wakati tunakumbuka kama Yehova ni kimbilio yetu, ile inafanya tujisikie salama. Lakini wakati fulani, tunaweza kuvunjika moyo na kukosa ya kufanya. Kama ile inatufikia, namna gani Yehova atatusaidia? (Soma Zaburi 136:23.) Ataweka mikono yake chini yetu, ni kusema, atatuinua, na atatusaidia ili tusiendelee kuvunjika moyo. (Zb. 28:9; 94:18) Faida yenye tunapata: Kujua kama tunaweza kumutegemea Yehova kila mara, kunatuhakikishia kama atatusaidia mu njia mbili. Njia ya kwanza, hata tuishi wapi Yehova atatulinda. Njia ya pili, Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo, atatuhangaikia kabisa.

Mali ya Kiroho

it-2 uku. 1175

Yah

Mara mingi, neno Yah inatumiwa wakati mutu anamusifu Mungu na kuimba ao wakati anasali na kumulilia Mungu. Ile neno inapatikana mara mingi mu maandishi yenye inazungumuzia furaha kisha kupata ushindi ao kukombolewa, ao pia kisha kujionea mukono wenye nguvu wa Mungu na nguvu zake. Kuko mifano ya mingi yenye inaonyesha matumizi ya ile neno mu ile namna. Musemwa “Mumusifu Yah!” (Haleluya) inatumiwa mara mingi juu ya kumusifu Mungu, na inapatikana mara mingi mu kitabu ya Zaburi. Kwa mara ya kwanza inapatikana mu Zaburi 104:35. Mu mafasi ingine mu zaburi, inapatikana ku mwanzo tu (Zb 111, 112), wakati fulani mu katikati (135:3), na wakati ingine ku mwisho tu (Zb 104, 105, 115-117), lakini mara mingi inapatikana ku mwanzo na ku mwisho (Zb 106, 113, 135, 146-150). Mu kitabu ya Ufunuo, bamalaika banarudilia ile musemwa mara kwa mara wakati biko namusifu Yehova.​—Ufu 19:1-6.

Onyesho: Je, Mashahidi wa Yehova Ni Wakristo?

ijwfq 7

Je, Ninyi Ni Wakristo?

Ndiyo. Sisi ni Wakristo sababu:

● Tunajikaza kufuata kabisa-kabisa mafundisho na mwenendo wa Yesu Kristo.​—1 Petro 2:21.

● Tunaamini kwamba Yesu ndiye ufunguo wa kupata wokovu, na kwamba “hakuna jina lingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu ambalo kupitia hilo lazima sisi tupate kuokolewa.”​—Matendo 4:12.

● Watu wanabatizwa katika jina la Yesu ili kuwa Mashahidi wa Yehova.​—Mathayo 28:18, 19.

● Tunasali kupitia jina la Yesu.​—Yohana 15:16.

● Tunaamini kwamba Yesu ndiye Kichwa, ao ndiye aliyepewa mamlaka juu ya kila mutu.​—1 Wakorintho 11:3.

Hata hivyo, kuna mambo mengi yanayotutofautisha na dini zingine zinazojiita za Kikristo. Kwa mufano, tunaamini kwamba Biblia inafundisha kama Yesu ni Mwana wa Mungu, yeye si sehemu ya Utatu. (Marko 12:29) Tunaamini kwamba nafsi inakufa, na kwamba hakuna andiko lolote linaonyesha kama Mungu anawatesa watu katika moto wa milele, na hatuamini kwamba wale wanaoongoza katika makanisa wanapaswa kuwa na macheo yanayowainua juu ya wengine.​—Mhubiri 9:5; Ezekieli 18:4; Mathayo 23:8-10.

TAREHE 20-26/1

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ZABURI 138-139

Usiache Boga Ikuzuie

w19.01 uku. 10 fu. 10

Umusifu Yehova Katika Kutaniko

10 Unasikiaka moyo wako unapiga-piga kila wakati unafikiria kutia mukono juu ili kutoa majibu? Kama ni vile, haiko wewe tu. Kusema kweli, wengi kati yetu wanasikiaka woga kwa kadiri fulani wakati wanatoa majibu. Mbele upiganishe woga huo, unapaswa kujua ni juu ya nini unaogopaka. Unaogopa kuwa utasahau mambo yenye unapenda kusema ao kama utasema mambo yenye makosa? Unaogopa kuwa maelezo yako haitakuwa ya muzuri kama ya wengine? Kwa kweli, kuogopa vile inaweza kuwa alama ya muzuri. Inaonyesha kama uko munyenyekevu na kama unaona wengine kuwa wazuri zaidi kukupita. Yehova anapenda ile sifa. (Zb. 138:6; Flp. 2:3) Lakini, Yehova anapenda pia umusifu na kutia moyo ndugu na dada zako ku mikutano. (1 Te. 5:11) Anakupenda na atakupatia uhodari wenye uko nao lazima.

w23.04 uku. 21 fu. 7

Tutiane Moyo ku Mikutano

7 Inaweza kuwa muzuri kujikumbusha mapendekezo fulani yenye kuwa mu habari za Munara wa Mulinzi zenye tulishajifunza. Kwa mufano, ujitayarishe muzuri. (Mez. 21:5) Kama unaelewa muzuri habari, itakuwa mwepesi kwako kutoa maelezo. Tena, utayarishe maelezo ya mufupi. (Mez. 15:23; 17:27) Maelezo ya mufupi itakusaidia usiogope sana wakati uko naitoa. Maelezo ya mufupi, pengine yenye kuwa na musemwa moya ao mbili inaweza kuwa hata mwepesi kwa ndugu na dada zako kuelewa kuliko maelezo ya murefu yenye kuwa na mawazo mingi. Wakati unatoa maelezo ya mufupi mu maneno yako, utaonyesha kama ulijitayarisha muzuri na kama ulielewa habari muzuri.

Mali ya Kiroho

it-2 uku. 490 fu. 10

Musamaha

Mukristo anapaswa kusamehe bengine hata kama banamukosea mara ngapi. (Lu 17:3, 4; Efe 4:32; Kol 3:13) Mungu hakuwake nasamehe bale benye banakatala kusamehe bengine. (Mt 6:14, 15) Lakini, hata wakati mutu anafanya zambi nzito na anafikia kutengwa na ushirika, kwa wakati wenye kufaa anaweza kusamehewa kama tu anaonyesha kuwa ametubu kikweli. Na akifanya vile, bote mu kutaniko banaweza kumuhakikishia kama banamupenda. (1Ko 5:13; 2Ko 2:6-11) Hata vile, Bakristo habapaswe kusamehe batu benye kufanya zambi nzito kimakusudi juu bale batu banakuwa baadui ya Mungu.​—Ebr 10:26-31; Zb 139:21, 22.

Hotuba: Nakuwaka Mutu wa Haya​—Nifanye Nini?

ijwyp 105

Nakuwaka Mutu wa Haya​—Nifanye Nini?

Jua kwanza nini njo inafanyaka uogope

Haya inaweza kufanya uogope kuzungumuza na watu uso kwa uso. Ile inaweza kufanya uone kama hauwezi kufanya urafiki na wengine, uone sawa vile uko peke yako mu chumba yenye muko giza. Ile inaweza kukuogopesha. Lakini ukijua muzuri jambo yenye inafanyaka uogope, utavumbua kama hauna sababu ya kuogopa.

Namna ya kupiganisha haya

● Usijilinganishe na wengine. Haiko lazima ukuwe mutu wa kusema-sema sana. Lakini, kusudi yako ikuwe kupiganisha haya yako juu usikose kufurahia urafiki wa muzuri na mambo ya wengine yenye kutia moyo.

“Haiko lazima mazungumuzo ikuwe ya murefu na ionekane kama weye njo uko unaiongoza. Usalimie mutu mwenye haujue na ujikaze mujuane ao unaweza kumuuliza maulizo kidogo.”​—Alicia.

Kanuni ya Biblia: “Kila mutu achunguze matendo yake mwenyewe, kisha atakuwa na sababu ya kufurahi juu yake yeye mwenyewe, na hapana kwa kujilinganisha na mutu mwingine.”​—Wagalatia 6:4.

● Ukuwe unaangalia mambo yenye iko inapitikana pembeni yako. Angalia watu wenye wanajuaka sana kufanya urafiki na uone vile wanazungumuzaka na wengine. Nini njo walifanya muzuri? Nini njo hawakufanya muzuri? Ni njia gani yenye wanatumiaka ili kuanzisha mazungumuzo, na weye unaweza kuwaiga namna gani?

“Angalia watu wenye wanajuaka sana kufanya urafiki na ufuate mufano wao. Ona vile wako wanatenda, mambo yenye wanaambia mutu mwenye wanaona kwa mara ya kwanza.”​—Aaron.

Kanuni ya Biblia: “Kama vile chuma kinanoa chuma, ni vile pia mutu ananoa rafiki yake.”​—Mezali 27:17.

● Uliza maulizo. Kwa kawaida, watu wanapendaka kusema byenye banawaza juu ya mambo fulani. Kwa hiyo, kuwauliza maulizo ni njia ya muzuri ya kuanzisha mazungumuzo nao. Inasaidiaka pia watu wasikaze akili sana juu yako.

“Ukijitayarisha mbele ya wakati, ile inaweza kukusaidia upunguze wasiwasi. Unaweza hata kufikiri mbele ya wakati juu ya habari fulani ao maulizo fulani yenye utatumia wakati mutakutana na marafiki fasi fulani ao wakati utakutana na watu wenye haujue.”​—Alana.

Kanuni ya Biblia: “Mukiendelea kuangalia, hapana faida zenu ninyi wenyewe tu, lakini pia faida za wengine.”​—Wafilipi 2:4.

TAREHE 27/1–2/2

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ZABURI 140-143

Tenda Kupatana na Sala Zako

w22.02 uku. 12 fu. 13-14

“Usikilize Maneno ya Wenye Hekima”

13 Uone shauri kuwa njia ya Mungu ya kutuonyesha upendo. Yehova anatutakia mambo ya muzuri zaidi. (Mez. 4:20-22) Wakati anatushauria kupitia Neno yake, kichapo fulani yenye inategemea Biblia, ao kupitia muamini fulani mukomavu, ni njia ya kutuonyesha upendo. Waebrania 12:9, 10 inasema: “Yeye anafanya vile kwa faida yetu.”

14 Ukazie akili shauri, hapana namna ilitolewa. Wakati fulani tunaweza kuwaza kama, hawakututolea shauri mu njia ya muzuri zaidi. Kusema kweli, kila mutu mwenye anatoa shauri anapaswa kujikaza kufanya ile shauri ikuwe mwepesi kadiri inawezekana juu ikubaliwe. (Gal. 6:1) Lakini kama ni siye njo wanatushauria tunapaswa kufikiria mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia ile shauri hata kama tunawaza kuwa mutu mwenye alitutolea ile shauri angepaswa kufanya vile mu njia ya muzuri zaidi. Pengine tunaweza kujiuliza hivi: ‘Hata kama sikupenda namna shauri ilitolewa kuko jambo fulani naweza kujifunza kupitia mambo yenye ilisemwa? Je, naweza kutia pembeni makosa ya mutu mwenye alinitolea shauria na kujifunza mambo fulani kupitia shauri yake?’ Ni jambo ya hekima kwetu kutafuta njia fulani ya kupata faida kupitia shauri yoyote yenye wanatutolea.​—Mez. 15:31.

w10-SW 15/3 uku. 32 fu. 4

Dumisha “Usafi wa Moyo” Katika Nyakati Hizi za Hatari

Mkazo kutoka kwa wapinzani, matatizo ya kiuchumi, na ugonjwa mbaya umefanya watumishi fulani wa Mungu wavunjike moyo. Pindi fulani, mambo kama hayo yamekuwa pia na matokeo mabaya kwa mioyo yao. Hata Mfalme Daudi alikabili hali kama hiyo, alisema hivi: “Roho yangu inazimia ndani yangu; moyo wangu wenyewe umekufa ganzi katikati yangu.” (Zab. 143:4) Nini kilichomsaidia kukabiliana na nyakati kama hizo? Daudi alikumbuka jinsi Mungu alivyokuwa amewatendea watumishi Wake na jinsi yeye mwenyewe alivyokombolewa. Alitafakari jinsi Yehova alivyokuwa ametenda kwa ajili ya Jina lake kuu. Daudi aliendelea kuhangaikia kazi za Mungu. (Zab. 143:5) Vivyo hivyo, kutafakari kuhusu Muumba wetu na yote ambayo tayari ametufanyia na anaendelea kutufanyia, kutatusaidia hata tunapojaribiwa.

w15 15/3 uku. 32 fu. 2

Amri ya Kuoa ao Kuolewa “Katika Bwana Tu” Ingali Yenye Kufaa?

Wakati fulani, unaweza kujisikia kama mutunga-zaburi Daudi, mwenye alisema hivi: “Ufanye haraka, unijibu, Ee Yehova; roho yangu imefikia mwisho. Usiufiche uso wako mbali nami.” (Zab. 143:5-7, 10) Katika hali kama hizo, umuachie Baba yako wa mbinguni wakati ili akuonyeshe anapenda ufanye nini. Unaweza kufanya hivyo kwa kuchukua wakati wa kusoma Neno lake na kutafakari sana juu ya mambo yenye unasoma. Utajua amri zake na utaona namna aliwatendea watumishi wake wa zamani. Ukimusikiliza, utakuwa hakika zaidi kwamba kumutii ni jambo la hekima.

Mali ya Kiroho

it-2 uku. 1134

Sumu

Matumizi ya Mufano. Maneno ya bongo ya batu babaya, yenye inaweza kuharibishia bengine sifa, inafananishwa na sumu ya nyoka. (Zb 58:3, 4) Sumu ya nyoka inatokeaka nyuma ya mudomo na meno yake ya yulu. Njo maana, kuhusu batu benye kusingizia bengine Biblia inasema kama “sumu ya nyoka iko nyuma ya midomo yao.” (Zb 140:3; Ro 3:13) Kama mutu anatumia ulimi wake mubaya juu ya kusingizia bengine, kusema mutu mubaya juu ya kumuharibishia sifa, kueneza mafundisho ya bongo, ao kusema maneno ingine tu ya mubaya, ulimi wake “umejaa sumu yenye kuua.”​—Yak 3:8.

Onyesho: Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawaitikake Kutiwa Damu mu Mishipa?

ijwfq 21

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawaitikake Kutiwa Damu mu Mishipa?

Mawazo ya watu wengi

● Uongo: Mashahidi wa Yehova wanakatalaka kutumia dawa na wanakatalaka kuenda ku hopitale juu ya kupata matunzo.

Ukweli: Siye Mashahidi wa Yehova tunajikazaka kutafuta matunzo ya muzuri juu yetu na juu ya familia zetu. Wakati tunagonjwa tunaendaka kwa wanganga wenye wako na uwezo wa kututunza ao kufanya upasuaji bila kutia damu. Tunafurahia maendeleo yenye imefanywa mu kinganga. Kusema kweli, kutunza bila kutia damu kuko nasaidia watu wengi, hapana tu Mashahidi wa Yehova. Mu inchi mingi, mugonjwa yeyote anaweza kuchagua kutunzwa bila kutiwa damu juu ya kuepuka hatari za kupata magonjwa yenye inaweza kutokana na damu, juu ya kuepuka magumu ingine ya afya, ao matatizo ingine yenye inaweza kutokea juu muganga alidanganyika.

● Uongo: Mashahidi wa Yehova wanaamini kama mutu atapona ikiwa tu iko na imani.

Ukweli: Hatuponyeshake watu kimuujiza.

● Uongo: Kutunza bila kutia damu kuko na bei sana.

Ukweli: Kutunza bila kutia damu hakuna bei sana.

● Uongo: Mashahidi wengi, kutia ndani watoto, wanakufaka kila mwaka juu wanakatalaka kutiwa damu mu mishipa.

Ukweli: Ile maneno ni ya uongo kabisa. Wanganga wanafanyaka upasuaji wa nguvu, sawa vile upasuaji wa moyo, upasuaji wa mifupa, na kunenepesha viungo fulani vya mwili bila kutia damu. Wagonjwa, kutia ndani watoto, wenye wanakatalaka kutiwa damu mara mingi wanaponaka haraka ao muzuri zaidi kupita wale wenye waliitika kutiwa damu mu mishipa. Kwa hiyo, hakuna mutu mwenye anaweza kuhakikisha kama mugonjwa atakufa juu anakatala kutiwa damu ao atapona juu anaitika kutiwa damu.

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawaitikake Kutiwa Damu mu Mishipa?

Ni juu ya mambo yenye tunaamini. Mu Biblia muko amri yenye kusema kama tunapaswa kujiepusha na damu. (Mwanzo 9:4; Mambo ya Walawi 17:10; Kumbukumbu la Torati 12:23; Matendo ya Mitume 15:28, 29) Tena, ku macho ya Mungu, damu ni uzima. (Mambo ya Walawi 17:14) Kwa hiyo, tunakatalaka kutiwa damu juu tunatii Mungu na tunamuheshimia kwa sababu yeye njo Chanzo ya uzima.

Walibadilisha namna ya kutunza

Zamani wanganga walikuwa nawaza kama kutunza bila kutumia damu ni kutia maisha ya mugonjwa mu hatari, lakini kulishapita miaka fulani tangu ile mawazo ibadilike. Kwa mufano, mu mwaka wa 2004, habari fulani yenye iliandikwa mu gazeti ya elimu ya wanganga ilisema hivi: “Ufundi wa kutunza bila kutia damu, wenye ulikuwa unatumiwa juu ya kutunza wagonjwa Mashahidi wa Yehova, utaanza pia kutumiwa juu ya kutunza wengine wenye hawako Mashahidi mu miaka yenye iko nakuya.” Mu mwaka wa 2010 habari moya ya mu gazeti Heart, Lung and Circulation ilisema hivi: “‘Hatutakuwa tunatunza tu Mashahidi wa Yehova bila kutumia damu,’ tutakuwa tunafanya vile pia kwa watu wengine wenye hawako Mashahidi wa Yehova.”

Leo wanganga wengi sana wako natumia njia yenye inafanya damu ya mugonjwa isikuwe inavuya sana wakati wa upasuaji. Ile njia inatumiwa mu inchi mingi zenye kuendelea, na hata wagonjwa wenye hawako Mashahidi wa Yehova wanaitumiaka.

TAREHE 3-9/2

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ZABURI 144-146

‘Benye Furaha Ni Bale Benye Mungu Wabo Ni Yehova!’

w18.04 uku. 32 fu. 3-4

Maulizo Ya Wasomaji Wetu

2. Maneno yenye kuwa katika tafsiri ya sasa yanategemea maana ya maneno na grama ao sarufi. Neno lenye kuunganisha Zaburi 144:12-15 na mustari wenye kutangulia, linategemea maana yenye neno la kwanza katika mustari wa 12 linapewa, ni neno la Kiebrania asher. Neno asher linaweza kutafsiriwa katika njia mbalimbali. Kwa mufano, linaweza kuelewaka kuwa neno lenye kutumiwa ili kuonyesha mutu mwenye kuzungumuziwa, neno kama vile “mwenye” ao “wenye.” Neno hilo lilipewa maana ya “wenye” katika tafsiri ya zamani. Kwa hiyo, vitu vizuri vyenye kutajwa katika mustari wa 12 mupaka wa 14 vilihusu waovu wenye walitajwa katika mustari wenye kutangulia. Lakini, neno asher linaweza pia kuonyesha matokeo na linaweza kutafsiriwa “kwa hiyo,” “ili,” ao “halafu.” Tafsiri ya sasa ya mwaka wa 2013 inatumia neno “halafu” na tafsiri zingine za Biblia zinafanya hivyo pia.

3. Namna inatafsiriwa katika tafsiri ya sasa inapatana kabisa na mistari ingine yote ya zaburi hiyo. Kutumia neno “halafu” katika mustari wa 12 kunamaanisha kwamba inaeleweka kama baraka zenye kufuata katika mustari wa 12 mupaka 14 zinahusu watu wenye haki, ni kusema, wale wenye wanaomba ‘kuwekwa huru na kukombolewa’ kutoka kwa waovu (mustari wa 11). Badiliko hilo linaonekana pia kwenye mustari wa 15 kwenye neno “furaha” linapatikana mara mbili na linapatana sasa katika njia ya muzuri. Kwa hiyo, nafasi hizo zote furaha hiyo inahusu watu walewale, ni kusema, wale “ambao Mungu wao ni Yehova!” Ukumbuke kama, maandishi ya zamani ya Kiebrania hayakuwa na alama za maandishi kama vile alama za kunukuu ao zenye kuonyesha maneno yenye mutu fulani alisema. Kwa hiyo, watafsiri wanapaswa kutafuta maana ya kweli ya maneno hayo, kwa kufikiria namna ya kuandika kwa njia ya shairi (poeme) katika Kiebrania, habari yenye kuzungumuziwa, na maandiko mengine ya Biblia yenye kuzungumuzia habari hiyo.

w22.10 uku. 28 fu. 16-17

Utie Nguvu Tumaini Yako ya Kikristo

16 Tumaini yetu ya uzima wa milele ni zawadi ya maana sana kutoka kwa Mungu. Tunangojea maisha ya muzuri sana, na ile ni jambo ya hakika. Tumaini yetu iko sawa vile nanga. Inatusaidia tusiyumbe-yumbe, lakini tuweze kuvumilia magumu, mateso, na hata kifo. Tumaini yetu iko sawa vile kofia ya chuma. Inalindaka akili yetu juu tuweze kuachana na mambo ya mubaya na kushikamana na mambo ya muzuri. Tumaini yenye Biblia inatupatia inatusaidia tumujue Mungu zaidi, na inatuonyesha kama Yehova anatupenda sana. Tunapata faida sana wakati tunatia nguvu tumaini yetu.

17 “Mu barua yenye mutume Paulo aliandikia Waroma, alitia Wakristo moyo ‘wafurahi katika tumaini.’ (Ro. 12:12) Paulo aliweza kufurahi juu alikuwa hakika kama ikiwa angeendelea kuwa mushikamanifu, angeweza kupata uzima wa milele mbinguni. Na siye pia tunaweza kufurahi katika tumaini juu tuko hakika kama Yehova atatimiza ahadi zake. Sawa vile mutunga-zaburi aliandika, “mwenye furaha ni ule . . . mwenye anamutumainia Yehova Mungu wake, . . . yeye mwenye kuwa muaminifu sikuzote.”​​—Zb 146:5, 6.

w18.01 uku. 26 fu. 19-20

Ni Upendo wa Aina Gani Wenye Kuleta Furaha ya Kweli?

19 Kisha wanadamu kuteseka kwa miaka 6000 hivi, ulimwengu wa Shetani unakaribia mwisho wake. Dunia inajaa watu wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, na wenye kupenda raha. Wanafikiria mambo yenye wanaweza kupata na wanafanya tamaa zao kuwa jambo la maana zaidi katika maisha yao. Watu kama hao hawawezi kuwa na furaha ya kweli hata kidogo. Lakini, Biblia inasema hivi: ‘Mwenye furaha ni yule ambaye Mungu wa Yakobo ni musaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yehova Mungu wake.’​—Zab. 146:5.

20 Watu wa Yehova wanaendelea kumupenda, na hesabu yetu inaendelea kuongezeka kila mwaka. Huo ni ushuhuda wenye kuonyesha kama Ufalme wa Mungu unatawala, na kama hivi karibuni utaleta baraka za ajabu duniani. Kufanya mapenzi ya Mungu ndiyo kunaleta furaha ya kweli na yenye kuendelea, kwa sababu tunajua kama tunamupendeza Ule Mwenye Kuwa Juu Zaidi. Na wale wenye kumupenda Yehova watakuwa na furaha milele! Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia tabia mbalimbali zenye kuletwa na upendo wenye uchoyo na tutaona namna gani tabia hizo ni tofauti na sifa zenye watu wa Yehova wanaonyesha.

Mali ya Kiroho

bh uku. 128 fu. 9

Mawazo ya Mungu juu ya Uzima

Tuseme nini juu ya uzima wa wanyama? Huo pia ni kitu kitakatifu machoni pa Muumbaji. Mungu anakubali tuue wanyama ili tupate chakula na mavazi ao ikiwa munyama anaweza kuhatarisha maisha ya watu. (Mwanzo 3:21; 9:3; Kutoka 21:28) Lakini, kutesa wanyama ao kuwaua kwa sababu ya kujifurahisha tu ni vibaya; kufanya hivyo ni kukosa kuheshimu utakatifu wa uzima.​—Methali 12:10.

TAREHE 10-16/2

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ZABURI 147-150

Tuko na Sababu za Mingi za Kumusifu Yah

w17.07 uku. 18 fu. 5-6

‘Musifu Yah!’​—Sababu Gani?

5 Yehova hakufariji tu taifa la Israeli wakiwa kikundi, lakini alifariji pia kila mutu mumoja-mumoja. Anafanya hivyo pia leo. Muandikaji wa zaburi aliandika hivi juu ya Mungu: “Anawaponya wenye mioyo iliyovunjika, naye anafunga sehemu zao zenye maumivu.” (Zab. 147:3) Kwa kweli, Yehova anahangaikia wale wenye kuwa na matatizo ya kimwili ao ya moyoni. Leo, Yehova anatamani sana kutufariji na kutuliza maumivu ya vidonda vyetu vya moyoni. (Zab. 34:18; Isa. 57:15) Anatupatia hekima na nguvu ili tupambane na magumu yoyote yenye tunaweza kupata.​—Yak. 1:5.

6 Kisha muandikaji wa zaburi anakazia akili yake juu ya mbingu na kutuambia kuwa Yehova “anahesabu idadi ya nyota” na “anaziita kwa majina yake.” (Zab. 147:4) Sababu gani inaonekana kuwa anabadilisha habari yenye alikuwa anazungumuzia na kuanza kuzungumuzia nyota za mbinguni? Fikiria jambo hili: Muandikaji wa zaburi angeweza kuona nyota na macho yake, lakini hangeweza kujua kabisa hesabu ya nyota hizo. Kadiri miaka inapita, hesabu ya nyota zenye tunaweza kuona imeongezeka sana. Watu fulani wanawaza kuwa galaksi yetu iko na mamiliare ya nyota. Na kunaweza kuwa trilioni ya magalaksi katika ulimwengu wote muzima! Sisi hatuwezi kujua kabisa hesabu ya nyota! Lakini Muumbaji anazipatia zote majina ao utambulisho. Hilo linamaanisha kuwa Yehova anajua muzuri kila nyota. (1 Ko. 15:41) Tuseme nini juu ya wanadamu wenye aliumba hapa duniani? Mungu anajua nafasi kwenye kila nyota inapatikana kwa wakati fulani na anakujua pia kipekee; anajua muzuri nafasi kwenye unapatikana kabisa, namna unajisikia kabisa, na mambo yenye uko nayo lazima kabisa kwa wakati fulani!

w17.07 uku. 18 fu. 7

‘Musifu Yah!’​—Sababu Gani?

7 Yehova hakuhangaikie tu kipekee, lakini pia iko na huruma na nguvu ya kukusaidia wakati uko na magumu katika maisha. (Soma Zaburi 147:5.) Unaweza kujisikia kuwa hali yako ni ngumu sana na muzigo ni muzito sana kwako kubeba. Mungu anaelewa mipaka yako, na ‘anakumbuka kwamba wewe ni mavumbi.’ (Zab. 103:14) Kwa sababu hatukamilike, tunafanya makosa yaleyale tena na tena. Wakati fulani, tunahuzunika kwa sababu tulitumia ulimi wetu mubaya, kwa sababu ya tamaa fulani za kimwili zenye kurudia tena na tena, ao muelekeo wa kutamani mambo yenye wengine wako nayo! Yehova hana uzaifu kama huo; lakini anaelewa muzuri zaidi namna tunajisikia kuliko namna tunaweza kuwazia!​—Isa. 40:28.

w17.07 uku. 21 fu. 18

‘Musifu Yah!’​—Sababu Gani?

18 Muandikaji wa zaburi alijua namna Mungu alipenda watu wake wa zamani, taifa la Israeli. Hilo tu ndilo taifa lenye Mungu alipatia “neno” lake na “maamuzi yake ya hukumu.” (Soma Zaburi 147:19, 20.) Leo, tumebarikiwa kwa sababu katika dunia yote, ni sisi tu ndio wenye kuitwa kwa jina la Mungu. Kumujua Yehova na kutumia Neno lake katika maisha yetu kumetusaidia tufurahie pendeleo la kuwa na urafiki pamoja naye. Kwa kweli, kama vile muandikaji wa Zaburi ya 147, uko na sababu nyingi za muzuri za kusema kwa sauti kubwa ‘Musifu Yah!’ na kutia wengine moyo wafanye hivyo.

Mali ya Kiroho

w23.03 uku. 17 fu. 6

Ujifunze Mambo Mingi Zaidi juu ya Yehova Kupitia Uumbaji

Yehova amepanga wakati. Kila mwaka, kati ya mwisho wa Mwezi wa pili na mu katikati ya Mwezi wa tano, Waisraeli walikuwa naona korongo wenye walikuwa naruka na kuhamia upande wa kaskazini. Mungu aliambia Waisraeli kama “korongo katika anga anajua vipindi vyake.” (Yer. 8:7) Sawa vile tu Yehova amepanga wakati juu ya wale ndege, ameweka pia wakati yenye ataleta hukumu. Leo, kuangalia ndege wenye wako nahama kunafanya tutumainie kabisa kama Yehova “ameweka wakati” ya kuharibu huu ulimwengu muovu.​​—Hab. 2:3.

Hotuba: Umusikilize Yesu​—Hubiri Habari Njema

w19.03 uku. 10 fu. 7-11

7 Soma Matayo 17:1-5. Mara ya pili yenye Yehova alisema kutoka mbinguni ilikuwa wakati Yesu ‘aligeuzwa sura.’ Yesu alikuwa amealika Petro, Yakobo, na Yohana wamusindikize juu ya mulima murefu. Wakati walikuwa kule, waliona maono ya ajabu. Sura ya Yesu na nguo zake vilingaa sana. Watu wawili, wenye walifananisha Musa na Eliya, wakaanza kuzungumuza na Yesu juu ya kifo chenye kingemupata na juu ya ufufuo wake. Hata kama mitume hao tatu walikuwa “wamelemewa na usingizi,” waliona ile maono ya kushangaza wakati walikuwa macho kabisa. (Lu. 9:29-32) Kisha, wingu lenye kungaa likawafunika, na wakasikia sauti kutoka katika lile wingu, ilikuwa sauti ya Mungu! Kama vile Yehova alifanya wakati Yesu alibatizwa, mara hii tena alisema kama alimukubali Mwana wake na kumupenda. Alisema hivi: “Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali.” Lakini mara hii Yehova aliongeza hivi: “Mumusikilize.”

8 Ile maono ilionyesha utukufu na uwezo wenye Yesu angekuwa nao wakati wenye kuja wakati angekuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Kwa kweli, Kristo alitiwa moyo na alitiwa nguvu ili kuvumilia mateso na kifo chenye maumivu chenye kingemupata. Pia, ile maono ilitia nguvu imani ya wanafunzi. Hilo liliwasaidia wajitayarishe juu ya majaribu ya uaminifu-mushikamanifu yenye ingewapata na kazi ya nguvu yenye wangepaswa kufanya kwa miaka mingi. Miaka 30 hivi kisha pale, mutume Petro alizungumuzia ile maono ya kugeuzwa sura, na hilo lilionyesha kama alikuwa angali anaikumbuka kabisa.​—2 Pe. 1:16-18.

9 “Mumusikilize.” Yehova alionyesha wazi kama anapenda tusikilize maneno ya Mwana wake na tuitii. Yesu alisema nini wakati alikuwa ku dunia? Alisema mambo mingi ya maana yenye tunapaswa kusikiliza! Kwa mufano, kwa upendo alifundisha wanafunzi wake namna ya kuhubiri habari njema, na mara kwa mara aliwakumbusha waendelee kukesha. (Mt. 24:42; 28:19, 20) Pia, aliwaomba wajikaze sana, na aliwatia moyo wasichoke. (Lu. 13:24) Yesu alikazia kama ni jambo la lazima wanafunzi wake wapendane, waendelee kuwa na umoja, na kushika amri zake. (Yoh. 15:10, 12, 13) Ile mashauri yenye Yesu alitolea wanafunzi wake ilikuwa yenye kufaa kabisa! Na ni ya maana sana leo kama vile tu ilikuwa wakati Yesu aliitoa.

10 Yesu alisema hivi: “Kila mutu mwenye iko upande wa ile kweli anasikiliza sauti yangu.” (Yoh. 18:37) Tunaonyesha kama tuko tunasikiliza sauti yake wakati ‘tunaendelea kuvumiliana na kusameheana kwa kupenda.’ (Kol. 3:13; Lu. 17:3, 4) Tena, tunaonyesha kama tuko tunasikiliza sauti yake wakati tunahubiri habari njema kwa bidii “katika nyakati zenye kufaa na nyakati zenye kuwa ngumu.”​—2 Ti. 4:2.

11 Yesu alisema hivi: “Kondoo wangu wanasikiliza sauti yangu.” (Yoh. 10:27) Wanafunzi wa Kristo wanaonyesha kama wanasikiliza sauti ya Yesu kwa kukazia uangalifu maneno yake na kuitii. Hawakengeushwe na “mahangaiko ya maisha.” (Lu. 21:34) Lakini, kutii amri za Yesu njo jambo lenye wanaona kuwa la maana sana mu maisha yao, hata wakati wanapatwa na magumu. Ndugu na dada zetu wengi wanavumilia magumu makali, kutia ndani kushambuliwa na wapinzani, umaskini wa sana, na misiba ya asili. Mu ile magumu yote, wanaendelea kuwa waaminifu, hata kutokee nini. Yesu anawahakikishia hivi: “Kila mutu mwenye kuwa na amri zangu na kuzishika, huyo ndiye mwenye ananipenda. Na kila mutu mwenye ananipenda atapendwa na Baba yangu.”​—Yoh. 14:21.

TAREHE 17-23/2

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 1

Vijana​—Mutamusikiliza Nani?

w17.11 uku. 29 fu. 16-17

Usiache Jambo Lolote Likuzuie Kupata Zawadi

16 Tuseme nini ikiwa uko kijana na unaona kuwa wazazi wako Wakristo hawakuelewe na wamekuwekea vizuizi vingi? Huzuni yako inaweza kukufanya hata ukuwe na mashaka ikiwa kumutumikia Yehova ndilo jambo la maana kabisa katika maisha. Lakini ikiwa unaacha huzuni ikufanye uache kumutumikia Yehova, hautakawia kuona kuwa hakuna mutu mwenye kukuhangaikia kabisa kuliko wazazi wako wenye kumuogopa Mungu na ndugu dada katika kutaniko lako.

17 Ikiwa wazazi wako hawakutolee nizamu hata kidogo, hautajiuliza ikiwa wanakuhangaikia kabisa? (Ebr. 12:8) Lakini pengine ni namna wazazi wako wanakutolea nizamu ndiyo yenye kukukasirisha. Kuliko kukasirika juu ya namna wanakutolea nizamu, ujikaze kuelewa sababu yenye ilifanya wakutolee nizamu katika njia hiyo. Kwa hiyo, ubakie mwenye kutulia na uepuke kabisa kutenda kwa hasira wakati wanasema mambo yenye hayakufurahishe. Neno la Mungu linasema hivi: ‘Yeyote anayezuia maneno yake ana ujuzi, na mutu mwenye utambuzi ana roho ya utulivu.’ (Met. 17:27) Ujiwekee muradi wa kuwa mutu mwenye kukomaa mwenye anaweza kusikiliza mashauri kwa utulivu, na kufaidika nayo bila kuhangaika kupita kiasi juu ya namna yalitolewa. (Met. 1:8) Kuwa na wazazi Mashahidi wenye kumupenda Yehova kabisa ni baraka. Kwa kweli, watakusaidia kupata zawadi ya uzima.

w05-SW 15/2 uku. 19-20 fu. 11-12

Kulinda Utambulisho Wetu wa Kikristo

11 Jitahidi kumpendeza Mungu, si mwanadamu. Ni jambo la kawaida kujitambulisha na kikundi fulani. Kila mtu anahitaji marafiki, na tunapokubaliwa na wengine tunafurahi na kuhisi usalama. Wakati wa kubalehe na pia baadaye maishani, msongo wa marika unaweza kuwa wenye nguvu na kumfanya mtu atake sana kuwaiga au kuwapendeza wengine. Lakini sikuzote marafiki na marika hawapendezwi na hali yetu nzuri. Nyakati nyingine wanataka tu mtu wa kushirikiana naye katika kufanya mabaya. (Methali 1:11-19) Mkristo anaposhindwa na msongo wa marika usiofaa, kwa kawaida yeye hujaribu kuficha utambulisho wake. (Zaburi 26:4) Mtume Paulo alionya hivi: “Usiruhusu ulimwengu unaokuzunguka ufinyange tabia yako.” (Waroma 12:2, The Jerusalem Bible) Yehova huandaa nguvu tunazohitaji ili kupinga mkazo wowote ambao hufanya tujipatanishe na ulimwengu.​—Waebrania 13:6.

12 Mkazo unapotisha kuharibu utambulisho wetu wa Kikristo, tunapaswa kukumbuka kwamba ushikamanifu wetu kwa Mungu ni muhimu zaidi kuliko maoni au maelekeo ya wengi. Maneno haya ya Kutoka 23:2 hutumika kama kanuni ya kutulinda: “Usiufuate umati kwa ajili ya makusudio maovu.” Waisraeli wengi walipotilia shaka uwezo wa Yehova wa kutimiza ahadi Zake, Kalebu alikataa kwa uthabiti kufuata walio wengi. Alikuwa na uhakika kwamba ahadi za Mungu zilikuwa zenye kutegemeka, naye alithawabishwa sana kwa msimamo wake. (Hesabu 13:30; Yoshua 14:6-11) Je, wewe pia uko tayari kupinga mkazo unaotokana na maoni ya wengi ili kulinda uhusiano wako pamoja na Mungu?

Mali ya Kiroho

it-2 uku. 1005

Mupumbavu

Mu Biblia, neno “mupumbavu” haimaanishe mutu mwenye hana akili. Inamaanisha njo mutu mwenye anakatala kufikiri muzuri na mwenye iko na mwenendo wenye haupatane na kanuni za Mungu za haki. Kuko maneno mingi ya Kiebrania yenye inazungumuzia mutu wa vile; kwa mufano kesilʹ (‘mupumbavu; Mez 1:22), ʼewilʹ (“mupumbavu”; Mez 12:15), na·valʹ (‘mupumbavu’; Mez 17:7), na lets (“mwenye kuchekelea”; Mez 13:1). Neno ya Kigiriki aʹphron inamaanisha “pumbavu” (Lu 12:20), a·noʹe·tos ‘mwenye kukosa akili’ (Ga 3:1), na mo·rosʹ ‘mupumbavu.’ (Mt 23:17; 25:2).

TAREHE 24/2–2/3

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 2

Juu ya Nini Unapaswa Kufurahia Funzo ya Kipekee?

w22.08 uku. 18 fu. 16

‘Endelea Kutembea Katika Kweli’

16 Haiko siye wote njo tunapendaka kusoma na kujifunza. Lakini, Yehova anatuomba ‘tuendelee kutafuta’ na ‘kuendelea kutafuta’ juu tuelewe kweli muzuri zaidi. (Soma Mezali 2:4-6.) Wakati tunajikaza kufanya vile, tunapataka tu faida. Corey anasema kama wakati iko nafanya usomaji wake wa Biblia, anakaziaka akili yake ku andiko moya tu. Anasema hivi: “Ninasomaka maelezo yote ya chini, ninasomaka kila referanse, na kufanya utafiti zaidi. . . . Ile inanisaidiaka kujua mambo mingi!” Ikuwe tunajifunza sawa vile Corey ao tunatumia njia ingine, tunaonyesha kama tunaona kweli kuwa ya maana sana kama tunapanga wakati ya kujifunza na tunajikaza sana kufanya vile.​​—Zb. 1:1-3.

w22.10 uku. 19 fu. 3-4

Hekima ya Kweli Inaita Kwa Sauti Kubwa

3 Hekima inaweza kumaanisha uwezo wa kutumia mambo yenye tunajua ili kukamata maamuzi ya muzuri. Lakini, hekima ya kweli inamaanisha mambo mingi zaidi. Biblia inasema hivi: “Kumuogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima, na kumujua Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi ni uelewaji.” (Mez. 9:10) Kwa hiyo, wakati tunataka kukamata maamuzi ya maana, tunapaswa kufikiria kwanza mawazo ya Yehova, ni kusema, kujiuliza kama maamuzi yetu itaonyesha kuwa ‘tunamujua Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi.’ Tunaweza kufanya vile kwa kujifunza Biblia na vichapo vyetu vyenye vinategemea Biblia. Wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tuko na hekima ya kweli.​​—Mez. 2:5-7.

4 Ni Yehova tu njo anaweza kutupatia hekima ya kweli. (Ro. 16:27) Juu ya nini tunaweza kusema kama hekima ya kweli inatoka tu kwake? Kwanza, juu Yehova njo Muumbaji, anajua na kuelewa muzuri sana vitu vyote vyenye aliumba. (Zb. 104:24) Pili, vitu vyote vyenye Yehova aliumba vinaonyesha kama iko na hekima. (Ro. 11:33) Tatu, mashauri yenye hekima ya Yehova sikuzote inaleteaka faida wale wenye wanaitumikisha. (Mez. 2:10-12) Kama tunapenda kupata hekima ya kweli, tunapaswa kukubali zile sababu tatu na kuziacha zituongoze wakati tunatafuta kukamata maamuzi na wakati tunatafuta kufanya jambo fulani.

w16.09 uku. 20 fu. 2-3

Vijana, Mutie Nguvu Imani Yenu

2 Leo, watu wengi hawaamini kama ni Mungu ndiye alituumba. Ikiwa wewe ni kijana mwenye kumutumikia Yehova ao uko unajifunza juu yake, wakati fulani unaweza kujiuliza namna unaweza kuonyesha kama yeye ndiye Muumbaji wetu. Biblia inatusaidia kuwaza sana juu mambo yenye tunasikia ao tunasoma na kufikiri pamoja na wengine juu ya mambo hayo. Neno la Mungu linasema hivi: “Uwezo wa kufikiri utakutunza.” Namna gani? Uwezo huo utakusaidia kupinga mawazo ya uongo na kutia nguvu imani yako kwa Yehova.​—Soma Methali 2:10-12.

3 Ili tukuwe na imani yenye nguvu kwa Yehova, tunapaswa kumujua muzuri. (1 Timotheo 2:4) Kwa hiyo, wakati unasoma Biblia na vichapo vyetu, ni muzuri usimamishe usomaji na kufikiri juu ya mambo yenye unasoma. Ujikaze kuelewa mambo hayo. (Mathayo 13:23) Ikiwa unajifunza kwa njia hiyo, utaona mambo mengi yenye kuhakikisha kama Yehova ndiye Muumbaji wetu na kama Biblia ilitoka kwake. (Waebrania 11:1) Tuone basi namna gani tunaweza kufanya hivyo.

Mali ya Kiroho

it-1 uku. 1195 fu. 4

Uaminifu-Mushikamanifu

Mutu hawezi kuendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu kwa nguvu yake yeye peke; anaweza kufikia vile kama tu iko na imani ya nguvu na anamutumainia kabisa Yehova na nguvu ya Yehova ya kuokoa. (Mez 25:21) Mungu anaahidi kama atakuwa “ngao” na “ngome,” yenye kulinda bale benye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu. (Mez 2:6-8; 10:29; Zb 41:12) Yehova iko nabasaidia baishi maisha yenye kutulia na baendelee kumutumikia bila kukengeushwa juu banapenda kukubaliwa naye. (Zb 26:1-3; Mez 11:5; 28:18) Vile Yobu alisemaka, inahuzunisha kuona kama mutu mwenye hana kosa anaweza kuteseka juu ya utawala mubaya wa banadamu na anaweza hata kufa pamoya na batu babaya. Lakini Yehova anajua maisha ya muaminifu-mushikamanifu na anamuhakikishia kama uriti wake utaendelea, atakuwa na maisha ya muzuri wakati wenye kuya, na atariti bitu bya muzuri. (Yob 9:20-22; Zb 37:18, 19, 37; 84:11; Mez 28:10) Vile ilikuwa kwa Yobu, haiko utajiri njo unafanyaka mutu akuwe wa kuheshimiwa, ni uaminifu-mushikamanifu. (Mez 19:1; 28:6) Batoto benye biko na baba muaminifu-mushikamanifu ni benye furaha (Mez 20:7), juu baba yabo anabaachia uriti muzuri: mufano wake muzuri, na heshima yenye alipata juu alikuwa muaminifu-mushikamanifu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine