Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp21 na. 2 uku. 10-12
  • Mambo Unaweza Kufanya juu Uishi mu Dunia Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo Unaweza Kufanya juu Uishi mu Dunia Mupya
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • JUU UOKOKE UNAPASWA ‘KUFIKIA KUMUJUAʼ MUNGU
  • USOME NENO YA MUNGU, BIBLIA, KILA SIKU
  • UMUOMBE MUNGU AKUSAIDIE
  • Ni Mambo Gani Yenye Mungu Amefanya?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Sababu Gani Yesu Aliteseka na Kufa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Unaweza Kuishi Milele Katika Dunia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
  • Inawezekana Kuishi Milele
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
wp21 na. 2 uku. 10-12

Mambo Unaweza Kufanya juu Uishi mu Dunia Mupya

Mu habari zenye zilitangulia, tuliona kama hivi karibuni, Mungu atatosha watu wote wabaya na magumu yote yenye iko mu dunia. Tunaweza kuwa hakika kama ile itatimia. Juu ya nini? Juu Neno ya Mungu, Biblia, ilishaahidi hivi:

“Ulimwengu (ao dunia) unapita.”​—1 YOHANA 2:17.

Tunaweza kuwa hakika kama kutakuwa watu fulani wenye wataokoka juu hii andiko ya Biblia ilishaahidi hivi:

“Ule mwenye anafanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”

Kwa hiyo, siri ya kuokoka ni kufanya mapenzi ya Mungu. Ili tufikie kujua mapenzi ya Mungu, tunapaswa kwanza kumujua Mungu muzuri.

JUU UOKOKE UNAPASWA ‘KUFIKIA KUMUJUAʼ MUNGU

Collage: 1. Munganga moja anaikala chini mu hopitali, alishachoka na analemewa. 2. Anapumuzika kidogo mu restaurant na anaona mufanyakazi mwenzake iko anasoma kwa furaha gazeti fulani. 3. Ule mufanyakazi mwenzake anamusomea andiko moja ya Biblia na anamupatia karte ya jw.org.

Yesu alisema: “Uzima wa milele ndio huu, wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli.” (Yohana 17:3) Juu tuokoke na kuishi milele, tunapaswa ‘kufikia kumujua’ Mungu. Ile haimaanishe tu kukubali kama Mungu iko na kujua mambo fulani juu yake. Tunapaswa kuwa marafiki wake. Iko tu sawa vile tunapenda urafiki wetu na mutu fulani ukuwe nguvu, tunapaswa kupitisha wakati pamoja naye. Ni vile pia juu ya kuwa rafiki ya Mungu. Ona kweli fulani za maana zenye ziko mu Biblia, zenye zitakusaidia kukomalisha urafiki wako pamoja na Mungu na kuendelea kuwa rafiki yake.

Kweli Zenye Tunajifunza mu Biblia

Ule munganga iko ku nyumba na iko anaangalia site ya jw.org.

Tunajifunza kama Mungu alikuwa anapenda tuishi mu Paradiso.

Aliumba wanadamu wa kwanza, ni kusema, Adamu na Eva na aliwaweka fasi ya muzuri yenye iliitwa bustani ya Edeni. Walikuwa wakamilifu na Mungu aliwapatia kila kitu walikuwa nayo lazima ili wafurahie maisha. Maisha yao haingekuwa na mwisho. Kama wangeendelea kuwa marafiki wa Mungu hawangekufa hata kidogo. Lakini, walichagua kutotii amri yenye haikukuwa nguvu kutii yenye Mungu aliwapatia.

Tunajifunza juu ya nini tuko tunateseka.

Juu ya kukosa kutii, mwanadamu wa kwanza, Adamu, alipoteza pendeleo ya kuishi milele yenye alikuwa nayo na hata wanadamu wote walipoteza ile pendeleo. Biblia inafasiria hivi: “Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote.” (Waroma 5:12) Sawa vile mutu anaweza kuriti ulemavu fulani wa wazazi wake, watoto wote wa Adamu waliriti zambi na kifo. Njo maana tunazeekaka na kufa.

Tunajifunza mambo yenye tayari Mungu alishafanya ili kutusaidia.

Biblia inasema: “Mungu alipenda ulimwengu sana na hivyo akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.” (Yohana 3:16) Mungu alimutuma Yesu ku dunia ili kutoa uzima wake kwa ajili yetu. Juu ya ile tendo ya upendo, Prabhakar, mwanaume Muhindi mwenye kuwa na miaka 86 anasema hivi: “Ile inaonyesha kabisa upendo wenye Yehovaa iko nayo kwangu. Upendo wake unanipatia tumaini ya kuishi milele.”

Tunajifunza namna tunaweza kuonyesha shukrani juu ya mambo yote yenye Yehova alishatufanyia.

Biblia inasema kama tunaweza kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye Yehova alishatufanyia kwa “kushika amri zake.” (1 Yohana 2:3) Kwa upendo, Yehova Mungu anatuonyesha mambo yenye tunaweza kufanya juu tukuwe na maisha yenye furaha leo. (Isaya 48:17, 18, maelezo ya chini) Mungu hapendake wakati tunateseka. Anatuahidi kama, ikiwa tunafuata maagizo yake, tutakuwa na maisha ya muzuri sasa lakini pia tutakuwa na pendeleo ya kuishi milele.

USOME NENO YA MUNGU, BIBLIA, KILA SIKU

Kisha kusoma Biblia, ule munganga anaangalia juu, wakati wa kutumia chakula kidogo inje ya hopitali.

Wakati unamuomba Mungu akusaidie na wakati unafanya mapenzi yake unaweza kuokoka wakati dunia itaharibiwa

Tunakulaka chakula kila siku juu tuishi. Lakini Yesu alisema: “Mwanadamu hapaswe kuishi kwa mukate tu, lakini kwa kila neno lenye linatoka katika kinywa cha Yehova.”​—Matayo 4:4.

Leo, tunapata Neno ya Yehova mu Biblia. Wakati unajifunza ile kitabu takatifu, utajua kweli za musingi juu ya mambo yenye Mungu alifanyaka zamani, mambo yenye iko anafanya sasa, na juu ya mambo yenye atafanya wakati wenye kuja.

UMUOMBE MUNGU AKUSAIDIE

Unaweza kufanya nini kama unapenda kutii maagizo ya Mungu lakini ni nguvu kwako kuacha kufanya mambo yenye haimufurahishe? Mu ile hali, kufikia kumujua Mungu kunaweza kukusaidia umutii.

Fikiria mwanamuke mwenye tutaita Sakura, mwenye alikuwa na mwenendo mubaya sana. Wakati alianza kujifunza Biblia, alifikia kujua amri ya Mungu yenye inasema “mukimbie uasherati.” (1 Wakorinto 6:18) Sakura alimuomba Mungu amupatie nguvu na alifikia kuacha ile tabia ya mubaya. Lakini iko anafanya yake yote juu asiangukie mu ile mutego. Anasema: “Wakati mawazo ya uasherati inakuya mu akili yangu, nasali waziwazi kwa Yehova, nikijua kama siwezi kupiganisha ile hali miye peke. Sala imenisaidia nimukaribie Yehova zaidi.” Sawa vile Sakura, mamilioni ya watu wamefikia kumujua Mungu. Iko anawapatia nguvu yenye wako nayo lazima ili kufanya mabadiliko mu maisha na kuishi mu njia yenye inamufurahisha.​—Wafilipi 4:13.

Kadiri unafikia kumujua Mungu muzuri, ni vile ‘Mungu atakujua’ sawa rafiki wake wa sana. (Wagalatia 4:9; Zaburi 25:14) Njo utaishi milele mu dunia mupya. Lakini ile dunia mupya itakuwa namna gani? Habari yenye kufuata itafasiria ile jambo.

a Yehova njo jina ya Mungu sawa vile inaonyeshwa mu Biblia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine