Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp22 na. 1 uku. 12-13
  • 4 | Ukubali Musaada wa Mungu Juu ya Kuachana na Chuki

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 4 | Ukubali Musaada wa Mungu Juu ya Kuachana na Chuki
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Fundisho ya Biblia:
  • Ile Iko na Maana Gani?
  • Mambo Yenye Unaweza Kufanya:
  • Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Namna ya Kuachana na Chuki
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Tunaweza Kuachana na Chuki!
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Juu ya Nini Chuki Iko Naendelea?
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
wp22 na. 1 uku. 12-13
Watu wako naenda kwenye Biblia yenye kuwaangazia. Kivuli inaonyesha kama walikuwa na chuki zamani.

NAMNA YA KUACHANA NA CHUKI

4 | Ukubali Musaada Wa Mungu Juu Ya Kuachana Na Chuki

Fundisho ya Biblia:

“Tunda la roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, fazili, wema, imani, upole, kujizuia.”​—WAGALATIA 5:22, 23.

Ile Iko na Maana Gani?

Mungu tu njo anaweza kutusaidia tupiganishe chuki. Roho yake takatifu inaweza kutusaidia tukomalishe sifa zenye pengine hatungeweza kukomalisha siye peke. Kuliko kujaribu kumaliza chuki siye wenyewe, ni muzuri tutumainie nguvu ya Mungu. Tukifanya vile, tutajionea kama Paulo alisema kweli wakati aliandika hivi: “Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.” (Wafilipi 4:13) Na bila shaka, tutaweza kusema: “Musaada wangu unatoka kwa Yehova.”​—Zaburi 121:2.

Mambo Yenye Unaweza Kufanya:

“Yehova amenibadilisha kabisa. Nilikuwa mutu wa jeuri, lakini sasa niko mutu mwenye kuishi kwa amani na wengine.”​—WALDO

Usali kwa Yehova kwa moyo wote. Umuombe akupatie roho yake takatifu. (Luka 11:13) Umuombe akusaidie ukomalishe sifa za muzuri mu maisha yako. Ujifunze mambo yenye Biblia inasema juu ya sifa zenye zinaweza kukusaidia upiganishe chuki. Sifa sawa vile upendo, amani, uvumilivu, na kujizuia. Fikiria namna unaweza kukomalisha zile sifa mu maisha yako. Na upitishe wakati pamoya na watu wenye wako najikaza kukomalisha zile sifa. Wale watu wanaweza ‘kukuchochea katika upendo na matendo ya muzuri.’​—Waebrania 10:24.

Habari ya Kweli​—WALDO

Aliachana na Chuki na Jeuri

Waldo.

Wakati alikuwa nakomala, Waldo alikuwa na maisha ya magumu sana. Ile ilifanya akuwe na chuki. Anasema hivi: “Nilikuwa na zoezi ya kupigana na watu wenye walikuwa nauzisha dawa za kulewesha . . . Siku moya, maadui wangu walilipa mutu fulani mwenye alijulikana kuwa anauaka watu sana, juu aniue. Niliponyoka, hata kama ule mutu aliniingiza kisu.”

Waldo hakufurahi wakati bibi yake alianza kujifunza Biblia pamoya na Mashahidi wa Yehova. Anasema hivi: “Nilichukia Mashahidi, na mara mingi nilikuwa nawatombokea na kuwatukana. Lakini kila mara walikuwa najibia kwa upole.”

Kisha wakati fulani, Waldo naye alianza kujifunza Biblia. Anasema hivi: “Ilikuwa nguvu kutumikisha mambo yenye nilikuwa najifunza. Nilikuwa hakika kabisa kama sitawezaka kuacha jeuri.” Lakini jambo fulani yenye alijifunza mu Biblia ilimusaidia abadilishe mawazo yake.

Waldo anasema hivi: “Siku moya, mwalimu wangu Alejandro aliniambia nisome Wagalatia 5:22, 23. . . . Alejandro aliniambia kama singeweza kukomalisha zile sifa kwa nguvu yangu mwenyewe. Iliomba nitegemee roho ya Mungu. Ile ilinisaidia kujua kama na miye ningeweza kubadilika!”

Juu alitegemea musaada wa Mungu, Waldo alifikia kuachana kabisa na chuki mu maisha yake. Anasema hivi: “Watu wa familia yangu na marafiki wangu wanashangala sana kuona namna nimebadilika.” Anasema tena hivi: “Yehova amenibadilisha kabisa. Nilikuwa mutu wa jeuri, lakini sasa niko mutu mwenye kuishi kwa amani na wengine.”

Ukipenda kujua mambo mingi juu ya Waldo, soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 10, 2013, ukurasa wa 12-13.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine