Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w22 Mwezi wa 12 uku. 15
  • Unakumbuka?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unakumbuka?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Musijiingize Katika Kazi Hiyo”
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Acha Yehova Akutumikishe
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Usiache Waamini Wenzako Hata Kidogo
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Uko na Miradi Gani kwa Ajili ya Mwaka Mupya wa Utumishi?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
w22 Mwezi wa 12 uku. 15

Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu magazeti ya Munara wa Mulinzi ya hii mwaka? Kama ni vile, pima kujibia hii maulizo:

Tutapata faida gani kama tunachukua wakati ya kuzungumuza, kusikiliza, na kufikiri juu ya Yehova?

Tutakamata maamuzi ya muzuri zaidi, tutakuwa walimu wazuri zaidi, imani yetu itakuwa nguvu zaidi, na tutamupenda Yehova zaidi.​—w22.01, uku. 30-31.

Tutapata faida gani kama tunajifunza kumutumainia Yehova na wale wenye wanamuwakilisha?

Hii njo wakati ya kujifunza kutumainia namna ya Mungu ya kufanya mambo kwa kuepuka kuwa na mashaka kuhusu muongozo na maamuzi ya wazee. Wakati taabu kubwa itaanza, tutakuwa tayari kutii hata kama tunapewa maagizo yenye inaonekana kuwa nguvu kuelewa ao nguvu kutumikisha.​—w22.02, uku. 4-6.

Malaika alimaanisha nini wakati alimuambia Zekaria kuhusu “kamba ya kupima usawa katika mukono wa [Gavana] Zerubabeli”? (Zek. 4:8-10)

Ile maono ilihakikishia watu wa Mungu kuwa hata kama hekalu ya mupya ilionekana kuwa tofauti na ile ya zamani yenye utukufu, ingemalizika na ingekuwa vile Yehova alipenda ikuwe.​—w22.03, uku. 16-17.

Namna gani tunaweza kuwa “mufano . . . katika kusema”? (1 Ti. 4:12)

Tunapaswa kusema kwa fazili na heshima mu mahubiri, kuimba kwa moyo wote, kutoa kwa ukawaida maelezo ku mikutano, kusema kweli, kujenga wengine, na kuepuka matukano.​—w22.04, uku. 6-9.

Juu ya nini sehemu za wanyama (falme) ine wenye kuzungumuziwa mu Danieli sura ya 7 zinafanana na sehemu za munyama moya mwenye kuzungumuziwa mu Ufunuo 13:1, 2?

Munyama wa pori mwenye kuzungumuziwa mu Ufunuo 13 hafananishe tu ufalme moya, sawa vile Roma. Lakini, anafananisha serikali zote kubwa zenye zimetawala wanadamu.​—w22.05, uku. 9.

Namna gani tunaonyesha kama tunatumainia haki ya Yehova?

Kama mutu anatutukana, anatukasirisha, ao anatukosea, tunajikaza kuacha kumukasirikia na kumuwekea kinyongo. Kwa kufanya vile, tunaacha mambo mu mikono ya Yehova. Atatosha mambo yote ya mubaya yenye inatokana na zambi.​—w22.06, uku. 10-11.

Ndugu mwenye iko natoa sala ku mukutano hapaswe kusahau nini?

Sala haipaswe kutumiwa juu ya kushauria kutaniko, ao kufanya matangazo. Haiko lazima kutumia “maneno mingi,” zaidi sana ku mwanzo wa mukutano. (Mt. 6:7)​—w22.07, uku. 24-25.

Ni mu maana gani “wale wenye walizoea kutenda mambo maovu” watapata “ufufuo wa hukumu”? (Yoh. 5:29)

Hawatapewa azabu ao malipizi juu ya matendo yao ya zamani. Yesu atakuwa nawachunguza ili kuona namna wako najiendesha kisha ufufuo wao.​—w22.09, uku. 18.

Ni maneno gani yenye kuchochea yenye Ndugu Rutherford alisemaka ku mukusanyiko wenye ulifanywa Mwezi wa 9, 1922?

Ku mukusanyiko moya wenye ulifanywa Cedar Point, Ohio, Amerika, alisema hivi: “Mufalme anatawala! Muko na mugao wa kuambia kila mutu kuhusu ile jambo. Kwa hiyo, mutangaze, mutangaze, mutangaze, Mufalme na Ufalme wake!”​—w22.10, uku. 3-5.

Isaya sura ya 30 inaonyesha mambo gani tatu yenye Mungu anafanyaka ili kutusaidia tuvumilie magumu?

Hii sura inaonyesha kama Mungu (1) anasikiliza na kujibia sala zetu, (2) anatuongoza, na (3) anatubariki sasa na atatubariki wakati yenye kuya.​—w22.11, uku. 9.

Juu ya nini tunaweza kusema kama maneno ya Zaburi 37:10, 11, 29 ilitimia zamani na itatimia wakati yenye kuya?

Maneno ya Daudi ilionyesha kama mu Israeli watu wa Mungu waliishi kwa amani na walikuwa na maisha ya muzuri, sawa vile mu utawala wa Sulemani. Yesu alikuwa nazungumuzia Paradiso ya wakati yenye kuya na alitaya maneno yenye kuwa mu mustari wa 11. (Mt. 5:5; Lu. 23:43)​—w22.12, uku. 8-10, 14.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine