Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp23 na. 1 uku. 14-15
  • Namna ya Kusaidia Wale Wenye Wako na Matatizo ya Akili

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kusaidia Wale Wenye Wako na Matatizo ya Akili
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ile Iko na Maana Gani?
  • Namna ile Inaweza Kusaidia
  • Musaada Wako Unaweza Kuwa wa Maana
  • Mungu Anataka Uwe Rafiki Yake
    Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Rafiki Muzuri Ni Nani?
    Amuka!—2014
  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Unawaza Namna Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
wp23 na. 1 uku. 14-15
Mwanaume iko nasikiliza kwa huruma bibi yake mwenye kuwa na mahangaiko.

Namna ya Kusaidia Wale Wenye Wako na Matatizo ya Akili

BIBLIA INASEMA HIVI: “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.” —MEZALI 17:17.

Ile Iko na Maana Gani?

Ni mwepesi kujisikia kuwa tunaishiwa wakati rafiki yetu iko nateseka juu ya mahangaiko ya akili. Lakini tunaweza kuonyesha kama tunamuhangaikia kwa kumusaidia apiganishe ile tatizo ya akili yenye iko namuhangaisha. Namna gani?

Namna ile Inaweza Kusaidia

‘Ukuwe mwepesi wa kusikiliza.’ —YAKOBO 1:19.

Jambo moya ya muzuri yenye unaweza kufanya juu ya kusaidia rafiki yako ni kumusikiliza wakati anapenda kuzungumuza. Usiwaze kama unalazimika kujibia ku kila jambo yenye anasema. Onyesha kama uko namusikiliza na uendelee kujitia pa nafasi yake. Ujikaze kumuelewa muzuri na uepuke kumuhukumu. Ukumbuke kama anaweza kusema mambo yenye hakupenda kusema na yenye anaweza kuhuzunikia kisha.—Yobu 6:2, 3.

“Museme kwa namna yenye kufariji.” —1 WATESALONIKE 5:14.

Rafiki yako anaweza kuwa na wasiwasi ao anaweza kujiona kuwa wa bure. Hata kama haujue useme nini juu ya kumufariji, kama tu unaonyesha kuwa unamuhangaikia, ile inaweza kumufariji na kumutia moyo.

“Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote.”​—MEZALI 17:17.

Umutolee musaada wenye kufaa. Kuliko kuwaza tu kama unajua namna ya kumusaidia, umuulize mambo yenye unaweza kumufanyia. Kama rafiki yako anashindwa kukuambia mambo yenye iko nayo lazima, upime kumuuliza kama munaweza kufanya jambo fulani pamoya, sawa vile kuenda kutembea. Ao unaweza kumusaidia kuenda kuuza vitu, kufanya usafi, ao kazi ingine.—Wagalatia 6:2.

“Mukuwe wavumilivu.” —1 WATESALONIKE 5:14.

Haiko kila wakati njo rafiki yako anaweza kuwa tayari kusema. Umuhakikishie kama utapenda kumusikiliza wakati atapenda kusema. Rafiki yako anaweza kufanya ao kusema jambo fulani yenye inakuhuzunisha. Pengine anaweza kubadilisha mipango yenye mulikuwa nayo, ao anaweza kubadilika tu na kuwa sawa mutu mwenye kukasirika. Ukuwe muvumilivu na ujikaze kumuelewa wakati uko namutolea musaada wenye iko nao lazima.—Mezali 18:24.

Musaada Wako Unaweza Kuwa wa Maana

“Najikazaka kuwa rafiki mwenye anaweza kutumainia. Hata kama siwezi kumaliza matatizo yake, najikazaka sana kumusikiliza wakati iko nasema. Wakati fulani anakuwaka na lazima tu ya mutu wa kumusikiliza juu ajisikie muzuri.”—Farrah,a mwenye rafiki yake iko na mahangaiko ya mingi, ugonjwa wa akili wenye unafanyaka ashindwe kula kwa kiasi yenye kufaa na ugonjwa wa kushuka moyo sana.

Mwanamuke anagusa mukono wa mwanamuke mwingine mwenye kuwa na umri mukubwa zaidi.

“Rafiki yangu moya anakuwaka mwenye fazili na anakuwaka nanitia moyo. Aliniitaka kwake juu tukule chakula ya butamu. Alinionyesha upendo na alikuwa muchangamufu. Ile ilinisaidia niseme namna nilikuwa najisikia. Ilinitia moyo kabisa!”—Ha-eun, mwenye iko na ugonjwa wa kushuka moyo sana.

“Uvumilivu ni wa maana sana. Wakati bibi yangu anafanya jambo fulani yenye hainifurahishe, nakuwaka najikumbusha kama ugonjwa wake njo unafanya atende vile, haiko vile njo anakuwaka. Ile inanisaidiaka niepuke kukasirika na nimuhangaikie zaidi.”—Jacob, mwenye bibi yake iko na tatizo ya kushuka moyo sana.

“Bibi yangu amenitegemeza sana na anakuwaka nanifariji. Wakati niko na mahangaiko ya mingi, hanikazake kufanya jambo yenye sipendi kufanya. Na wakati fulani ile inaombaka akose kufanya mambo yenye angependa kufanya. Roho yake ya kujinyima na ukarimu wake ni mambo yenye inafanyaka akuwe wa maana sana kwangu.”—Enrico, mwenye iko na tatizo ya akili yenye inafanyaka akuwe na wasiwasi sana.

a Majina fulani imebadilishwa.

Juu ya Kupata Musaada Ingine:

Soma ku jw.org habari “Wakati Mutu Fulani Mwenye Unapenda Anagonjwa,” mu gazeti Amuka! ya Mwezi wa 10, 2015.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine