NAMNA YA KUJIFUNZA
Zungumuza na Bengine Juu ya Mambo Yenye Umejifunza
Kujifunza kunaweza kufurahisha. Lakini tunaweza kufurahi tena zaidi kama tunaambia bengine mambo yenye tulijifunza yenye inatusaidia tumukaribie Yehova zaidi. Mezali 11:25 inasema hivi: “Ule mwenye kuburudisha wengine yeye mwenyewe ataburudishwa.”
Kuzungumuza na bengine juu ya mambo yenye tulijifunza, kunatusaidia tukumbuke mambo yenye tulijifunza na tuielewe muzuri zaidi. Na juu ile mambo inaweza kusaidia bengine, tunakuwa na furaha wakati tunazungumuzia ile mambo pamoya nabo.—Mdo. 20:35.
Pima kufanya hivi: Mu juma yenye iko nakuya utafute nafasi ya kuambia mutu mwingine mambo yenye ulijifunza. Unaweza kuambia mutu wa mu familia, wa mu kutaniko yenu, mufanyakazi mwenzako, mwanafunzi mwenzako, jirani yako ao mutu mwenye unakutana naye mu mahubiri. Jaribu kuzungumuzia ile mambo kwa kutumia maneno yako mwenyewe, mu njia ya mwepesi na yenye kuwa wazi.
Kumbuka: Ambia bengine mambo yenye unajifunza juu ya kubatia moyo hapana juu ya kujionyesha.—1 Ko. 8:1.