Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 36
  • Yesu Alizaliwa Wakati Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Alizaliwa Wakati Gani?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu la Biblia
  • Sababu gani Noeli inafanywa tarehe 25 Mwezi wa 12?
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Noeli?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Sababu gani watu wengine hawafanye sikukuu ya Noeli?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yesu
    Amuka!—2013
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 36

Yesu Alizaliwa Wakati Gani?

Jibu la Biblia

Biblia haitoe tarehe ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo, kama inavyoonyeshwa katika vitabu vinavyofuata:

  • “Tarehe ya kweli ya kuzaliwa kwa Kristo haijulikane.”—New Catholic Encyclopedia.

  • “Tarehe kamili ya kuzaliwa kwa Kristo haijulikane.”—Encyclopedia of Early Christianity.

Biblia haionyeshe tarehe ya kuzaliwa kwa Yesu. Lakini inazungumuzia mambo mawili yaliyotokea yanayohusiana na kuzaliwa kwake na yanayowafanya wengi wafikie kutambua kwamba hakuzaliwa tarehe 25 Mwezi wa 12.

Hakuzaliwa wakati wa kipindi cha baridi kali

  1. Kuandikishwa kwa watu. Muda mufupi tu mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Kaisari Agusto aliamuru “dunia yote inayokaliwa iandikishwe.” Kwa kuwa kila mutu alipaswa kujiandikisha katika “jiji lake mwenyewe,” wazazi wa Yesu walipaswa kufanya safari ya juma moja ao zaidi ili wajiandikishe. (Luka 2:1-3) Amri hiyo ambayo pengine ilitolewa ili isaidie kulipisha kodi na kuandikisha watu katika jeshi, haingekubaliwa na wengi wa wakati huo, lakini inaonekana kwamba Agusto hangewasumbua watu zaidi kwa kuwalazimisha kufanya safari ndefu wakati huo wa majira ya baridi kali.

  2. Kondoo. Wachungaji walikuwa ‘wakiishi inje, wakichunga makundi yao usiku.’ (Luka 2:8) Kitabu kimoja kinasema kwamba makundi ya kondoo yalikuwa inje “juma moja mbele ya Pasaka [mwishoni mwa Mwezi wa 3]” mupaka katikati ya Mwezi wa 11. (Daily Life in the Time of Jesus). Kisha kitabu hicho kinaongezea hivi: “Walikuwa ndani ya nyumba katika kipindi hicho cha baridi kali, na jambo hilo pekee linaonyesha kwamba tarehe ya Noeli, katika majira ya baridi kali, ni ya uongo kwa sababu Injili inasema kwamba walikuwa mashambani.”

Alizaliwa katika majira ya kuanguka kwa majani

Tunaweza kukadiria wakati ambapo Yesu alizaliwa kwa kuhesabu tukirudi nyuma kuanzia wakati wa kifo chake wakati wa Pasaka ya Nisani 14 katika majira ya kuchipua ya mwaka wa 33. (Yohana 19:14-16) Yesu alikuwa na miaka karibu 30 alipoanza kazi yake ya miaka tatu na nusu, hilo linaonyesha kwamba alizaliwa mwanzoni mwa majira ya kuanguka kwa majani (printemps) ya Mwezi wa 10, mwaka wa 2.—Luka 3:23.

Sababu gani Noeli inafanywa tarehe 25 Mwezi wa 12?

Kwa kuwa hakuna jambo linaloonyesha kwamba Yesu Kristo alizaliwa tarehe 25 Mwezi wa 12, sababu gani Noeli inafanywa siku hiyo? Kitabu kimoja kinasema kwamba inaonekana kwamba viongozi wa kanisa walichagua tarehe hiyo “ili ipatane na sikukuu ya kipagani ya Waroma ya ‘kuzaliwa kwa jua lisiloshindwa,’”wakati wa majira ya baridi kali (hiver). (Encyclopædia Britannica). Kitabu kingine kinasema kwamba watu wengi wenye elimu wanaamini kwamba tarehe hiyo ilichaguliwa “ili kufanya Ukristo uwe wa maana zaidi kwa wapagani waliogeuza imani yao.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine