MUSAADA KWA FAMILIA | KULEA WATOTO
Namna ya Kushugulika na Milipuko ya Hasira ya Mutoto Wako
TATIZO
Wakati anakasirika, mutoto wako aliye na miaka miwili anapiga kelele, anapiga-piga miguu chini, na anajigeuza-geuza chini. Unajiuliza: ‘Mutoto wangu ana akili sawa? Analipuka kwa hasira kwa sababu ninafanya jambo fulani mbaya? Ataacha tabia hiyo wakati atakomaa?’
Unaweza kumusaidia mutoto wako aliye na miaka miwili kubadilisha tabia yake. Kwanza, chunguza jambo ambalo linamufanya awe na tabia hiyo.a
SABABU GANI JAMBO HILO LINATOKEA?
Watoto hawana uwezo mwingi wa kujua namna ya kuzuia hasira yao. Jambo hilo peke yake linaweza kuwafanya walipuke kwa hasira mara kwa mara. Lakini kuna mambo mengine zaidi.
Wazia namna mutoto anavyobadilika wakati anapokaribia kueneza miaka miwili. Tangu wakati alizaliwa, wazazi wake walikuwa wanamufanyia kila kitu ambacho alihitaji. Kwa mufano, ikiwa analia, wazazi walikuwa wanakuja haraka na kujiuliza: ‘Mutoto anagonjwa? Anahitaji chakula? kubembelezwa? kubadilishwa nguo?’ Wazazi walifanya yote yaliyohitajiwa ili kufanya mutoto ajisikie vizuri. Na hilo lilikuwa jambo lenye kufaa kwa sababu mutoto alitegemea kabisa wazazi wake.
Hata hivyo, anapokaribia kueneza miaka miwili, mutoto anaanza kutambua kwamba wazazi wake hawamufanyie tena kila kitu ambacho anataka. Kwa kweli, kuliko kumufanyia mambo ambayo anahitaji, wazazi wanamutazamia yeye akubaliane pia na mambo ambayo wao wanataka. Sasa mambo yamebadilika, na labda mutoto aliye na miaka miwili hatakubaliana na jambo hilo bila kupinga—labda atafanya hivyo kupitia milipuko ya hasira.
Baada ya muda, kwa kawaida mutoto anajirekebisha anapoelewa kwamba wazazi wake ni walimu wake, na si watunzaji wake tu. Jambo la kupendeza ni kwamba mutoto anaelewa pia kuwa ana daraka la ‘kuwatii wazazi wake.’ (Wakolosai 3:20) Wakati huohuo, mutoto anaweza kujaribu mupaka mwisho uvumilivu wa wazazi wake kwa kulipuka kwa hasira mara kwa mara.
MAMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA
Umuelewe mutoto wako. Mutoto wako si mutu muzima. Kwa sababu hana uwezo wa kuzuia hasira yake, anaweza kulipuka kwa hasira wakati anakasirika. Jaribu kuona hali hiyo kama mutoto anavyoiona.—Kanuni ya Biblia: 1 Wakorintho 13:11.
Uwe mutulivu. Mutoto wako anapokuwa na milipuko ya hasira, hautamusaidia mutoto wako ikiwa wewe pia unakasirika. Kwa kadiri inavyowezekana, usijali milipuko yake ya hasira na usikasirike. Ukijua sababu gani mutoto wako analipuka kwa hasira, hilo litakusaidia uendelee kuwa mutulivu.—Kanuni ya Biblia: Methali 19:11.
Usikubali kila kitu mutoto wako anataka. Ukikubali kila kitu ambacho mutoto wako anaomba, inaelekea atalipuka tena kwa hasira wakati mwengine ikiwa anataka kitu fulani. Tenda kwa utulivu kwa njia ambayo itamuonyesha mutoto wako kwamba hautabadilisha hata kidogo uamuzi wako.—Kanuni ya Biblia: Mathayo 5:37.
Uwe muvumilivu. Usitazamie kwamba milipuko ya hasira ya mutoto wako itaisha mara moja, zaidi sana ikiwa umemuonyesha kwamba unaweza kufanya jambo lolote analoomba wakati anakukaza kufanya hivyo. Hata hivyo, ukitenda vizuri na bila kubadilika-badilika, milipuko ya hasira ya mutoto wako inaweza kupunguka. Mwishowe, milipuko hiyo ya hasira itaisha tu. Biblia inasema hivi: “Upendo ni wenye ustahimilivu,” ni kusema, unavumilia mambo yote.—1 Wakorintho 13:4.
Pia, jaribu kufanya hivi:
Wakati mutoto wako anaanza kulipuka kwa hasira, umukumbatie katika mikono yako (ikiwezekana) na, bila kumuumiza, umukataze kujigeuza-geuza chini. Usimufokee mutoto wako. Ngojea tu hasira yake kali iishe. Mwishowe, mutoto atatambua kwamba milipuko yake ya hasira haikumuletea faida yoyote.
Chagua mahali fulani ambapo unaweza kumuweka mutoto wako kila mara anapokuwa na milipuko ya hasira. Umuambie kwamba atatoka hapo wakati tu anatulia, na kisha umuache hapo.
Ikiwa mutoto wako analipuka kwa hasira mbele ya watu, umuondoe mbele ya watu wengine. Usimuachilie kwa sababu tu anafanya mambo ya kushangaza mbele ya watu. Ikiwa unamuachilia mutoto wako, ataona kwamba kwa kulipuka kwa hasira anaweza kupata jambo lolote ambalo anataka.
a Ijapokuwa katika habari hii tunazungumuza juu ya mutoto mwanaume, kanuni zinazozungumuziwa zinahusu pia mutoto mwanamuke.
Ukijua sababu gani mutoto wako analipuka kwa hasira, hilo litakusaidia uendelee kuwa mutulivu