Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 5/15 uku. 8-9
  • Kufundisha Watoto Kutii

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kufundisha Watoto Kutii
  • Amuka!—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TATIZO
  • Malipizi Yenye Kuleta Matokeo Mazuri
    Amuka!—2015
  • Namna ya Kushugulika na Milipuko ya Hasira ya Mutoto Wako
    Amuka!—2013
  • Namna ya Kukataa Ombi la Mutoto
    Amuka!—2014
  • Namna ya Kufundisha Watoto Wako Adabu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Amuka!—2015
g 5/15 uku. 8-9
Mutoto mudogo mwanaume anakataa kutii mama yake

MUSAADA KWA FAMILIA | KULEA WATOTO

Kufundisha Watoto Kutii

TATIZO

Kila mara wewe na mutoto wako wa miaka ine munapigania uongozi, na kila mara inaonekana ni mutoto wako ndiye anapata ushindi.

  • Wakati unamuambia afanye jambo lenye hapendi kufanya, anakataa na anaonyesha kuwa hataki kukutii.

  • Wakati unamuambia asifanye jambo lenye anapenda kufanya, analia kwa hasira.

Unajiuliza hivi: ‘Hiyo tu ni tabia ya watoto wa miaka yake? Ninaweza kutumainia kuwa ataiacha?’

Unaweza kufundisha mutoto wako kutii. Lakini mbele tuzungumuzie namna unaweza kufanya hivyo, tuone kwanza sababu moja yenye pengine inafanya akose kutii.

SABABU GANI ANAKOSA KUTII?

Wakati mutoto wako alikuwa mudogo sana, kazi yako kubwa ilikuwa kumuchunga. Ulikuwa tayari kumuhangaikia kila wakati alikuwa na lazima yako. Wakati alikuwa tu analia, ulikuwa unakuja haraka na kumufanyia mambo yenye iko nayo lazima. Bila shaka, ilikuwa vizuri kufanya hivyo na ilikuwa jambo la lazima. Mutoto mudogo sana iko na lazima ya kuhangaikiwa na wazazi kila mara.

Kisha kumuhangaikia hivyo kwa miezi mingi, ni jambo la kawaida mutoto atende kwa njia yenye kuonyesha kuwa yeye ndiye mwenye mamlaka katika nyumba, na wazazi wake ni watumishi wa kumufanyia kila kitu anataka. Mara nyingi wakati mutoto anafikia miaka mbili hivi, anatambua kuwa “mamlaka” yenye alikuwa nayo imeisha. Wazazi wake hawafuate tena muongozo wake; wanataka yeye afuate muongozo wao. Jambo hilo linasumbua sana watoto. Kwa hiyo, watoto fulani wanalia kwa hasira. Wengine wanakataa kutii ili kujaribu mamlaka ya wazazi wao.

Wakati huo mugumu muzazi anakuwa na kazi ingine ya kufanya, ni kusema, anapaswa kuonyesha kuwa iko na mamlaka na kutoa muongozo wenye kuwa wazi juu ya mambo mutoto anapaswa kufanya. Muzazi atafanya nini ikiwa mutoto anaonyesha kuwa hataki kumutii na anakosa kufuata muongozo wenye amepewa, kama vile mufano wenye kuwa mwanzoni mwa habari hii unaonyesha?

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Chukua uongozi. Mutoto wako hatakubali kama ni wewe unaongoza ikiwa hakuone unachukua uongozi. Kwa hiyo, unapaswa kuonyesha mamlaka yako, lakini utafanya hivyo bila kupitisha mipaka. Katika miaka fulani yenye imepita, watu fulani wenye elimu wamefanya neno “mamlaka” lionekane mubaya. Mumoja wao anasema kama ni kosa kubwa wazazi kutumia mamlaka juu ya watoto, na haifae kufanya hivyo. Lakini, kuachilia watoto kunaweza kufanya wakose muongozo wa kufuata, waone kuwa wanaweza kufanya kila kitu wanataka, na wajione kuwa na mamlaka yote. Kufanya hivyo hakuwatayarishe kuwa watu wazima wenye kutegemeka.—Kanuni ya Biblia: Methali 29:15.

Patia mutoto malipizi. Kamusi moja inasema kama malipizi ni “mazoezi yenye inafanya mutu akuwe mutiifu ao mwenye kujizuia; inatolewa mara nyingi wakati mutu anavunja sheria fulani yenye amepewa.” Bila shaka, malipizi haipaswe kupitisha mipaka. Lakini, inapaswa kuwa wazi, yenye kuwa na matokeo, na inapaswa kuchochea mutoto abadilike.—Kanuni ya Biblia: Methali 23:13.

Ukuwe wazi. Wazazi fulani wanaomba watoto wao wawatii. (“Ningependa usafishe chumba chako—sawa?”) Pengine wanaona kuwa kufanya hivyo ni kuonyesha adabu. Lakini hilo linaweza kufanya muzazi akuwe mwenye kutii mutoto wake. Pia litafanya mutoto ajipatie uhuru wa kuchunguza mambo yenye anafurahia na yenye hafurahie kuhusu jambo lenye ameombwa kufanya, na kisha anaamua ikiwa atatii ao hapana. Kuliko kuachilia mamlaka yako, toa muongozo wenye kuwa wazi; uutoe kama sheria.—Kanuni ya Biblia: 1 Wakorintho 14:9.

Usibadilike-badilike. Ukisema hapana, usibadilike, na uhakikishe kama wewe na bibi ao bwana yako munapatana juu ya jambo hilo. Ikiwa umeamua kumupatia mutoto malipizi sababu ya kukosa kutii, usibadilike. Usikubali mutoto wako akubembeleze, ao usiendelee kubishana naye juu ya sababu yenye ilifanya uchukue uamuzi huo. Itakuwa vyepesi zaidi kwako na kwa mutoto wako ikiwa ‘unaacha Ndiyo yako imaanishe Ndiyo, na Siyo yako, Siyo.’—Yakobo 5:12.

Ukuwe mwenye upendo. Katika familia, haiko kila mutu iko na uhuru wa kuongoza ao kulazimisha wengine wafuate uongozi wake. Lakini familia ni mupango wa Mungu. Kupitia mupango huo watoto wanaweza kuongozwa kwa upendo ili wakuwe watu wazima wenye hekima. Ni kweli kwamba malipizi inaweza kumusaidia mutoto wako ajifunze kutii na pia ajisikie mwenye kupendwa.

MAANDIKO YA LAZIMA

  • ‘Muvulana [mutoto] aliyeachiliwa atamuletea mama yake aibu [haya].’—Methali 29:15.

  • ‘Usimunyime muvulana nizamu [malipizi].’—Methali 23:13.

  • ‘Musiposema maneno yenye kueleweka kwa urahisi, . . . watu watajuaje linalosemwa?’—1 Wakorintho 14:9.

Ili Kupata Habari Zaidi

Ili kupata habari zaidi juu ya namna kanuni za Biblia zinaweza kusaidia wazazi, fungua adresi yetu ya Internete jw.org. Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA >WENZI WA NDOA NA WAZAZI. Hapo utapata habari kama vile:

  • “Kuwapatia Watoto Malipizi”

  • “Jinsi ya Kushughulika na Mtoto Mwenye Milipuko ya Hasira”

  • “Jinsi ya Kusema Hapana”

  • “Uwafundishe Watoto Wako Tabia ya Muzuri”

  • “Mtoto Wako Anaposema Uwongo”

  • “Jinsi ya Kumtia Nidhamu Kijana Wako”

Soma pia habari kubwa ya gazeti Amuka! ya Mwezi wa 4, 2015, yenye kichwa “Ni Mubaya Kupatia Mutoto Malipizi?”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine