Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 7/13 uku. 14-15
  • Ufalme Wa Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ufalme Wa Mungu
  • Amuka!—2013
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ufalme wa Mungu ni hali iliyo ndani ya moyo wa mutu?
  • Ufalme wa Mungu ni nini?
  • Ufalme wa Mungu utakuja kupitia bidii ya wanadamu?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Ufalme wa Mungu Uko mu Moyo Wako?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Kweli Kuhusu Ufalme wa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2013
g 7/13 uku. 14-15

MAONI YA BIBLIA | Ufalme Wa Mungu

Ufalme Wa Mungu

Ufalme wa Mungu ni hali iliyo ndani ya moyo wa mutu?

‘Wewe hauko mbali na ufalme wa Mungu.’​—Marko 12:34.

MAMBO AMBAYO WATU WANASEMA Kama dini moja kubwa kati ya dini za uongo zinazojiita kuwa za Kikristo inavyofundisha, watu wengi wanaamini kwamba Ufalme wa Mungu ni “utawala wa Mungu katika moyo na maisha ya mutu.”

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA Ufalme wa Mungu ni serikali ya kweli, haufananishe hali ya mutu ya kujitiisha kwa Mungu katika moyo wake. Ufalme wa Mungu utatawala dunia yote.​—Zaburi 72:8; Danieli 7:14.

Kwa hiyo basi, Yesu alimaanisha nini aliposema “Ufalme wa Mungu ni ndani yenu”? (Sisi ndio tunatia italiki; Luka 17:21, La Sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo) Yesu hangemaanisha kwamba Ufalme wa Mungu ulikuwa katika mioyo ya wasikilizaji wake. Sababu gani? Kwa sababu watu ambao aliambia hivyo walikuwa Mafarisayo. Yesu alisema kwamba wangetengwa na Ufalme kwa sababu namna yao ya kuabudu Mungu ilikuwa ya kinafiki na kwa hiyo haikuwa yenye kukubaliwa na Mungu. (Mathayo 23:13) Hata hivyo, Yesu alikuwa na haki ya kusema Ufalme ni “ndani yenu” ao, “katikati yenu,” kulingana na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Sababu gani alikuwa na haki ya kusema hivyo? Kwa sababu yeye, akiwa Mufalme wa Ufalme huo, alikuwa anasimama mbele yao.​—Luka 17:21.

Ufalme wa Mungu ni nini?

“Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.”​—Mathayo 6:10.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA Ufalme ni serikali ya kweli ya Mungu ambayo inaongozwa na Yesu Kristo akiwa Mutawala. (Mathayo 28:18; 1 Timotheo 6:14, 15) Kusudi la Ufalme huo ni kutimiza mapenzi ya Mungu mbinguni na duniani. (Mathayo 6:10) Kwa hiyo, kupitia Ufalme wake, Mungu atamaliza magumu ya wanadamu. Ufalme utafanya mambo ambayo serikali za wanadamu haziwezi kutimiza.

Chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu, wanadamu watakuwa na amani, usalama, na mafanikio katika paradiso duniani. (Zaburi 46:9; Isaya 35:1; Mika 4:4) Hakuna mutu ambaye atagonjwa wala kufa, na magonjwa yataondolewa. (Isaya 33:24; Ufunuo 21:4) Na hata uzee hautakuwa tena. Biblia inatabiri hivi: “Nyama yake na iwe laini kuliko wakati wa ujana; na arudi kwenye siku za nguvu za ujana wake.”​—Ayubu 33:25.

MAMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA Hata iwe wewe ni mutu wa rangi gani ao ulizaliwa wapi, unaweza kuwa raia wa Ufalme wa Mungu ikiwa unafanya mambo ambayo Mungu anakuomba. Biblia inasema hivi: ‘Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mutu ambaye anamuogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.’​—Matendo 10:34, 35.

Ufalme wa Mungu utakuja kupitia bidii ya wanadamu?

“Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe.”​—Danieli 2:44.

MAMBO AMBAYO WATU WANASEMA Watu fulani wanaamini kwamba wanadamu watasimamisha Ufalme wa Mungu duniani, iwe kwa kufanya watu wengine wakubali imani yao ao kwa kutumika ili kuleta amani na undugu duniani pote.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA Mungu anasimamisha Ufalme wala si wanadamu. (Danieli 2:44) Wakati Ufalme ulianza kutawala, Mungu alisema: ‘Mimi, naam, mimi nimemweka mufalme wangu.’ (Zaburi 2:6) Ufalme wa Mungu hautaletwa na wanadamu, na hawawezi kuvuruga kazi za Ufalme huo, kwa sababu Ufalme huo utatawala duniani ukiwa mbinguni.​—Mathayo 4:17.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO? Ni jambo la kawaida kutumaini kwamba wanadamu wanaweza kuleta amani na umoja duniani. Unaweza hata kutumia nguvu zako ili kujaribu kuleta amani na umoja na kuvunjika moyo baadaye kwa kuona kwamba miradi yako haitimizwe. Kujua kwamba Mungu anatumia nguvu zake kupitia Ufalme wake, jambo hilo litakusaidia kujikaza kutumia bidii yako kwa njia nzuri zaidi, kwa kuwa raia wa Ufalme huo.

[Picha katika ukurasa wa 14]

Tafuta majibu mengine ya maulizo juu ya habari za Biblia kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine