HABARI FULANI ZA ULIMWENGU
Asia ya Kusini-Mashariki
Kulingana na shirika Hazina ya Wanyama wa Pori Ulimwenguni, kati ya mwaka wa 1997 na 2011, aina mupya nyingi za mimea na wanyama, kutia ndani nyoka wenye macho mekundu sana wanaoishi katika mashimo (Trimeresurus rubeus), zilivumbuliwa katika Eneo la Mekong, linalochukua sehemu ya Kambodia, Laos, Myanmar, Thailand, Vietnam, na jimbo la Yunnan, katika inchi ya China. Kati ya aina mupya zilizovumbuliwa katika mwaka wa 2011 peke yake, kulikuwa aina 82 za mimea, aina 21 za wanyama wanaotambaa, aina 13 za samaki, aina 5 za vyura na wanyama wengine wanaofanana na vyura, na aina 5 za wanyama wanaonyonyesha.
Ulaya
Ripoti moja inasema kwamba biashara ya watu imekuwa tatizo kubwa katika “inchi zote za Umoja wa Ulaya.” Watu wanauzishwa ili kutumiwa vibaya kingono, kufanya kazi ya kulazimishwa, na hata “biashara isiyokubaliwa ya viungo vya mwili wa mwanadamu.” (The Moscow Times) Kwa sababu ya umaskini, ukosefu wa kazi, na ukosefu wa usawa kati ya wanaume na wanawake, wachuuzi hao wanapata kwa vyepesi biashara hiyo ya watu.
Nouvelle-Zélande
Watu wenye walifanya uchunguzi juu ya watoto na vijana wanaoangalia sana televisheni, walisema kwamba kuangalia televisheni kwa muda murefu ndiyo sababu “inayofanya kuwe na ongezeko la watu walio na tabia ya kuuzi wengine tangu wanapoanza kukomaa.” Uchunguzi wa watu hao unaunga mukono wazo la kwamba watoto wanapaswa kuangalia tu “vipindi vizuri vya televisheni kwa saa 1 mupaka saa 2 kwa siku.”
Alaska
Karibu “vijiji vya Wazaliwa wa Alaska” vyote vinapatikana pembeni-pembeni ya bahari ao karibu na mito, na vijiji 86 juu ya 100 kati ya vijiji hivyo vinapatwa na mafuriko na kuporomoka kwa udongo. Ripoti zinaonyesha kwamba kuongezeka kwa joto kunachelewesha kutokea kwa barafu inayolinda pembeni ya bahari, na hilo linafanya vijiji hivyo vipigwe kwa vyepesi na upepo wa zoruba za wakati wa kuanguka kwa majani.
Ulimwengu
Hata ikiwa feza nyingi zinatumiwa ili kutokeza umeme wa kiteknolojia, kama vile umeme wa upepo na nguvu za jua, Maria van der Hoeven aliye musimamizi mukubwa wa Shirika la Kimataifa la Umeme, anasema kwamba, “kiasi cha umeme kinachotokezwa leo ni chenye kuchafuka kama ilivyokuwa miaka 20 iliyopita.”