Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 10/14 uku. 8-9
  • Namna ya Kupambana na Kishawishi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kupambana na Kishawishi
  • Amuka!—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TATIZO
  • Jaribu
    Amuka!—2017
  • Mukuwe Waangalifu ili Musiingie Katika Jaribu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Unaweza Kushinda Kishawishi!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Namna ya Kupiganisha Tamaa za Mubaya
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2014
g 10/14 uku. 8-9
Kijana anamuacha binti ambaye alimuomba namba yake ya telefone

MUSAADA KWA FAMILIA | VIJANA

Namna ya Kupambana na Kishawishi

TATIZO

“Wakati fulani binti wananiomba namba yangu ya telefone na kuniambia kama wanataka walale na mimi. Ninakataa na kuwaacha. Lakini ninaendelea kujiuliza, ‘Ikiwa ningemupatia namba yangu, kungetokea nini?’ Kwa kweli, binti fulani kati yao wana sura nzuri. Ni rahisi kujiuliza, ‘Sababu gani sikuwapatia?’” —Carlos,a 16.

Je, unapambana na kishawishi kama vile Carlos? Ikiwa ndiyo, unaweza kubaki mwaminifu wakati unashawishiwa.

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Panya ambaye ametegwa na kipande cha fromaje iliyo katika mutego

IIkiwa haubaki mwaminifu wakati unashawishiwa, utaumia

Kila mutu anashawishiwa, hata watu wakubwa. Vishawishi vinaweza kutokea katika njia mbalimbali. Mutume Paulo alikuwa mutu mukubwa wakati aliandika: ‘Kwa kweli naipenda sheria ya Mungu kulingana na mutu niliye kwa ndani lakini mimi naona ndani ya viungo vyangu sheria nyingine ikipigana na sheria ya akili yangu na kunichukua mateka kwa sheria ya zambi.’ (Waroma 7:22, 23) Ijapokuwa mikazo, Paulo aliendelea kupambana, na wewe pia unaweza kufanya hivyo! Sababu gani ujifanye mutumwa wa tamaa zako? (1 Wakorintho 9:27) Kujifunza kupambana na vishawishi wakati ungali kijana kutakuepusha na mahangaiko ya sasa na kutakusaidia sana wakati utakuwa mukubwa.

Vyombo vya habari vinachochea tamaa mbaya. Biblia inazungumuzia ‘tamaa zinazotokea wakati wa ujana.’ Tamaa hizo ziko nguvu kwa kiasi fulani. (2 Timotheo 2:22) Lakini mara nyingi filme, TV, muziki, na vitabu vinavyoandikwa kwa ajili ya vijana vinachochea tamaa hizo kwa kufanya ionekane kuwa kuanguka katika kishawishi kunakubalika. Kwa mufano, ikiwa watu wawili katika filme ‘wanapendana,’ ni wazi kwamba watalala pamoja wakati fulani katika filme hiyo. Lakini, Biblia inasema kama mwanaume na mwanamuke wana uwezo wa “kujiepusha na tamaa za mwili.” (1 Petro 2:11) Maana yake unaweza kuamua kubaki mwaminifu wakati wa vishawishi. Namna gani?

MAMBO YA KUFANYA

Jua uzaifu wako. Munyororo unaweza kukatika haraka ikiwa una kiunganishi zaifu. Vile vile, uamuzi wako wa kufanya mambo mazuri unaweza kujaribiwa katika hali ambamo unaweza kuanguka kwa vyepesi. Ni katika hali gani unapaswa kuwa mwangalifu?—Kanuni ya Biblia: Yakobo 1:14.

Jitayarishe kwa ajili ya kishawishi. Fikiria hali ambamo unaweza kushawishiwa. Tatayarisha katika akili jambo ambalo utafanya ikiwa kishawishi kinatokea.—Kanuni ya Biblia: Methali 22:3.

Jua kabisa tofauti kati ya mema na mabaya. Biblia inasema kwamba wakati alishawishiwa kufanya uasherati, Yosefu alisema: ‘Ninawezaje kufanya ubaya huu mukubwa na kwa kweli nimutendee Mungu zambi?’ (Mwanzo 39:9) Neno “Ninawezaje” linaonyesha kama Yosefu alijua kabisa mema na mabaya. Namna gani wewe?

Tafuta marafiki wanaoweza kukusaidia. Unaweza kuepuka vishawishi vingi katika maisha yako ikiwa unachagua marafiki walio na maoni kama yako juu ya mwenendo. Biblia inasema: “Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima.”—Methali 13:20.

Epuka hali zinazoweza kufanya iwe vyepesi kuanguka katika kishawishi. Kwa mufano:

  • Ikiwa uko mwanaume usikubali kuwa peke yako na mwanamuke na ikiwa uko mwanamuke usikubali kuwa peke yako na mwanaume.

  • Epuka kutumia Internete wakati na kwenye unaweza kushawishiwa kutazama ponografia.

  • Jiepushe na watu ambao masemi na mwenendo wao vinafanya mabaya yaonekane kuwa yenye kupendeza.

Unaweza kujitilia mipaka gani ili usianguke katika vishawishi?—Kanuni ya Biblia: 2 Timotheo 2:22.

Muombe Mungu akusaidie. Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: ‘Musali sikuzote ili musiingie katika jaribu.’ (Mathayo 26:41) Ukweli ni kwamba Yehova Mungu anataka upambane muzuri na vishawishi, na anaweza kukusaidia ufanye hivyo. Biblia inasema: ‘Hatawaacha mujaribiwe kupita munavyoweza kuhimili, bali pamoja na hilo jaribu ataifanya pia njia ya kutokea kusudi muweze kulivumilia.’—1 Wakorintho 10:13.

a Majina yamebadilishwa.

MAANDIKO YA MAANA

  • ‘Kila mutu anajaribiwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe.’—Yakobo 1:14.

  • ‘Mutu mwerevu ni yule ambaye ameona musiba na kujificha.’—Methali 22:3.

  • ‘Kimbia tamaa zinazotokea wakati wa ujana.’—2 Timotheo 2:22.

Amanda

AMANDA

“Wakati kishawishi kinatokea, ninakiepuka mara moja. Ninaona haiko muzuri kuendelea kuwaza, ‘Ikiwa ninafanya hivyo, itakuwa namna gani’ ao ‘pengine haiko mubaya.’ Kuendelea kuwaza hivyo kunaweza kukuingiza mara moja katika hatari.”

Emily

EMILY

“Epuka hali zinazoweza kukuingiza katika kishawishi. Fanya urafiki na watu wanaokutia moyo ufanye mambo mazuri. Kupambana na vishawishi kunakuzoeza ili uweze kushugulika muzuri na hali ngumu zinazoweza kutokea wakati unaokuja.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine