Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g17 na. 1 uku. 8-9
  • Tabasamu Yako—Ni Zawadi Yenye Unaweza Kutoa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tabasamu Yako—Ni Zawadi Yenye Unaweza Kutoa
  • Amuka!—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KUTABASAMU “KULIFANYA NIJISIKIE MUZURI ZAIDI”
  • Somo 5
    Ninajifunza Biblia
  • Ile Yote Juu Tu Dada Yetu Aliwaonyesha Sura ya Kicheko!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Inawezekana Kuwa na Maisha Yenye Furaha Hata Leo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Kuzungumuza kwa Upole na kwa Upendo
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2017
g17 na. 1 uku. 8-9
Watu wa miaka na rangi mbalimbali wanatabasamu sana

Tabasamu Yako Ni Zawadi Yenye Unaweza Kutoa

UNAFANYA nini wakati mutu fulani anakuonyesha kwa uchangamufu tabasamu [ao, sura yenye kicheko]? Bila shaka unamuonyesha pia tabasamu. Na inawezekana wewe pia unafurahi. Tabasamu yenye kutoka moyoni, ikuwe ya marafiki ao ya watu wenye haujue kabisa inaambukiza, na inaonyesha kwamba mutu anajisikia muzuri moyoni. Mwanamuke mwenye kuitwa Magdalena alisema hivi: “Georg, bwana yangu mwenye amekwisha kufa, alikuwa na tabia ya kutabasamu kwa uchangamufu. Wakati tulikuwa tunaangaliana, nilikuwa ninajisikia muzuri na salama.”

Tabasamu yenye kutoka moyoni inafunua namna mutu anajisikia, kama vile kusikia furaha, na raha. Kulingana na habari moja ya Observer, gazeti lenye kutokea kwenye Internete la Shirika la Sayansi ya Saikolojia (katika Kiingereza), “inaonekana kila mutu anazaliwa na uwezo wa kutabasamu.” Habari hiyo ilionyesha kwamba hata watoto wenye wametoka kuzaliwa wako na uwezo wa “kuelewa muzuri sana ishara za uso.” Habari hiyo ilisema tena hivi: “Watu wanapata habari za maana kupitia tabasamu, na hilo linawasaidia kujua namna watajiendesha.”a

Watafiti kwenye Masomo ya Juu ya Harvard katika inchi ya Amerika walifanya uchunguzi juu ya kikundi cha wazee wenye kugonjwa na namna wanaitikia ishara za uso za wanganga wenye walikuwa wanawatunza. Watafiti hao walionyesha kwamba wagonjwa walijisikia muzuri zaidi na afya yao ya kimwili na ya kiakili ilikuwa muzuri zaidi wakati wanganga “walionekana kuwa wenye kuwachangamukia, kuwahangaikia, kuwajali, na kujitia pa nafasi yao.” Mambo yalikuwa tofauti wakati wanganga hawakuonyesha ishara hizo.

Wakati unatabasamu, unaweza kujiletea faida wewe mwenyewe. Uchunguzi mbalimbali unaonyesha kwamba kati ya faida hizo kuna kujiona kuwa wa maana, kuwa na furaha na kupunguza mukazo wa akili. Lakini kukunja sura, kunaweza kuleta matokeo yenye kuwa tofauti na hayo.

KUTABASAMU “KULIFANYA NIJISIKIE MUZURI ZAIDI”

Magdalena, mwenye tumekwisha kutaja, alikuwa Shahidi wa Yehova wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Alitumwa pamoja na watu wengine wa familia yake kwenye kambi ya mateso ya Ravensbrück katika inchi ya Ujerumani kwa sababu ya kukataa kuunga mukono mawazo ya Wanazi. Anakumbuka hivi: “Wakati fulani walinzi walitukataza kusema na wafungwa wengine. Lakini, hawakuweza kutuzuia kuonyesha ishara za uso. Kuona tu mama na dada yangu wanatabasamu kulifanya nijisikie muzuri zaidi na kulitia nguvu uamuzi wangu wa kuendelea kuvumilia.”

Pengine unaona kwamba mahangaiko ya maisha yanafanya usitabasamu sana. Lakini, kumbuka kwamba mara nyingi mawazo yanatangulia namna mutu anajisikia. (Methali 15:15; Wafilipi 4:8, 9) Kwa hiyo, hata kama uko katika hali ngumu ya namna gani, sababu gani usikazie akili yako juu ya mambo yenye kufaa na yenye kufurahisha wakati inawezekana?b Kusoma Biblia na kusali kumesaidia watu wengi kufanya hivyo. (Mathayo 5:3; Wafilipi 4:6, 7) Kwa kweli, maneno “furaha” na “shangwe” na maneno mengine yenye kutokana na maneno hayo yanapatikana mara nyingi sana katika Biblia! Sababu gani usisome ukurasa moja ao mbili kila siku? Pengine kufanya hivyo kutakusaidia kutabasamu mara nyingi.

Pia, usingojee wengine wakuonyeshe tabasamu. Ukuwe wa kwanza kufanya hivyo; uchangie kuongeza furaha ya mutu mwengine. Ndiyo, uone tabasamu yako kuwa zawadi nzuri kutoka kwa Mungu, yenye inakuletea faida wewe na watu wengine wenye wanaiona.

a Kwa kutumia maneno ya mufano, Biblia inasema kwamba hata Mungu anatabasamu. Andiko la Zaburi 119:135 linasema hivi: ‘Ufanye uso wako utabasamu [kwa kumukubali] mutumishi wako.’—Maelezo ya chini katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya 2013 ya Kiingereza.

b Ona habari “Wewe, Una ‘Karamu Sikuzote’?” katika Amuka! ya Mwezi wa 11, 2013.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine