Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g17 na. 3 uku. 3
  • Biblia—‘Iliongozwa na Roho ya Mungu’ Kabisa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Biblia—‘Iliongozwa na Roho ya Mungu’ Kabisa?
  • Amuka!—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAANA YA MANENO ‘KUONGOZWA NA ROHO’
  • ‘Waliongozwa na Roho Takatifu’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Biblia Ni Neno ya Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Habari Njema Yenye Iko mu Biblia Inatoka Kabisa kwa Mungu?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Namna Muumbaji Amefunua Ahadi Zake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
Amuka!—2017
g17 na. 3 uku. 3
Mukubwa wa kazi anaambia mwandishi wake mambo ya kuandika katika barua

HABARI KUBWA | BIBLIA INATOKA KABISA KWA MUNGU?

BIBLIA​—‘Iliongozwa na Roho ya Mungu’ Kabisa?

UNAAMINI kwamba Biblia inatoka kwa Mungu? Ao unawaza kwamba ni kitabu chenye kuwa na mawazo ya wanadamu tu?

Watu wanaendelea kubishana juu ya jambo hilo, hata wale wenye kujiita Wakristo. Kwa mufano, katika mwaka wa 2014, uchunguzi wenye ulifanywa na shirika la Gallup katika inchi ya États-Unis, ulionyesha kama watu wengi wenye kujiita Wakristo walikubali kama “kuna uhusiano fulani kati ya Biblia na Mungu.” Lakini, mutu 1 kati ya watu 5 wenye waliulizwa alisema kama Biblia ni kitabu cha “hadisi za kutunga, historia, na sheria za zamani zenye ziliandikwa na mwanadamu.” Mawazo haya yenye kupingana kuhusu Biblia yanafanya tufikirie maana ya maneno ‘kuongozwa na roho.’​—2 Timotheo 3:16.

MAANA YA MANENO ‘KUONGOZWA NA ROHO’

Biblia iko na vitabu vidogo-vidogo 66 vyenye viliandikwa na watu karibu 40 kwa muda wa miaka 1600 hivi. Lakini, kama Biblia iliandikwa na wanadamu, namna gani tunaweza kusema kwamba ‘iliongozwa na roho ya Mungu’? Kwa kifupi, maneno ‘kuongozwa na roho ya Mungu’ yanamaanisha kwamba Mungu ndiye Chanzo cha habari yenye kuwa katika maandiko hayo. Biblia inasema hivi: “Wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.” (2 Petro 1:21) Hilo linamaanisha kwamba Mungu alitumia nguvu yake ya utendaji, ni kusema, roho takatifu, ili kutolea waandikaji wa vitabu vya Biblia ujumbe wake. Tunaweza kulinganisha jambo hilo na mukubwa fulani wa kazi mwenye anaambia mwandishi wake maneno ya kuandika katika barua. Barua hiyo haiko ya mwandishi lakini ni ya mukubwa wa kazi.

Waandikaji fulani wa Biblia walisikia ujumbe wa Mungu kupitia malaika. Wengine waliona maono kutoka kwa Mungu. Katika hali fulani, Mungu alitoa ujumbe wake kupitia ndoto. Hata kama wakati fulani Mungu aliachia waandikaji uhuru wa kutumia maneno yao ili kuandika ujumbe wake, wakati mwingine aliwaambia maneno yenye walipaswa kuandika bila kuyabadilisha. Katika hali hizo zote, waandikaji hao waliandika mawazo ya Mungu, hapana mawazo yao.

Namna gani tunaweza kuwa hakika kwamba Mungu ndiye aliongoza waandikaji wa Biblia kupitia roho yake? Tufikirie mambo tatu yenye kuhakikisha kwamba Biblia inatoka kwa Mungu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine