Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g19 na. 1 uku. 12-15
  • Chini ya Ufalme wa Mungu “Amani Itakuwa Nyingi”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Chini ya Ufalme wa Mungu “Amani Itakuwa Nyingi”
  • Amuka!—2019
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UFALME WA MUNGU UTAKUJA WAKATI GANI?
  • NAMNA GANI UFALME WA MUNGU UTAANZA KUTAWALA?
  • UNAWEZA KUFANYA NINI ILI KUFAIDIKA NA UTAWALA WA UFALME?
  • Kweli Kuhusu Ufalme wa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Tumaini
    Amuka!—2018
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2019
g19 na. 1 uku. 12-15
Watu wanafurahia maisha katika Paradiso

NAMNA MAGUMU ITAMALIZWA KABISA

Chini ya Ufalme wa Mungu “Amani Itakuwa Nyingi”

Hivi karibuni, Ufalme wa Mungu wenye tumengojea kwa muda murefu​—serikali ya ulimwengu wote yenye Mungu ameanzisha​—itafanya wanadamu wote ku dunia waishi kwa umoja na amani. Kama vile andiko la Zaburi 72:7 limeahidi, “amani itakuwa nyingi.” Lakini ni wakati gani Ufalme huo utaanza kutawala dunia yote? Utafanya vile namna gani? Na unaweza kufanya nini ili kufaidika na utawala wa Ufalme huo?

UFALME WA MUNGU UTAKUJA WAKATI GANI?

Biblia ilitabiri matukio fulani makubwa yenye ingeonyesha kama Ufalme wa Mungu uko unakuja hivi karibuni. Ile matukio yote inafanyiza “alama” zenye kutia ndani vita kati ya mataifa, njaa, magonjwa, matetemeko mingi ya dunia, na kuongezeka kwa uvunjaji wa sheria.​—Matayo 24:3, 7, 12; Luka 21:11; Ufunuo 6:2-8.

Unabii mwingine unasema hivi: “Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, . . . wenye hawatii wazazi, wenye hawana shukrani, wenye hawana ushikamanifu, wenye hawana upendo wa asili, wenye hawataki makubaliano yoyote, wachongezi, wenye hawajizuie, wakali, wenye hawapendi wema, . . . wenye kujivuna kwa kiburi, wenye kupenda raha kuliko kumupenda Mungu.” (2 Timoteo 3:1-4) Tangu zamani, watu fulani wamekuwa wakionyesha zile tabia. Lakini leo, watu wengi sana wanaonyesha zile tabia.

Unabii mbalimbali wenye tumezungumuzia ulianza kutimia mwaka wa 1914. Kwa kweli, wanahistoria, wakubwa wenye kuheshimiwa katika mambo ya politike, na waandikaji walizungumuzia namna ulimwengu ulibadilika kisha ule mwaka. Kwa mufano, mwanahistoria wa Danemark Peter Munch aliandika hivi: “Vita yenye ilitokea mwaka wa 1914 ilileta mabadiliko makubwa katika historia ya wanadamu. Mbele ya ule mwaka, watu waliwaza kama hali ya ulimwengu itakuwa muzuri zaidi, . . . lakini ule mwaka ulituingiza mu kipindi cha misiba, woga, chuki na cha kukosa amani kila fasi.”

Lakini jambo la kufurahisha ni kwamba, kisha ile mambo yote, kutakuwa hali za amani. Ile inaonyesha kama hivi karibuni Ufalme utaanza kutawala dunia. Yesu alizungumuzia jambo hili la muzuri wakati alitaja alama za siku za mwisho: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”​—Matayo 24:14.

Ile habari njema njo kichwa cha musingi cha ujumbe wenye Mashahidi wa Yehova wanatangaza. Kwa kweli, kichapo chenye wanachapisha sana kinaitwa Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova. Unazungumuzia kwa ukawaida mambo ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utafanyia wanadamu ku dunia.

NAMNA GANI UFALME WA MUNGU UTAANZA KUTAWALA?

Jibu linatia ndani mambo ine ya maana yenye kufuata:

  1. Ufalme hautatumia kiongozi yeyote wa politike wa hii dunia.

  2. Viongozi wa politike wa hii dunia hawatapenda kuacha mamlaka yao na kwa upumbavu watapigana na Ufalme wa Mungu.​—Zaburi 2:2-9.

  3. Ufalme wa Mungu utaharibu serikali za kipolitike zenye zinapenda kuendelea kutawala wanadamu. (Danieli 2:44; Ufunuo 19:17-21) Ile vita ya mwisho yenye itapiganwa mu dunia yote inaitwa Armagedoni.​—Ufunuo 16:14, 16.

  4. Wale wenye wanapenda kujitiisha ku Ufalme wa Mungu wataokoka vita ya Armagedoni na kuingia mu dunia mupya yenye amani. Watafanyiza ile yenye Biblia inaita “kundi kubwa la watu,” wenye pengine hesabu yao itakuwa mamilioni.​—Ufunuo 7:9, 10, 13, 14.

    UFALME WA MUNGU UTAFANYA NINI?

    Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alituonyesha mbele ya wakati mambo yenye atafanya akiwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Aliponyesha wagonjwa na vilema. (Matayo 4:23) Alipatia maelfu ya watu chakula. (Marko 6:35-44) Alikuwa hata na uwezo juu ya nguvu za asili.​—Marko 4:37-41.

    Yesu anafundisha watu wenye wanamuzunguka

    Zaidi ya yote, Yesu alifundisha watu namna ya kuishi kwa amani na umoja. Wote wenye wanatumikisha kwa unyenyekevu mafundisho yake wanakomalisha tabia za muzuri zenye zitawawezesha kuishi kwa furaha chini ya utawala wake milele. Hakuna mwalimu mwingine mwenye anaweza kufanya vile. Unaweza kupata mifano ya muzuri ya mafundisho ya Yesu katika ile yenye kujulikana kuwa Mahubiri ya Mulimani mu Matayo sura ya 5 mupaka sura ya 7. Tunakutia moyo uisome. Maneno ya ile mahubiri iko mwepesi. Lakini ujumbe wenye kuwa ndani ni wenye kujaa hekima na unagusa moyo kabisa.

UNAWEZA KUFANYA NINI ILI KUFAIDIKA NA UTAWALA WA UFALME?

Hatua ya kwanza yenye unaweza kukamata ili kuwa raia wa Ufalme wa Mungu ni kupata elimu. Kwa kweli, wakati alisali kwa Mungu, Yesu alisema hivi: “Uzima wa milele ndio huu, wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli, na ule mwenye ulituma, Yesu Kristo.”​—Yohana 17:3.

Wakati watu wanamujua Yehova Mungu kuwa Mutu wa kweli, wanapata faida mu njia mingi. Tufikirie faida mbili kati ya zile faida: Kwanza, wanakuwa na imani yenye nguvu katika Yehova. Ile imani yenye kutegemea mambo yenye kuwa hakika, inawafanya wakuwe hakika kama Ufalme wa Mungu ni kitu cha kweli kabisa na kuwa utawala wake uko karibu. (Waebrania 11:1) Pili, upendo wao kwa Mungu na jirani unakuwa wenye nguvu zaidi. Upendo wao kwa Mungu unawachochea wamutii yeye kwa kupenda. Upendo wao kwa jirani unawachochea kutumikisha maneno ya Yesu yenye kusema hivi: “Kama vile munataka watu wawatendee ninyi, muwatendee kwa njia ileile.”​—Luka 6:31.

Kama Baba mwenye upendo, Muumbaji wetu anatutakia mambo ya muzuri sana. Anapenda tukuwe na ile yenye Biblia inaita “uzima wa kwelikweli.” (1 Timoteo 6:19) Leo uzima hauko “wa kwelikweli.” Kwa mamilioni ya watu, maisha iko nguvu sana, na wanapaswa kujikaza sana ili waendelee kuishi. Ili ujue namna ule “uzima wa kwelikweli” utakuwa, fikiria mambo fulani ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utafanyia raia wake.

NAMNA UZIMA WA KWELIKWELI UTAKUWA

  • “Katika siku zake [wakati Kristo atatawala akiwa Mufalme] mwenye haki atasitawi, na amani itakuwa nyingi . . . Atakuwa na raia . . . mupaka kwenye miisho ya dunia.”​—Zaburi 72:7, 8, 13, 14.

  • “[Mungu] anamaliza vita katika dunia yote. Anavunja upinde na kuvunja mukuki vipande-vipande.”​—Zaburi 46:9.

  • “Kutakuwa nafaka nyingi juu ya dunia; itajaa sana kwenye kichwa cha milima.”​—Zaburi 72:16.

  • “Watajenga nyumba na kuishi ndani, na watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatajenga ili mutu mwingine akae ndani, wala hawatapanda ili wengine wakule. . . . Wachaguliwa wangu watafurahia kwa ukamili kazi ya mikono yao.”​—Isaya 65:21, 22.

  • “Hema ya Mungu iko pamoja na wanadamu . . . Atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—Ufunuo 21:3, 4.

Watu wanafurahia maisha mu Paradiso

Wakati wa utawala wa Ufalme, watu wataishi kwa amani na usalama na watakuwa na chakula mingi

WAZO KUBWA

MAFUNDISHO YA YESU INAPATIA WATU NGUVU YA KUFANYA MAMBO YA MUZURI. WOTE WENYE WANAKUBALI ILE MAFUNDISHO WATAISHI KWA UMOJA NA AMANI KABISA CHINI YA ILE SERIKALI YA ULIMWENGU WOTE

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine