KITULIZO KWA WALE WENYE KUWA NA MUKAZO
Ni Mambo Gani Yenye Inaleta Mukazo?
Kituo kimoja chenye kujulikana sana chenye kuitwa Mayo Clinic kinasema hivi: “Watu wazima wengi wanasema kama wako na mukazo wenye kuendelea kuongezeka. Maisha katika ulimwengu wa leo, ni yenye kujaa mabadiliko na wasiwasi kuhusu wakati wenye kuja.” Mambo yenye kufuata ni kati ya mambo yenye kufanya watu wakuwe na mukazo:
ndoa kuvunjika
kifo cha mupendwa
ugonjwa mukali
aksidenti kali
uvunjaji wa sheria
kuwa na mambo mingi sana ya kufanya mu maisha
misiba ya asili ao yenye kuletwa na watu
mikazo kwenye masomo ao kwenye kazi
wasiwasi kuhusu kupata na kuchunga kazi yenye itakusaidia kupata feza za kutosha ili kuhangaikia familia