Utangulizi
Kwa kiasi fulani, kila mutu alishaka kupatwa na mateso; inaweza kuwa ugonjwa, aksidenti, musiba wa asili, ao kutendewa kwa njia ya jeuri.
Watu wanapenda kujua sababu gani wanateseka.
Wamoja wanasema kama mateso ni jambo fulani lenye lilishaka kupangwa ao wanasema kama hakuna jambo lolote lenye tunaweza kufanya ili kuepuka mateso.
Wengine wanaamini kama tunateseka kwa sababu ya mambo fulani ya mubaya yenye tumetoka tu kufanya mu maisha ya sasa ao yenye tulifanyaka mu maisha ya zamani.
Mara mingi mateso inafanya watu wajiulize maulizo mingi.