Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/7 uku. 3
  • Mambo Mabaya Yanaongezeka Sana

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo Mabaya Yanaongezeka Sana
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Mabaya Yanafikia Watu Wazuri—Sababu Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mungu Njo Anatuleteaka Mateso?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Utangulizi
    Amuka!—2020
  • Ulizo la 3: Sababu Gani Mungu Anaacha Niteseke?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/7 uku. 3

Kichwa | SABABU GANI MAMBO MABAYA YANAFIKIA WATU WAZURI?

Mambo Mabaya Yanaongezeka Sana!

Watu wa familia wanaolemewa na uchungu na huzuni

Smita,a mwanamuke aliyekuwa na miaka 35 katika muji wa Dhaka, Bangladesh, alijulikana kuwa mutu mwenye upendo na mwenye kuhangaikia wengine. Watu walimujua kuwa mwanamuke kijana mwenye bidii na mwenye furaha aliyetaka kusaidia wengine wajue mambo yenye alijifunza juu ya Mungu. Watu wa familia yake na marafiki wake walihuzunika sana wakati Smita aligonjwa kwa gafula na kufa bila kumaliza juma moja!

James na bibi yake, walikuwa wangali vijana, walikuwa na miaka kati ya 31 na 40. Katika kipindi fulani cha kuchipuka kwa majani, walienda kutembelea marafiki wao katika sehemu iliyo pembeni ya bahari ya Mashariki mwa inchi ya Amerika. Hawakurudi tena nyumbani kwao katika muji wa New York. Walipokuwa katika muji kwenye walitembelea, walifanya aksidenti mbaya ya motokari na kuacha marafiki wao na wafanyakazi wenzao katika huzuni kubwa.

Hauhitaji kuwaza sana ili kuona kwamba mambo mabaya na mateso vinaongezeka sana leo. Vita inaua raia na maaskari pia. Watu wasio na kosa wanauawa na kutendewa vibaya. Aksidenti zenye kuua na magonjwa mabaya sana vinapata watu bila kuchagua miaka yao ao cheo chao katika maisha. Misiba ya asili inafagia vikundi vya watu bila kuchagua. Ubaguzi na ukosefu wa haki ni mambo yenye kuenea sana. Labda wewe pia umekwisha kubaguliwa ao kutendewa bila haki.

Ni jambo la kawaida kuuliza maulizo kama haya:

  • Sababu gani mambo mabaya yanafikia watu wazuri?

  • Mungu ndiye analetea watu mambo kama hayo?

  • Misiba inatokea yenyewe tu, ao inaletwa na wanadamu?

  • Inaweza kuwa Karma, ni kusema, matokeo ya mambo mutu alifanya katika maisha yake ya zamani, yanayomuletea mateso?

  • Ikiwa kuna Mungu mweza-yote, sababu gani hawalinde watu wazuri wasipatwe na mambo mabaya?

  • Kuna wakati watu wataishi bila kupatwa na mambo mabaya na mateso?

Ili kujibu maulizo hayo, ni lazima tuelewe majibu ya maulizo haya mawili ya maana: Sababu gani mambo mabaya yanatokea, na Mungu atafanya nini?

a Majina yamebadilishwa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine