Mambo Yenye Watu Fulani Wanaamini
Wahindu
wanaamini kama mateso inatokana na matendo ya mubaya ya mutu, yenye amefanya mu maisha yake ya sasa ao ya zamani. Wanaamini kama mutu anaweza kufikia moksha, ni kusema, kuwekwa huru ili asikuwe anazaliwa tena upya, kwa kujifunza kutohangaikia mambo ya ulimwengu huu.
Waislamu
wanaona mateso kuwa malipizi ya zambi kwa wenye hawako waamini na jaribu la imani kwa waamini. Sayyid Syeed, mutu mwenye elimu na musimamizi wa Jamii ya Kiislamu ya Amerika ya Kaskazini (Islamic Society of North America), anasema kama mateso inatukumbusha kama tunapaswa “kuendelea kuwa wenye shukrani kwa Mungu kwa sababu ya baraka zake na kuendelea kukubali kama tunapaswa kutegemeza wenye wako katika uhitaji.”
Wayahudi
wanaamini kama mateso inatokana na matendo ya mutu mwenyewe. Wayahudi fulani wanasema kama kutakuwa ufufuo, na kama kisha ufufuo mutu mwenye aliteseka bila kosa atatendewa kwa haki. Dini ya Kiyahudi ya kifumbo, yenye kuitwa Kabala, inafundisha kama mutu anazaliwa tena katika mwili ingine, na ile inapatia mutu nafasi mbalimbali za kuonyesha kuwa anatubu makosa yake.
Wabuda
wanaamini kama mutu anaweza kupata mateso katika vipindi mingi vya maisha, ni kusema, mutu anazaliwa tena upya mara mingi mupaka mawazo yake ya mubaya, hisia, na tamaa zake za mubaya zifikie mwisho. Kupitia hekima, matendo ya muzuri, na akili yenye kutulia, mutu anaweza kufikia nirvana, ni kusema, hali ya kutokuteseka tena.
Wafuasi wa Confucius
Kamusi moja (A Dictionary of Comparative Religion) inasema kama wafuasi wa Confucius wanaamini kama mateso inatokana na “kushindwa kwa mwanadamu na pia makosa yake.” Imani yao inasema kuwa hata kama mateso inaweza kupunguzwa kwa kufanya mambo ya muzuri, mateso mingi inatokana na “viumbe wa roho wenye kuwa na nguvu zaidi kuliko wanadamu. Katika hali za vile, mutu anapaswa tu kukubali mambo yenye wale viumbe wamepanga.”
Dini fulani za kikabila
zinaamini kama mateso inatokana na ulozi. Kulingana na ile imani, walozi wanaweza kuletea mutu bahati ya muzuri ao musiba, na ili kupunguza mateso yenye wanaweza kuleta ni lazima kufanya desturi fulani zenye wanaomba. Inaaminiwa kuwa wakati mutu ni mugonjwa, desturi na dawa za wachawi ao wafumu zinazuia kazi ya walozi.
Wakristo
wanaamini kama mateso inatokana na zambi ya watu wawili wa kwanza, namna inazungumuziwa katika Biblia mu kitabu cha Mwanzo. Lakini, watu wa dini mingi wameongeza mawazo yao kwenye fundisho hilo. Kwa mufano, Wakatoliki fulani wanasema kama mutu anaweza ‘kutolea Mungu’ mateso yenye iko anapambana nayo ili kumuomba asaidie kanisa ao atumie ile mateso ili kuokoa mutu mwingine.
IKIWA UNAPENDA KUJUA MINGI ZAIDI
Angalia video Mungu Anakubali Dini Zote? yenye kuwa ku jw.org.