Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g20 na. 2 uku. 10-11
  • 3. Juu ya Nini Watu Wazuri Wanateseka?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 3. Juu ya Nini Watu Wazuri Wanateseka?
  • Amuka!—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Ni Muzuri Kujiuliza Vile?
  • Jambo la Kufikiria
  • Mambo Yenye Biblia Inasema
  • 4. Mungu Alituumba Juu Tuteseke?
    Amuka!—2020
  • Mambo Biblia Inasema Juu ya Mateso
    Amuka!—2015
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2020
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2020
g20 na. 2 uku. 10-11
Wazazi wanaangalia mutoto wao kijana mwenye kulala ku kitanda cha hospitali kisha sehemu ya mukono wake kukatwa.

3. Juu Ya Nini Watu Wazuri Wanateseka?

Juu ya Nini Ni Muzuri Kujiuliza Vile?

Juu wakati watu wazuri wanateseka, ile inaonekana kuwa ni ukosefu wa haki. Watu fulani wanaona kama haiko lazima kuwa mutu muzuri ikiwa utateseka tu.

Jambo la Kufikiria

Watu fulani wanaamini kama wanadamu wanakufa na kuzaliwa tena na tena. Wanasema kama watu wenye walifanya mambo ya muzuri wanazaliwa tena katika maisha ya muzuri, lakini wenye walifanya mambo ya mubaya wanazaliwa tena katika maisha ya mateso. Kulingana na ile imani, hata mutu muzuri anaweza kuteseka ikiwa alifanyaka mambo ya mubaya katika “maisha yake ya zamani.” Sasa . . .

  • Ile mateso iko na kusudi gani, wakati mutu mwenye inawaziwa kama alizaliwa tena hawezi hata kukumbuka maisha yake ya zamani?

  • Sababu gani tunatumika sana ili kuendelea kuwa na afya ya muzuri na tunaepuka kufanya aksidenti ikiwa maisha yetu ilishaka kupangwa kulingana na mambo yenye tulifanya zamani?

    IKIWA UNAPENDA KUJUA MINGI ZAIDI

    Angalia video Sababu Gani Mungu Anaacha Mateso? yenye kuwa ku jw.org.

Mambo Yenye Biblia Inasema

Mateso haiko malipizi kutoka kwa Mungu.

Tofauti na ile, mateso mingi inatokea bila kutazamiwa​—mara mingi, ni kwa sababu ya kuwa fasi ya mubaya kwa wakati wa mubaya.

“Haiko wenye mbio ndio wanashinda kila mara katika mbio, wala haiko wenye nguvu ndio wanashinda katika vita, wala haiko wenye hekima ndio wanapata kila mara chakula, wala haiko wenye akili ndio wanakuwa kila mara na utajiri, wala haiko wenye ujuzi ndio wanafanikiwa kila mara, kwa sababu wakati na matukio yenye hayatazamiwe yanafikia wote.”​—MUHUBIRI 9:11.

Hali yetu ya zambi ni kati ya mambo yenye inafanya tuteseke.

Mara mingi watu wanatumia neno “zambi” ili kumaanisha jambo la mubaya lenye mutu anafanya. Lakini, Biblia inatumia pia neno hilo ili kuzungumuzia hali yenye wanadamu wote, wabaya na wazuri, waliriti.

“Nilizaliwa nikiwa na hatia ya kosa, na nilikuwa na zambi tangu wakati mama yangu alichukua mimba yangu.”​—ZABURI 51:5, Maelezo ya chini.

Zambi imekuwa na matokeo ya mubaya sana kwa wanadamu.

Haikuharibu tu uhusiano wetu pamoja na Muumbaji wetu, lakini pia imefanya tusikuwe katika upatano na viumbe vingine vya Mungu. Na ile imeletea wanadamu, wakiwa mutu mumoja-mumoja na hata wote kwa ujumla, mateso makubwa.

“Wakati ninataka kufanya mambo yenye kuwa sawa, mambo ya mubaya yako pamoja na mimi.”​—WAROMA 7:21.

“Uumbaji wote unaendelea kulia kwa maumivu pamoja na kuwa katika uchungu pamoja.”​—WAROMA 8:22.

Juu ya nini watu wazuri wanateseka?

Mingi kati ya mateso yetu inaletwa na hali yetu ya zambi, yenye watu wazuri na wabaya waliriti. Ile hali ya zambi ni kati ya mambo yenye kufanya tukuwe na matatizo ya kimwili na ya kiakili, na pia inafanya tukuwe na tabia zenye kuletea wengine mateso.

Ile njo ilikuwa kusudi la Mungu kwa wanadamu? Mungu alituumba juu tuteseke?

Pata jibu kwenye ulizo la 4.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine