Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g20 na. 3 uku. 10-11
  • Ufanye Urafiki na Watu Wenye Kuwa Tofauti na Wewe

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ufanye Urafiki na Watu Wenye Kuwa Tofauti na Wewe
  • Amuka!—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tatizo
  • Kanuni ya Biblia
  • Faida ya Kufanya Urafiki na Watu Wenye Kuwa Tofauti na Sisi
  • Mambo Yenye Unaweza Kufanya
  • Waliachana Kabisa na Ubaguzi
    Amuka!—2020
  • Onyesha Upendo
    Amuka!—2020
  • Uchagule Marafiki Wazuri
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Mafundisho ya Mungu Yanamaliza Chuki
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2020
g20 na. 3 uku. 10-11
Wanamuke ine wa rangi tofauti ya ngozi wako wanazungumuza na kucheka pamoja wakati watoto wao wako wanacheza.

Ufanye Urafiki na Watu Wenye Kuwa Tofauti na Wewe

Tatizo

Kama tunaepuka watu wenye hatufurahie, ile inaweza kufanya tukuwe na ubaguzi zaidi. Na kama tunafanya tu urafiki na watu wenye kuwa kama sisi, tunaweza kuanza kuwaza kama namna yetu ya kufikiri, namna tunajisikia, na namna tunatenda njo tu ya muzuri.

Kanuni ya Biblia

“Mufungue mioyo yenu wazi.” ​—2 WAKORINTO 6:13.

Ile inamaanisha nini? Wakati Biblia inatumia neno “moyo” inazungumuzia hisia na upendo wetu. Ikiwa tunapenda tu watu wenye kuwa kama sisi, tunafanya moyo wetu usikuwe wazi. Ili tuepuke ile tatizo, tunapaswa kuwa tayari kufanya urafiki na watu wenye kuwa tofauti na sisi.

Faida ya Kufanya Urafiki na Watu Wenye Kuwa Tofauti na Sisi

Wakati tunajua watu wengine kipekee, tunafikia kuelewa ni juu ya nini wanafanya mambo kwa njia tofauti. Na wakati tunafanya nao urafiki, tunaanza kuwaona kama hawako tofauti na sisi. Tunafikia kuwaona kuwa wa maana sana, na tunaanza kujitia pa nafasi yao.

Tufikirie mufano wa Nazaré. Zamani, alikuwa anabagua watu wenye walitoka mu inchi zingine. Alifasiria jambo lenye lilimusaidia kuacha ubaguzi. Anasema hivi: “Nilipitisha wakati pamoja nao na kutumika pamoja nao. Nilikutana na watu wenye walikuwa tofauti kabisa na vile wengine walikuwa wanawasema. Wakati tu unafanya urafiki na mutu wa desturi ingine, ile inakusaidia usimubague. Na tena, unafikia kumupenda na kumuona kuwa wa maana.”

Chagua Muzuri Marafiki

Watu fulani wanachagua kuwa na tabia zenye zinaweza kuwaletea hatari na kuletea wengine hatari. Kwa hiyo, tunapaswa kuchagua muzuri marafiki wetu. Kukataa kufanya urafiki na watu wenye hawako waaminifu ao wenye kuwa na mwenendo mubaya hakumaanishe kama tuko na ubaguzi. Hata kama hatupaswe kutendea mubaya watu wenye wanazarau kanuni za mwenendo muzuri ao kuwazuia wasifanye mambo yenye wanapenda, ni jambo la hekima tusiwafanye kuwa marafiki wetu. ​—Mezali 13:20.

Mambo Yenye Unaweza Kufanya

Tafuta nafasi ya kuzungumuza na watu wa inchi ingine, kabila, ao wa luga ingine. Unaweza

  • Kuwaomba wakuambie mambo fulani kuwahusu.

  • Kuwaalika ku chakula.

  • Kuwasikiliza kwa uangalifu wakati wanakuelezea maisha yao, na utafute kujua mambo yenye wanaona kuwa ya maana.

Ikiwa unajikaza kuelewa mambo yenye watu fulani walikutana nayo, utajua ni juu ya nini wako na sifa fulani. Na ile itakusaidia uwapende na kupenda kikundi chao.

Mufano wa Kweli: Kandasamy na Sookammah (wa Inchi ya Kanada)

“Tulikomalia mu Afrika ya Kusini wakati wa ubaguzi wa rangi ya ngozi. Walilazimisha watu wa rangi tofauti ya ngozi wasiishi pamoja, na ile ikachochea ubaguzi kati ya watu rangi tofauti ya ngozi. Hatukukuwa wazungu, na tulichukia sana wazungu juu wa moja kati yao walitutendea kama watu wa hali ya chini. Ile wakati tuliwaza kama ile haiko ubaguzi. Lakini tuliona kama sisi njo walibagua.

“Juu tubadilishe mawazo yetu, tulikamata hatua ya kufungua mioyo yetu wazi na tukakuwa na marafiki wa desturi mbalimbali. Wakati tulianza kupitisha wakati na wazungu, tulielewa kama tuko na mambo mingi yenye kufanana. Sisi wote tunapatwa na mambo ileile na tunapatwa na magumu ileile.

“Tulikamata hata mupango wa kukaribisha mu nyumba yetu bibi na bwana wazungu, na waliishi mu nyumba yetu siku mingi. Tulifikia kuwajua muzuri. Bila kukawia tukakuwa marafiki na tukaanza kuona kama sisi wote tuko sawasawa. Ile ilitusaidia tukuwe na mawazo yenye kufaa kuhusu wazungu.”

Sasa Ni Ndugu wa Kweli

Johny na Gideon wako wanasalimia watoto inje ya Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova.

Hata kama Johny na Gideon walikuwa na rangi tofauti ya ngozi, na kila mutu alikuwa na chama yake ya politike, walifikia kuwa marafiki wa sana.

Angalia video Johny na Gideon: Zamani Walikuwa Maadui, Sasa Ni Ndugu. Tafuta ile video ku jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine