Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g24 na. 1 uku. 10-12
  • Juu ya Nini Batu Habaheshimiane Tena mu Familia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Batu Habaheshimiane Tena mu Familia?
  • Amuka!—2024
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA KUHESHIMIANA MU FAMILIA?
  • MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA
  • MAMBO YENYE TUKO NAFANYA
  • Unaweza Kupata Musaada
    Amuka!—2020
  • Musaada Zaidi Kwa Ajili Ya Familia
    Amuka!—2018
  • Pata Hekima Yenye Itakusaidia mu Maisha ya Kila Siku ku JW.ORG
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2022
  • Namna ya Kujifunza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2024
g24 na. 1 uku. 10-12
Bwana moya mwenye iko natumikisha telefone hafurahi wakati bibi yake iko napenda kumuongelesha. Mutoto yabo mwanaume iko nabaangalia.

Juu ya Nini Batu Habaheshimiane Tena mu Familia?

JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA KUHESHIMIANA MU FAMILIA?

Wakati batu mu familia banaheshimiana, ile inafanyaka mu familia mukuwe amani.

  • Kitabu moya (The Seven Principles for Making Marriage Work) inasema kama wakati bibi na bwana banaheshimiana, ile ni njia moya yenye banatumia juu ya kuonyeshana upendo “ikuwe mu mambo ya kidogo-kidogo ao mu mambo ya mukubwa ya mu maisha ya kila siku.”

  • Uchunguzi moya unaonyesha kama batoto benye balijifunza kuheshimia bengine, habajionake kuwa ba bure, banakuwaka na uhusiano wa muzuri pamoya na bazazi yabo na mara mingi habakuwake na matatizo ya kihisia na ya kiakili.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Mupange kuzungumuzia ile jambo mu familia. Kwanza, muhakikishe kama kila mutu mu familia anaelewa maana ya kuonyesha heshima. Pili, muandike tabia zenye kila mutu mu familia anapaswa kuonyesha na zenye kila mutu anapaswa kuepuka. Tatu, muzungumuzie ile jambo mu familia juu kila mutu ajue mambo yenye anapaswa kufanya juu ya kuonyesha heshima.

“Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio.”—Mezali 21:5.

Uonyeshe mufano. Fikiria namna unatendaka. Unakuwaka nachambua-chambua batu ya familia yako wakati banafanya makosa, kuchekelea mawazo yabo, ao kufanya sawa vile hauhangaikie mambo yenye biko nasema na kubakatiza wakati biko nakusemesha?

Shauri: Ujikaze kuona heshima kuwa jambo yenye unapaswa kuonyesha bibi ao bwana yako na batoto yako; hapana sawa jambo yenye unaweza kubaonyesha kama unapenda.

“Katika kuonyeshana heshima, mukuwe wa kwanza.”—Waroma 12:10.

Muheshimiane hata kama hamukubaliane. Wakati uko najieleza, uepuke maneno sawa vile “weye unakuwaka tu hivi” ao “weye haufanyake hivi.” Maneno ya vile inaweza kuumiza ao kukasirisha batu ya famila yako na hata kufanya hali ya familia yako iharibike tena zaidi.

“Jibu la upole linatuliza kasirani kali, lakini neno la ukali linachochea hasira.”—Mezali 15:1.

Kijana moya mwanamuke iko naangalia video ku jw.org.

MAMBO YENYE TUKO NAFANYA

Mashahidi wa Yehova wanatiaka moyo batu ya familia batendeane kwa heshima. Njo maana, mara mingi banazungumuziaka heshima mu habari mbalimbali, vitabu, mabroshua, na mu mavideo yenye banatoleaka batu kwa bure.

KWA AJILI YA BIBI NA BWANA: Sehemu Musaada kwa Familia inaweza kusaidia bibi na bwana wajue namna ya . . .

  • kuwa wasikilizaji wazuri

  • kuepuka tabia ya kuacha kusemeshana

  • kuacha kugombana

(Utafute sehemu “Musaada kwa Familia” ku jw.org)

KWA AJILI YA WAZAZI: Sehemu Musaada kwa Familia inaweza kusaidia bazazi basaidie batoto yabo . . .

  • kukuwa natii

  • kukuwa nafanya kazi za mu nyumba

  • kusema “tafazali” na “aksanti”

(Utafute sehemu “Kukomalisha Watoto” na “Kukomalisha Vijana” ku jw.org)

Ona pia nyongeza, “Maswali Ambayo Wazazi Huuliza,” mu kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1. (Utafute “Maswali Ambayo Wazazi Huuliza” ku jw.org)

KWA AJILI YA VIJANA: Sehemu Vijana yenye kuwa ku jw.org iko na habari mbalimbali, video, na karatasi za mazoezi zenye zinaweza kusaidia vijana . . .

  • wasikilizane na wazazi wao na wakubwa ao wadogo wao

  • wazungumuze na wazazi wao kwa heshima juu ya kanuni za ku nyumba

  • juu wazazi wao wawatumainie

(Utafute sehemu “Vijana” ku jw.org)

Unaweza kutumia site jw.org kwa bure. Haitalomba ulipe makuta, ujiandikishe, ao ufungule konte. Na haitalomba utie habari zako za kipekee.

Joseph Ehrenbogen.

UJIFUNZE MAMBO MINGI

Wakati Joseph Ehrenbogen alioa, alikuwa mutu mwenye kupenda jeuri na mutumwa wa dawa za kulewesha. Juu ya kuona namna kujifunza Biblia pamoya na Mashahidi wa Yehova kulisaidia familia yake, usome habari “Nilijifunza Kujiheshimia na Kuheshimia Wanawake” ku jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine