MAISHA YA MUKRISTO
Pata Hekima Yenye Itakusaidia mu Maisha ya Kila Siku ku JW.ORG
Neno ya Mungu inatupatia kila kitu yenye tuko nayo lazima juu tuweze kupambana na magumu ya mu hizi siku za mwisho zenye kuwa ngumu. (2Ti 3:1, 16, 17) Lakini, wakati fulani tunaweza kuwa na lazima ya mutu wa kutuonyesha namna ya kupata kanuni za Biblia zenye zinapatana kabisa na hali fulani. Kwa mufano, uko muzazi na uko natafuta mashauri juu ya namna ya kukomalisha watoto? Uko kijana na uko naona kama ni nguvu kwako kuendelea kuwa muaminifu kwa Yehova? Ulifiwa na bwana ao bibi, na ungali na huzuni juu ya ile jambo? Utapata habari zenye zitakuongoza mara moya ku kanuni za Biblia zenye zitakusaidia mu ile hali na mu hali zingine mingi ku jw.org.—Mez 2:3-6.
Ku ukurasa wa mwanzo wa jw.org, finyanga ku sehemu MAFUNDISHO YA BIBLIA. (Ona picha ya 1.) Kisha, ku liste yenye kuwa chini, chagua jambo yenye unapenda kujifunza. Ao finyanga ku sehemu MAKTABA> HABARI MBALIMBALI na uchague jambo yenye unapenda kujifunza. (Ona picha ya 2.) Unaweza kupata pia zile sehemu ku JW Library®.a Ikuwe utasoma zile habari ku site ao ku jw library, utazifurahia kabisa. Namna ingine ya kufanya, ni kuandika habari fulani mu sehemu tafuta, ku jw.org.
Andika habari zenye kufuata mu sehemu tafuta, na uandike habari ao mambo mbalimbali yenye unapenda kusoma.
Kukomalisha watoto
Vijana wanashuka moyo
Ikiwa unafiwa na bibi ao bwana
a Kuhusu sehemu fulani, habari zote ziko naonekana tu ku jw.org.