Somo 8
Maisha ya Familia Yanayomupendeza Mungu
Mume ana cheo gani katika familia? (1)
Namna gani mume anapaswa kumutendea muke wake? (2)
Baba wa familia ana madaraka gani? (3)
Muke ana kazi gani katika familia? (4)
Yehova anataka nini kwa wazazi na kwa watoto? (5)
Maoni ya Biblia ni nini kuhusu kutengana na talaka (kuvunja doa)? (6, 7)
1. Biblia inasema kwamba mume ni kichwa cha familia yake. (1 Wakorinto 11:3) Mume anapaswa kuwa na muke mumoja peke yake. Wanapaswa kuwa wenye kuoana kama inavyofaa kulingana na sheria.—1 Timoteo 3:2; Tito 3:1.
2. Mume anapaswa kumupenda muke wake kama vile anavyojipenda yeye mwenyewe. Anapaswa kumutendea muke wake katika njia ile Kristo anawatendea wafuasi wake. (Waefeso 5:25, 28, 29) Hapaswi kamwe kumupiga muke wake au kumutesa katika njia yoyote. Badala yake, anapaswa kumuonyesha heshima na staha (heshima kubwa).—Wakolosayi 3:19; 1 Petro 3:7.
3. Baba anapaswa kutumika kwa nguvu ili aitunze familia yake. Anapaswa kupatia muke wake na watoto chakula, nguo, na nyumba. Baba anapaswa pia kuipatia familia yake mahitaji ya kiroho. (1 Timoteo 5:8) Yeye anachukua uongozi katika kusaidia familia yake kujifunza juu ya Mungu na makusudi Yake.—Kumbukumbu la Torati 6:4-9; Waefeso 6:4.
4. Muke anapaswa kuwa musaidizi mwema kwa mume wake. (Mwanzo 2:18) Anapaswa kumusaidia mume wake katika kufundisha na kuzoeza watoto wao. (Mezali 1:8) Yehova anataka muke atunze familia yake kwa upendo. (Mezali 31:10, 15, 26, 27; Tito 2:4, 5) Muke anapaswa kumustahi sana mume wake.—Waefeso 5:22, 23, 33.
5. Mungu anataka watoto wawe na utii kwa wazazi wao. (Waefeso 6:1-3) Anatazamia wazazi kuelimisha na kuadibisha watoto wao. Wazazi wana lazima ya kupitisha wakati wakiwa pamoja na watoto wao na kujifunza Biblia pamoja nao, kuwatimizia mahitaji yao ya kimwili na ya kimoyoni. (Kumbukumbu la Torati 11:18, 19; Mezali 22:6, 15) Wazazi hawapaswi kuadibisha watoto wao kwa kutumia ukali au jeuri.—Wakolosayi 3:21.
6. Wakati mume na muke wana magumu ya kusikilizana katika ndoa, wanapaswa kujaribu kutumia shauri la Biblia. Biblia inatusukuma kuonyesha upendo na kuwa wenye kusamehe. (Wakolosayi 3:12-14) Neno la Mungu halitii moyo kutengana kuwa njia ya kumaliza magumu madogo-madogo. Lakini muke anaweza kuchagua kumwacha mume wake ikiwa (1) mume anakataa kimakusudi kutegemeza familia yake, (2) mume ni mukali sana hivi kwamba afya ya muke wake na uhai wake vimo katika hatari, au (3) upinzani wake unaopitisha kipimo unafanya isiwezekane kwa muke wake kumuabudu Yehova.—1 Wakorinto 7:12, 13.
7. Mume na muke katika ndoa wanapaswa kuwa waaminifu kila mumoja kwa mwenzake. Uzinifu ni zambi kwa Mungu na kwa mwenzi wa ndoa. (Waebrania 13:4) Kufanya ngonoinje ya ndoa ndiyo sababu pekee kulingana na Maandiko nayoruhusu kuvunja ndoa na kuwa huru kuoa au kuolewa tena. (Matayo 19:6-9; Waroma 7:2, 3) Yehova anachukia wakati watu wanavunja ndoa bila sababu za kimaandiko na kuoa au kuolewa na mutu mwingine.—Malaki 2:14-16.
[Picha katika ukurasa wa 17]
Mungu anatazamia wazazi kuelimisha watoto wao na kuwaadibisha
[Picha katika ukurasa wa 17]
Baba mwenye upendo anatunza familia yake kiroho na kimwili