SEHEMU YA 12
Unaweza Kufanya Nini ili Ukuwe na Maisha ya Familia Yenye Furaha?
Upendo ni jambo la maana ili familia ikuwe na furaha. Waefeso 5:33
Mungu anaomba ndoa ikuwe kati ya mwanaume mumoja na mwanamuke mumoja.
Bwana mwenye upendo anatendeaka bibi yake kwa upole na anajikaza kumuelewa.
Bibi anapaswa kuunga mukono bwana yake.
Watoto wanapaswa kutii ao kusikia wazazi wao.
Ukuwe mupole na muaminifu na usikuwe mukali. Wakolosai 3:5, 8-10
Neno la Mungu linasema kama bwana anapaswa kumupenda bibi yake kama mwili wake mwenyewe, na bibi naye anapaswa kumuheshimia sana bwana yake.
Ni mubaya bibi ao bwana kufanya kitendo cha ndoa na mutu mwingine. Tena, ni mubaya kuwa na bibi wengi ao kuwa na bwana wengi.
Neno la Yehova linafundisha watu wa familia mambo yenye wanapaswa kufanya ili wakuwe na furaha.