Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rq somo 9 uku. 18-19
  • Watumishi wa Mungu Wanapaswa Kuwa Safi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Watumishi wa Mungu Wanapaswa Kuwa Safi
  • Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mungu Anapenda Watu Walio Safi
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Yehova Anapenda Watu Wake Wakuwe Safi
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Tunaweza Kufanya Nini Juu Tukuwe Safi mu Macho ya Mungu?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • “Munapaswa Kuwa Watakatifu”
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
Mungu Anataka Nini Kwetu?
rq somo 9 uku. 18-19

Somo 9

Watumishi wa Mungu Wanapaswa Kuwa Safi

Kwa nini tunapaswa kuwa safi katika kila njia? (1)

Inamaanisha nini kuwa safi kiroho? (2) safi kiadili? (3) safi kiakili? (4) safi kimwili? (5)

Aina gani ya usemi usio safi tunapaswa kuepuka? (6)

1. Yehova Mungu ni musafi na mutakatifu. Yeye anatazamia kwamba watumishi wake wabaki safi​—⁠kiroho, kiadili, kiakili, na kimwili. (1 Petro 1:16) Inaomba kufanya nguvu kabisa ili kubaki safi machoni pa Mungu. Tunaishi katika ulimwengu usio safi. Sisi pia tunapaswa kushindana na maelekeo yetu wenyewe ya kufanya mabaya. Lakini hatupaswi kukata tamaa.

2. Usafi wa Kiroho: Ikiwa tunapenda kumutumikia Yehova, hatuwezi kuendelea kushikamana na yoyote ya yale mafundisho au desturi ya dini isiyo ya kweli. Tunapaswa kutoka katika dini isiyo ya kweli na kuacha kuiunga mukono katika njia yoyote. (2 Wakorinto 6:​14-18; Ufunuo 18:⁠4) Mara tunapojifunza ile kweli kuhusu Mungu, tunapaswa kuwa macho tusidanganywe na watu wanaofundisha mambo yasiyo ya kweli.​—⁠2 Yoane 10, 11.

3. Usafi wa Kiadili: Yehova anapenda kwamba watumishi wake wajiendeshe kama Wakristo wa kweli wakati wote. (1 Petro 2:12) Yeye anaona kila jambo tunalofanya, hata katika siri. (Waebrania 4:13) Tunapaswa kuepuka matendo ya uasherati na mazoea mengine yasiyo safi ya ulimwengu huu.​—⁠1 Wakorinto 6:​9-11.

4. Usafi wa Kiakili: Ikiwa tunajaza akili zetu na mawazo yaliyo safi, yenye kutakata, mwenendo wetu pia utakuwa safi. (Wafilipi 4:⁠8) Lakini ikiwa tunaendelea kufikiri sana juu ya mambo yasiyo safi, matokeo ni kutenda mambo maovu. (Matayo 15:​18-20) Tunapaswa kuepuka namna ya viburudisho ambavyo vinaweza kuharibu akili zetu. Tunaweza kujaza akili zetu mawazo safi kwa kujifunza Neno la Mungu.

5. Usafi wa Kimwili: Kwa kuwa Wakristo wanamwakilisha Mungu, wanapaswa kuchunga mwili wao na mavazi yao vikiwa safi. Tunapaswa kusafisha mikono yetu kisha kutoka chooni, na tunapaswa kuisafisha mbele ya kula chakula au kugusa kitu chochote cha kula. Ikiwa hauna choo, uchafu kama mavi unapaswa kuzikwa. (Kumbukumbu la Torati 23:​12, 13) Kuwa safi kimwili kunasaidia kuwa na afya njema. Nyumba ya Mkristo inapaswa kuwa nzuri inje na ndani. Inapaswa kutofautiana na zile za watu wengine anaoishi pamoja nao ikiwa hivyo mufano mzuri.

6. Usafi Katika Usemi: Watu wa Mungu wanapaswa kila siku kusema kweli. Wanaosema uwongo hawataingia katika Ufalme wa Mungu. (Waefeso 4:25; Ufunuo 21:⁠8) Wakristo hawatumii usemi usio muzuri. Hawasikilizi au kueleza hadisi zisizo safi au mambo ya muzaha ya kuchekesha yaliyo machafu. Kwa sababu ya usemi wao ulio safi, wao wanaonekana kuwa tofauti na wengine mahali pa kazi au kwenye masomo na katika ujirani.​—⁠Waefeso 4:​29, 31; 5:⁠3.

[Picha katika ukurasa wa 19]

Watumishi wa Mungu wanapaswa kuwa safi katika mambo yote

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine