Somo 10
Mazoea Ambayo Mungu Anachukia
Unapaswa kujisikia namna gani juu ya mambo ambayo Mungu anasema ni mabaya? (1)
Aina gani za mwenendo wa ngono (kulalana mwanaume na mwanamuke) ni mbaya? (2)
Namna gani Mkristo anapaswa kuona kusema uwongo? (3) kucheza kamari (muchezo wa kugombea pesa)? (3) kuiba? (3) jeuri? (4) uhusiano na roho wabaya? (5) ulevi? (6)
Namna gani mutu anaweza kuachana na mazoea mabaya? (7)
1. Watumishi wa Mungu wanapenda yaliyo mazuri. Lakini wanapaswa pia kujifunza kuchukia yaliyo mabaya. (Zaburi 97:10) Hilo linamaanisha kuepuka mazoea fulani ambayo Mungu anachukia. Mengine kati ya mazoea hayo ni gani?
2. Uasherati: Kulalana mwanaume na mwanamuke mbele ya kufunga ndoa, uzinifu, kulalana na munyama, kulalana na mutu wa jamaa ya karibu, na kulalana kwa watu wa jinsia moja (wanaume kwa wanaume) ni zambi nzito kwa Mungu. (Walawi 18:6; Waroma 1:26, 27; 1 Wakorinto 6:9, 10) Ikiwa mume na muke hawakufunga ndoa lakini wanaishi pamoja, wanapaswa kutengana au namna nyingine kufanya ndoa yao iandikishwe kisheria.—Waebrania 13:4.
3. Kusema Uwongo, Kucheza Kamari, Kuiba: Yehova hawezi kusema uwongo. (Tito 1:2) Watu wanaopenda kukubaliwa na yeye wanapaswa kuepuka kusema uwongo. (Mezali 6:16-19; Wakolosayi 3:9, 10) Kila aina ya muchezo wa kamari inatokana na pupa. Kwa hiyo Wakristo hawashiriki katika aina yo yote ya muchezo wa kamari, kama vile muchezo wa tombola, mbio za farasi, bingo (muchezo-karata wa pesa). (Waefeso 5:3-5) Wakristo hawaibi. Pia hawanunuwi vitu ikiwa wanajua kwamba viliibwa wala hawachukuwi vitu pasipo ruhusa.—Kutoka 20:15; Waefeso 4:28.
4. Hasira-Hasira, Jeuri: Hasira isiyozuiliwa inaweza kuongoza kwenye matendo ya ujeuri. (Mwanzo 4:5-8) Mutu mujeuri hawezi kuwa rafiki ya Mungu. (Zaburi 11:5; Mezali 22:24, 25) Ni kosa kulipiza kisasi au kurudisha uovu kwa ajili ya mambo mabaya ambayo wengine waliweza kututendea.—Mezali 24:29; Waroma 12:17-21.
5. Uchawi na Uhusiano na Roho Wabaya: Watu wengine wanaomba musaada wa roho wabaya ili kujaribu kuponya magonjwa. Wengine wanatupia maadui zao ulozi ili kuwafanya wawe wagojwa au hata kuwaua. Nguvu inayojificha nyuma ya mazoea hayo yote ni Shetani. Kwa hiyo Wakristo hawapaswi kuwa na sehemu yo yote katika mambo hayo. (Kumbukumbu la Torati 18:9-13) Kubakia karibu sana na Yehova ndiyo ulinzi muzuri zaidi juu ya ulozi ambao watu wengine wanaweza kututupia.—Mezali 18:10.
6. Ulevi: Si kosa kunywa divai ndogo, pombe, au kinywaji kingine chenye kuwa na alkoli. (Zaburi 104:15; 1 Timoteo 5:23) Lakini kunywa sana na pia ulevi ni makosa machoni pa Mungu. (1 Wakorinto 5:11-13; 1 Timoteo 3:8) Kunywa sana kunaweza kuharibu afya yako na kuvunja familia yako. Kunaweza pia kukufanya uwe mutu anayejiachilia kwa upesi sana kuingia katika majaribu mengine.—Mezali 23:20, 21, 29-35.
7. Watu wanaozoea mambo ambayo Mungu anasema ni mabaya “hawatariti Ufalme wa Mungu.” (Wagalatia 5:19-21) Ikiwa kweli unamupenda Mungu na unataka kumupendeza yeye, unaweza kuachana na mazoea haya. (1 Yoane 5:3) Jifunze kuchukia kile Mungu anasema ni kibaya. (Waroma 12:9) Shirikiana na watu ambao wana tabia za kimungu. (Mezali 13:20) Wakristo wenzetu waliokomaa wanaweza kuwa chemchemi ya musaada. (Yakobo 5:14) Zaidi ya yote, tegemea musaada wa Mungu kupitia sala.—Wafilipi 4:6, 7, 13.
[Picha katika ukurasa wa 20]
Mungu anachukia ulevi, kuiba, muchezo wa kamari, na matendo ya ujeuri