Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rq somo 14 uku. 28-29
  • Namna Mashahidi wa Yehova Wanavyofanywa Kitengenezo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Mashahidi wa Yehova Wanavyofanywa Kitengenezo
  • Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Mungu Iko na Tengenezo?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Kwa Nini Mungu Amewapanga Watu Wake kwa Utaratibu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mashahidi wa Yehova Wanatumia Namna Gani Michango?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Utapata Faida Gani Kama Unaenda ku Mikutano ya Mashahidi wa Yehova?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Mungu Anataka Nini Kwetu?
rq somo 14 uku. 28-29

Somo 14

Namna Mashahidi wa Yehova Wanavyofanywa Kitengenezo

Siku hizi za kisasa Mashahidi wa Yehova walianza wakati gani? (1)

Mikutano ya Mashahidi wa Yehova inaendeshwa namna gani? (2)

Garama zinalipwa namna gani? (3)

Nani anayechukua uongozi katika kila kutaniko? (4)

Mikusanyiko gani mikubwa inayofanyika kila mwaka? (5)

Kazi gani inafanywa kwenye makao yao makuu na kwenye afisi za matawi? (6)

1. Siku hizi za kisasa Mashahidi wa Yehova walianza katika miaka ya 1870. Hapo kwanza, walikuwa wanaitwa Wanafunzi wa Biblia. Lakini katika 1931 walichukua jina la Kimaandiko la Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10) Kutoka mwanzo mudogo tengenezo limekua kufikia maelfu ya Mashahidi, ambao wanashugulika sana na kuhubiri katika inchi zaidi ya 230.

2. Kwa kawaida makutaniko ya Mashahidi wa Yehova yanafanya mikusanyiko mara tatu kila juma. Wewe unaalikwa kuhuzuria mukusanyiko wowote katika hiyo. (Waebrania 10:​24, 25) Biblia ndiyo musingi wa yale yanayofundishwa. Mikusanyiko inafunguliwa na kumalizwa kwa sala. “Nyimbo za kiroho” zenye kugusa moyo pia zinaimbwa kwenye mikusanyiko mingi. (Waefeso 5:​18, 19) Kuingia ni bila malipo, na hakuna sadaka zinazokusanywa.​—⁠Matayo 10:⁠8.

3. Kwa kawaida makutaniko yanafanya mikusanyiko yao katika Majumba ya Ufalme. Haya kwa desturi ni majengo ya kawaida yanayojengwa na Mashahidi wenye kujitolea. Hautaona sanamu yo yote, misalaba au vitu kama hivyo kwenye Jumba la Ufalme. Garama zinalipwa kwa zawadi za kujipendea. Kwa wale wote wanaotamani kutoa zawadi, kuna sanduku la michango.​—⁠2 Wakorinto 9:⁠7.

4. Katika kila kutaniko, kuna wazee, au waangalizi. Wanachukua uongozi katika kufundisha katika kutaniko. (1 Timoteo 3:​1-7; 5:17) Wanasaidiwa na watumishi wa huduma. (1 Timoteo 3:​8-10, 12, 13) Wanaume hao hawainuliwi juu ya wengine katika kutaniko. (2 Wakorinto 1:24) Wao hawapewi majina ya cheo ya kipekee. (Matayo 23:​8-10) Hawavai tofauti na wengine. Wala hawalipwi kwa ajili ya kazi yao. Wazee kwa kujipendea wanaangalia mahitaji ya kiroho ya kutaniko. Wanaweza kuleta kitulizo na mwongozo wakati wa magumu.​—⁠Yakobo 5:​14-16; 1 Petro 5:​2, 3.

5. Mashahidi wa Yehova pia wanafanya makusanyiko makubwa kila mwaka. Katika nyakati hizo makutaniko mengi yanakusanyika pamoja kwa ajili ya programu ya pekee ya mafundisho ya Biblia. Ubatizo wa wanafunzi wapya ni sehemu ya kawaida ya programu ya kila kusanyiko.​—⁠Matayo 3:​13-17; 28:​19, 20.

6. Makao makuu ya ulimwenguni ya Mashahidi wa Yehova yanapatikana katika New York. Hapo kuna ile Baraza Inayoongoza, kikundi chenye kufanyizwa na wazee wenye maarifa mengi wanaoangalia kutaniko la ulimwenguni pote. Pia kuzunguka ulimwengu kuna afisi za matawi zaidi ya 100. Mahali hapa, wafanya kazi wenye kujipendea wanasaidia kuchapa na kusafirisha vichapo. Uongozi unatolewa pia ili kutengeneza vizuri kazi ya kuhubiri. Kwa nini usifanye mupango wa kutembelea afisi ya tawi iliyo karibu yako zaidi?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine