Somo 14
Namna Mashahidi wa Yehova Wanavyofanywa Kitengenezo
Siku hizi za kisasa Mashahidi wa Yehova walianza wakati gani? (1)
Mikutano ya Mashahidi wa Yehova inaendeshwa namna gani? (2)
Garama zinalipwa namna gani? (3)
Nani anayechukua uongozi katika kila kutaniko? (4)
Mikusanyiko gani mikubwa inayofanyika kila mwaka? (5)
Kazi gani inafanywa kwenye makao yao makuu na kwenye afisi za matawi? (6)
1. Siku hizi za kisasa Mashahidi wa Yehova walianza katika miaka ya 1870. Hapo kwanza, walikuwa wanaitwa Wanafunzi wa Biblia. Lakini katika 1931 walichukua jina la Kimaandiko la Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10) Kutoka mwanzo mudogo tengenezo limekua kufikia maelfu ya Mashahidi, ambao wanashugulika sana na kuhubiri katika inchi zaidi ya 230.
2. Kwa kawaida makutaniko ya Mashahidi wa Yehova yanafanya mikusanyiko mara tatu kila juma. Wewe unaalikwa kuhuzuria mukusanyiko wowote katika hiyo. (Waebrania 10:24, 25) Biblia ndiyo musingi wa yale yanayofundishwa. Mikusanyiko inafunguliwa na kumalizwa kwa sala. “Nyimbo za kiroho” zenye kugusa moyo pia zinaimbwa kwenye mikusanyiko mingi. (Waefeso 5:18, 19) Kuingia ni bila malipo, na hakuna sadaka zinazokusanywa.—Matayo 10:8.
3. Kwa kawaida makutaniko yanafanya mikusanyiko yao katika Majumba ya Ufalme. Haya kwa desturi ni majengo ya kawaida yanayojengwa na Mashahidi wenye kujitolea. Hautaona sanamu yo yote, misalaba au vitu kama hivyo kwenye Jumba la Ufalme. Garama zinalipwa kwa zawadi za kujipendea. Kwa wale wote wanaotamani kutoa zawadi, kuna sanduku la michango.—2 Wakorinto 9:7.
4. Katika kila kutaniko, kuna wazee, au waangalizi. Wanachukua uongozi katika kufundisha katika kutaniko. (1 Timoteo 3:1-7; 5:17) Wanasaidiwa na watumishi wa huduma. (1 Timoteo 3:8-10, 12, 13) Wanaume hao hawainuliwi juu ya wengine katika kutaniko. (2 Wakorinto 1:24) Wao hawapewi majina ya cheo ya kipekee. (Matayo 23:8-10) Hawavai tofauti na wengine. Wala hawalipwi kwa ajili ya kazi yao. Wazee kwa kujipendea wanaangalia mahitaji ya kiroho ya kutaniko. Wanaweza kuleta kitulizo na mwongozo wakati wa magumu.—Yakobo 5:14-16; 1 Petro 5:2, 3.
5. Mashahidi wa Yehova pia wanafanya makusanyiko makubwa kila mwaka. Katika nyakati hizo makutaniko mengi yanakusanyika pamoja kwa ajili ya programu ya pekee ya mafundisho ya Biblia. Ubatizo wa wanafunzi wapya ni sehemu ya kawaida ya programu ya kila kusanyiko.—Matayo 3:13-17; 28:19, 20.
6. Makao makuu ya ulimwenguni ya Mashahidi wa Yehova yanapatikana katika New York. Hapo kuna ile Baraza Inayoongoza, kikundi chenye kufanyizwa na wazee wenye maarifa mengi wanaoangalia kutaniko la ulimwenguni pote. Pia kuzunguka ulimwengu kuna afisi za matawi zaidi ya 100. Mahali hapa, wafanya kazi wenye kujipendea wanasaidia kuchapa na kusafirisha vichapo. Uongozi unatolewa pia ili kutengeneza vizuri kazi ya kuhubiri. Kwa nini usifanye mupango wa kutembelea afisi ya tawi iliyo karibu yako zaidi?