Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • fg somo 14 uli. 1-4
  • Juu ya Nini Mungu Iko na Tengenezo?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Mungu Iko na Tengenezo?
  • Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kwa Nini Mungu Amewapanga Watu Wake kwa Utaratibu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Je, Mungu Ana Watu Wanaomtumikia kwa Utaratibu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Kutaniko Inapangwa na Kuongozwa Namna Gani?
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Namna Mashahidi wa Yehova Wanavyofanywa Kitengenezo
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
Ona Habari Zaidi
Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
fg somo 14 uli. 1-4

SOMO LA 14

Juu ya Nini Mungu Iko na Tengenezo?

1. Juu ya nini Mungu alipanga muzuri taifa la Israeli?

1. Watu wa Mungu wa taifa la Israeli; 2. Wakristo wa kwanza-kwanza katika mahubiri

Mungu alifanya watoto wa Abrahamu kuwa taifa na akawapatia sheria mbalimbali. Aliita taifa hilo “Israeli.” Walipaswa kulinda ibada ya kweli na neno lake. (Zaburi 147:19, 20) Kwa hiyo, watu wa mataifa yote wangeweza kubarikiwa kupitia taifa la Israeli.​—Soma Mwanzo 22:18.

Mungu alichagua Waisraeli ili wakuwe mashahidi wake. Historia ya Waisraeli inaonyesha namna watu wanapata faida wakati wanafuata sheria za Mungu. (Kumbukumbu la Torati 4:6) Kwa hiyo, kupitia Waisraeli, watu wengine wangeweza kumujua Mungu wa kweli.​—Soma Isaya 43:10, 12.

2. Juu ya nini Wakristo wa kweli wanapangwa muzuri?

Kisha wakati fulani, Yehova Mungu alikataa Waisraeli. Kwa hiyo, alichagua kutaniko la Kikristo ili likamate nafasi ya taifa hilo. (Matayo 21:43; 23:37, 38) Leo Wakristo wa kweli njo mashahidi wake, haiko Waisraeli.​—Soma Matendo 15:14, 17.

Yesu alipanga muzuri wanafunzi wake ili wahubiri na wafanye wanafunzi mu mataifa yote. (Matayo 10:7, 11; 24:14; 28:19, 20) Mu siku hizi za mwisho za ulimwengu huu, kazi hiyo inafanywa sana kuliko zamani. Kwa mara ya kwanza mu historia, Yehova anaunganisha mu ibada ya kweli mamilioni ya watu kutoka mu mataifa yote. (Ufunuo 7:9, 10) Wakristo wa kweli wanaungana mu tengenezo moja ili kutiana moyo na kusaidiana. Mu dunia yote, wako na programu ileile ya mafundisho ya Biblia kwenye mikutano yao.​—Soma Waebrania 10:24, 25.

3. Tengenezo la leo la Mashahidi wa Yehova lilianza namna gani?

Picha za Mashahidi wa Yehova katika miaka ya 1900 na leo; vichapo vinavyosaidia kujifunza Biblia katika luga nyingi.

Mu miaka ya 1870, kikundi kidogo cha wanafunzi wa Biblia kilianza kutafuta tena mafundisho ya kweli ya Biblia yenye ilikuwa imefichwa kwa wakati murefu. Walijua kama Yesu alikuwa amepanga muzuri kutaniko la Kikristo ili lifanye kazi ya kuhubiri. Kwa hiyo, wanafunzi hao wa Biblia walianza kuhubiri Ufalme mu mataifa yote. Mu mwaka wa 1931, walikamata jina Mashahidi wa Yehova.​—Soma Matendo 1:8; 2:1, 4; 5:42.

4. Tengenezo la Mashahidi wa Yehova linaongozwa namna gani?

Wakati wa mitume, kulikuwa makutaniko ya Kikristo mu inchi mingi. Ile makutaniko iliongozwa na baraza lenye kuongoza, lenye lilimuitika Yesu kuwa Kichwa cha kutaniko. (Matendo 16:4, 5) Leo vilevile, Mashahidi wa Yehova mu dunia yote wanaongozwa na Baraza Lenye Kuongoza, lenye kufanyizwa na wazee wenye kuwa na uzoefu. Baraza hilo linasimamia biro za tawi za Mashahidi wa Yehova zenye kutafsiri, kuchapisha, na kugawa vichapo vyenye kutusaidia kujifunza Biblia; vile vichapo vinapatikana mu luga zaidi ya 800. Kupitia njia hiyo, Baraza Lenye Kuongoza linatia moyo na kuongoza makutaniko zaidi ya 120 000 yenye kupatikana mu dunia yote. Mu kila kutaniko la Mashahidi wa Yehova, muko wanaume wenye kustahili wenye kuwa wazee ao waangalizi. Wanaume hao wanachunga kundi la Mungu kwa upendo.​—Soma 1 Petro 5:2, 3.

Mashahidi wa Yehova wamepangwa muzuri ili kuhubiri habari njema na kufanya wanafunzi. Kama vile mitume walikuwa wanafanya, tunahubiri nyumba kwa nyumba. (Matendo 20:20) Tena, tunajifunza Biblia na watu wenye wanapenda kabisa kujua kweli. Lakini sisi Mashahidi wa Yehova hatuko tu tengenezo. Tuko familia yenye kuwa na Baba mwenye upendo. Tuko ndugu na dada wenye kuhangaikiana. (2 Watesalonike 1:3) Kwa sababu Mashahidi wa Yehova wanapangwa muzuri ili kumufurahisha Mungu na kusaidia wengine, wao ni familia yenye furaha zaidi ku dunia.​—Soma Zaburi 33:12; Matendo 20:35.

Ili kupata habari zaidi, ona sura ya 19 ya kitabu Biblia Inatufundisha Nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine