Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • kn35 uku. 1-2
  • Je! Kuna wakati ambao watu wataweza kupendana?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je! Kuna wakati ambao watu wataweza kupendana?
  • Je! Kuna wakati ambao watu wataweza kupendana?
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Upendo kwa jirani umepoa
  • Kwa nini upendo kwa jirani umepoa?
  • Upendo kwa jirani—jambo halisi
  • Wakati watu wote watakapopendana
  • ‘Mupende Jirani Yako Kama Wewe Mwenyewe’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • ‘Unamupenda Jirani Yako Kama Wewe Mwenyewe’?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • “Je! Kuna Wakati Ambao Watu Wataweza Kupendana?”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Je, Kuna Dini Yoyote Ambayo Unaweza Kutumainia Kuhusiana na Vita?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Je! Kuna wakati ambao watu wataweza kupendana?
kn35 uku. 1-2

Habari za Ufalme Na. 35

Je! Kuna wakati ambao watu wataweza kupendana?

Upendo kwa jirani umepoa

MAMILIONI ya watu hujisikia kukosa tumaini pia wao ni katika hali ya kusikitikiwa, pasipo msaada wowote. Mwanamke mmoja mfanya-biashara aliyeacha kazi alieleza: “Mjane mmoja aliyeishi kwenye orofa juu yangu, jioni moja aligonga mlangoni na kusema alikuwa mpweke. Niliamwambia kwa adabu lakini kwa haraka kwamba nilikuwa mwenye shughuli nyingi. Aliniomba radhi na akaondoka zake.”

Jambo la huzuni ni kwamba, usiku huohuo, mjane huyo alijiua. Mwanamke mfanya-biashara huyo, baadaye, alisema kwamba alipata “somo kubwa.”

Ukosefu wa upendo kwa jirani mara nyingi hutokeza msiba. Katika Bosnia na Herzegovina, zilizokuwa hapo zamani sehemu za Yugoslavia, zaidi ya watu milioni moja walilazimika kuacha makao yao na makumi ya maelfu waliuawa katika mapigano ya kikabila. Walitendewa hivyo na nani? Na “majirani wetu,” aliomboleza binti mmoja aliyefukuzwa kutoka kijiji chake. “Tunawajua” akaongeza.

Katika Rwanda mamia ya maelfu ya watu walichinjwa, mara nyingi na majirani wao wenyewe. The New York Times liliripoti: “Wahutu na Watutsi waliishi pamoja, walioana kati yao, bila ya shaka, au bila hata kujua nani aliyekuwa Muhutu na nani Mututsi. Ndipo jambo fulani likaingizwa kwa ghafla,” nayo “mauaji yakaanza.”

Vivyo hivyo, katika Israeli Wayahudi na Waarabu huishi pamoja, lakini wengi wao huchukiana. Hali ni ileile kati ya Wakatoliki na Waprotestanti wengi katika Ailandi na idadi ya watu wanaofanya hivyo katika nchi nyingine huongezeka. Hakujapata kuwa katika historia ya ulimwengu kipindi chenye ukosefu wa upendo kama leo.

Kwa nini upendo kwa jirani umepoa?

Muumba wetu anatoa jibu. Neno lake Biblia linaita wakati tunamoishi “siku za mwisho.” Hiki ni kipindi ambamo unabii wa Biblia husema kwamba watu watakuwa “wasio na na shauku ya kiasili.” Kuhusu hizi “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,” zinazoitwa pia katika Maandiko “umalizio wa mfumo wa mambo,” Yesu Kristo alisema kimbele kwamba “upendo wa idadi iliyo kubwa zaidi utapoa.” —2 Timotheo 3:1-5; Mathayo 24:3, 12.

Hivyo, ukosefu wa upendo leo ni mojawapo ya mambo yanayoshuhudia kwamba sisi tunaishi katika siku za mwisho za ulimwengu huu. Jambo la furaha, itamaanisha pia kwamba ulimwengu mpya wa haki wenye kuongozwa na upendo utachukua mahali pa huu ulimwengu wa watu wasiomwogopa Mungu. —Mathayo 24:3-14; 2 Petro 2:5; 3:7, 13.

Lakini, je! tunayo kweli sababu ya kuamini kwamba badiliko kama hilo linawezekana na kwamba watu wote wanaweza kujifunza kupendana na kuishi pamoja kwa amani wamoja na wengine?

Upendo kwa jirani—jambo halisi

“Ni nani kwa kweli aliye jirani yangu?” ndivyo mwana-sheria mmoja wa karne ya kwanza alivyomuuliza Yesu. Bila shaka, yeye alimtazamia Yesu aseme, ‘Myahudi mwenzako.’ Lakini katika hadithi ya msamaria mwenye fadhili, Yesu alionyesha kwamba watu wa mataifa mengine wao pia ni majirani wetu.—Luka 10:29-37; Yohana 4:7-9.

Yesu alitia mkazo kwamba, lifuatalo upendo kwa Mungu, ni upendo kwa jirani unaopaswa kuongoza maisha yetu. (Mathayo 22:34-40) Lakini, je! kumepata kuwa na kikundi chochote cha watu kilichopata kupenda majirani kwelikweli? Wakristo wa kwanza walifanya hivyo! Walijulikana sana kwa ule upendo waliokuwa nao kwa wengine.—Yohana 13:34, 35.

Namna gani leo? Je! kuna yeyote anayezoea au kuonyesha upendo unaolingana na ule wa Kristo? Encyclopedia Canadiana yasema: “Ile kazi ya Mashahidi wa Yehova ni uamsho na kuwekwa upya kwa Ukristo wa zamani za kwanza uliozoewa na Yesu na wanafunzi wake pia . . . Wote ni ndugu.”

Haya yanamaanisha nini? Yamaanisha kwamba Mashahidi wa Yehova hawaruhusu kitu chochote—iwe asili ya mtu, taifa, wala ukabila—kuwa sababu ya kuchukia majirani wao. Wala hawataweza kumuua mtu mwingine, kwa kuwa wamekwisha, kwa namna ya mfano, kufua mapanga yao kuwa majembe na mikuki kuwa miundu ya kukata matawi. (Isaya 2:4) Kwa kweli, Mashahidi wanajulikana sana kwa kuchukua hatua ya kwanza ili kusaidia majirani wao.—Wagalatia 6:10.

Si jambo la kushangaza kwamba gazeti Sacramento Union la California liliandika: “Yatosha kusema kwamba ikiwa ulimwengu wote ungeishi kulingana na kanuni za imani za Mashahidi wa Yehova umwagaji damu na chuki vingekoma, pia upendo ungetawala kama mfalme.” Katika gazeti Ring la Hangari mwandishi mmoja alisema: “Nimekuja kufikia kwenye lile neno la mwisho kwamba ikiwa Mashahidi wa Yehova wangekuwa ndio peke yao wanaoishi duniani, vita vingekoma kuweko, na polisi wangalikuwa na kazi tu ya kuelekeza magari na watu barabarani, na pia kutolea paspoti.”

Ingawa hivyo, ikubaliwe kwamba badiliko kubwa mno la ulimwenguni pote litahitajiwa ikiwa watu wote watapendana. Badiliko hilo litakujaje? (Tafadhali angalia ukurasa wa nyuma.)

Wakati watu wote watakapopendana

Sala aliyoifundisha Yesu Kristo yaonyesha kwamba badiliko la kustaajabisha la karibia. Katika hotuba yake maarufu juu ya Mlima, Yesu alitufundisha kusali hivi: “Ufalme wako uje. Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama mbinguni.”—Mathayo 6:10, Zaïre Swahili Bible.

Ufalme wa Mungu ni nini? Ni serikali halisi, ambayo hutawala kutoka mbinguni. Ni kwa sababu hiyo unaitwa “Ufalme wa mbingu.” Yesu, “Mwana-mfalme wa Amani,” amewekwa rasmi na Baba yake kuwa mtawala wa Ufalme huo.—Mathayo 10:7; Isaya 9:6, 7; Zaburi 72:1-8.

Ufalme wa Mungu unapokuja, nini litatukia kwa ulimwengu huu unaojaa na chuki? “Ule Ufalme utaponda na kukomesha” serikali zote potovu za ulimwengu huu. (Danieli 2:44) Biblia yaeleza: “Ulimwengu unapitilia mbali . . . , lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hudumu milele.”—1 Yohana 2:17.

Kuhusu ulimwengu mpya wa Mungu, Biblia yasema: “Wenye haki watariti inchi, na kukaa ndani yake milele.” (Zaburi 37:9-11, 29; Mithali 2:21, 22, ZSB) Utakuwa wakati mtukufu kama nini! “Kifo hakitakuwapo tena, wala ombolezo wala kupaaza kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe.” (Ufunuo 21:4) Hata wafu wataishi tena, na dunia nzima itageuzwa kuwa paradiso halisi.—Isaya 11:6-9; 35:1, 2; Luka 23:43; Matendo 24:15.

Ili kuishi katika ulimwengu huo mpya wa Mungu, tunapaswa kupendana, kama Mungu atufundishavyo kufanya. (1 Wathesalonike 4:9) Mwanafunzi wa Biblia mmoja wa Mashariki alisema: “Ninatazamia wakati ujao, kama Biblia inavyoahidi, wakati watu wote watajifunza kupendana.” Nasi tunaweza kuwa hakika kwamba Mungu atatimiza ahadi zake! ‘Hata nimesema juu yazo,’ anasema, ‘Nami nitafanya hivyo pia.’—Isaya 46:11.

Lakini kufurahia baraka chini ya Ufalme wa Mungu, yakupasa utwae ujuzi wa Biblia, kama wanavyofanya mamilioni ya watu wenye mioyo minyofu ulimwenguni pote. (Yohana 17:3) Broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? yenye kurasa 32 itakusaidia kufanya hivyo. Ujipatie nakala moja kwa kujaza sehemu inayoweza kukatwa inayotolewa kwenye ukurasa unaotangulia na uitume kwenye anwani iliyo karibu sana na makao yako.

[Mahali Picha Ilitoka ukurasa wa 2]

Muuaji Anayejificha na Mazishi Katika Bosnia: Reuters/Corbis-Bettmann

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine