“Je! Kuna Wakati Ambao Watu Wataweza Kupendana?”
1 Ujumbe mzuri sana, wenye kusisimua na kuburudisha utatangazwa hivi karibuni ulimwenguni pote katika lugha 169. Ni mambo gani yaliyomo? Utatolewa jinsi gani?
2 Ni ujumbe kuhusu upendo wa jirani. Tunaupata katika trakti Habari za Ufalme Na. 35 yenye kichwa kifuatacho: “Je! Kuna Wakati Ambao Watu Wataweza Kupendana?” Trakti hiyo inafanya uchunguzi mfupi wa hali ya ulimwengu na inafasiria kwamba ni ukosefu wa upendo kati ya watu ndicho chanzo cha maumivu mengi na mateso. Inaonyesha pia kwa nini, hasa leo, upendo kwa jirani umepoa na lile ambalo hilo humaanisha kwa wakati ujao.
3 Zaidi ya hilo, trakti Habari za Ufalme Na. 35 inafunua kwamba upendo wa kweli kwa jirani uko kati ya mamilioni ya watu wanaoishi sasa ulimwenguni. Inaonyesha ni watu gani wanaorudisha Ukristo wa kwanza, ibada iliyokuwa ikitolewa kwenye karne ya kwanza ambayo ilikuwa na alama ya upendo kwa jirani kama vile Yesu Kristo alivyofundisha.—Lk. 10:25-37.
4 Trakti Habari za Ufalme Na. 35 inamalizia kwa kufasiria jinsi wanadamu wote watakavyotumikisha hivi karibuni upendo kwa jirani chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu uliokabidhiwa Kristo. Wale watakaosoma ujumbe huo wanaalikwa kujipatia broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? na kuvumbua jinsi ya kufaidika na mipango yenye kujaa upendo inayoonyeshwa katika Neno la Mungu.
5 Nani Atatangaza Ujumbe Huo? Mnamo miezi ya Novemba na Desemba, Mashahidi wa Yehova wa ulimwenguni pote watatangaza ujumbe huo wa upendo kwa jirani kwa marafiki zao, kwa majirani zao na washiriki wa familia zao. Wote ambao wanatimiza matakwa yanayoombwa wanaalikwa kugawa trakti Habari za Ufalme Na. 35.
6 Kusudi la kampeni hiyo ni kuamsha kupendezwa kwa watu kwa ajili ya funzo la Biblia kwa msingi wa broshua Anataka au wa kitabu Ujuzi. Zaidi ya hilo, jitihada ambazo kila mmoja wa watumishi wa Yehova atafanya kwa moyo wake wote zitatoa ushuhuda mkubwa kuhusu Mungu wa upendo, Yehova, na kwa Mwana wake, Yesu Kristo.