Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • kn36 uku. 1-4
  • Mileani Mpya wakati ujao unakuwekea nini wewe?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mileani Mpya wakati ujao unakuwekea nini wewe?
  • Mileani Mpya wakati ujao unakuwekea nini wewe?
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mileani Mpya mwanzo wa wakati mpya?
  • Uchafuzi
  • Ugonjwa
  • Umaskini
  • Vita
  • Mileani itakayoletea wanadamu baraka
  • Ujuzi uongozao kwenye uhai!
  • Tukuze kupendezwa kulikoamshwa na Habari za Ufalme na. 36
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Mileani Mpya wakati ujao unakuwekea nini wewe?
kn36 uku. 1-4

Habari za Ufalme Na. 36

Mileani Mpya wakati ujao unakuwekea nini wewe?

Mileani Mpya mwanzo wa wakati mpya?

MNAMO Desemba 31, 1999, pa saa sita za usiku, karne ya 20 ilimalizika.a Ilikuwa karne iliyoona msukosuko mwingi. Lakini hiyo iliona pia mwanzo wa teknolojia mpya, maendeleo makubwa ya kiganga, mlipuko katika kueneza habari, na uchumi wenye kukua haraka ulimwenguni pote. Kwa hiyo, mileani mpya imekaribishwa na wengi kuwa alama ya tumaini na mabadiliko. Je, yaelekea hiyo itaona mwisho wa vita, umaskini, uchafuzi wa mazingira, na ugonjwa?

Wengi wanatumaini hivyo. Lakini kuna uwezekano gani kwamba mileani mpya itatokeza mabadiliko yanayokufaidi wewe—mabadiliko ambayo yatafanya maisha yawe salama na bila hofu kwako na kwa familia yako? Fikiria ukubwa wa matatizo machache tu ambayo tunakabiliana nayo.

Uchafuzi

Nchi zenye viwanda ni “zenye kutokeza uharibifu wa mazingira ulimwenguni pote na uchafuzi wenye kuenea mahali pote na mvurugo wa pori na wanyama wanaoishi ndani.” Ikiwa mielekeo ya sasa inaendelea, “mazingira ya kiasili yatakuwa chini ya mikazo.”— “ Avenir de l’environnement mondial — 2000 ”, Programme des Nations Unies pour l’environnement.

Ugonjwa

“Kufikia mwaka 2020, magonjwa yasiyoambukiza yanatazamiwa kuwa sababu kubwa ya vifo saba kwa kumi katika maeneo yanayoendelea, kwa kulinganisha na hesabu yenye kupungua nusu leo.”— “Ulimwengu Unaosumbuliwa na Magonjwa,” Harvard University Press, 1996 (Kiingereza).

Wataalamu fulani wanasema kwamba “kufikia 2010, zile nchi 23 zenye magonjwa makali zaidi [ya UKIMWI] yenye kushika watu wengi pamoja zitakuwa zimepoteza watu milioni 66.”— “ Face au sida : la situation dans les pays en développement ”, rapport conjoint de la Commission européenne et de la Banque mondiale.

Umaskini

“Karibu watu bilioni 1.3 wanaishi na kiasi chenye kupungua dola moja kwa siku, na karibu bilioni 1 hawawezi kutosheleza mahitaji yao ya msingi ya chakula.”—“ Rapport mondial sur le développement humain 1999 ”, Programme des Nations Unies pour le développement.

Vita

“Labda jeuri katika [nchi mbalimbali] itafikia kiwango ambacho hakijafikiwa kamwe. Ikitokezwa na [migawanyiko] ya kikabila na ya kidini, . . . jeuri kama hiyo itafanyiza . . . pambano la kawaida zaidi katika miaka 25 ya kwanza ya karne ijayo . . . , ikiua mamia ya maelfu ya watu kila mwaka.”— “ À l’aube d’un nouveau monde : la sécurité nationale au XXI e siècle ”, Commission américaine d’étude sur la sécurité nationale au XXI e siècle.

Kwa hiyo, makelele na msisimuko kwa sababu ya mileani mpya vinaficha jambo la kwamba uchafuzi, ugonjwa, umaskini, na vita vinaonekana kuwa tisho kubwa zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Msingi wa matatizo hayo ni pupa, kutotumainiana, na ubinafsi—tabia ambazo haziwezi kuondolewa tu na utafiti wa kisayansi, teknolojia, au siasa.

Mileani itakayoletea wanadamu baraka

Mwandishi mmoja wa kale alisema: “Njia ya mutu haiko katika nafsi yake mwenyewe; kuongoza hatua zake si katika uwezo wa mutu anayetembea.” (Yeremia 10:23) Mwanadamu hana uwezo wala haki ya kutawala dunia. Mfanyi wetu, Yehova Mungu, peke yake ndiye aliye na haki na ujuzi wa kutatua kwa matokeo matatizo ya wanadamu.—Waroma 11:33-36; Ufunuo 4:11.

Lakini wakati gani? Jinsi gani? Uhakikisho wa kwamba tunakaribia mwisho wa “siku za mwisho” ni wenye nguvu sana. Fungua Biblia yako, tafadhali, na usome 2 Timotheo 3:1-5. Andiko hilo linatoa habari kwa nguvu kuhusu tabia za utu ambazo watu wangeonyesha katika hizi “nyakati za hatari.” Mathayo 24:3-14 na Luka 21:10, 11 yanatoa pia habari kuhusu “siku za mwisho.” Katika maandiko hayo, mkazo unawekwa juu ya matukio yaonekanayo ambayo yametukia tangu 1914, matukio kama vile vita vya ulimwenguni pote, magonjwa ya kuambukiza, na ukosefu wa chakula wenye kuenea mahali pote.

Karibuni, “siku za mwisho” zitakwisha. Danieli 2:44 linasema: “Mungu wa mbinguni atasimamisha ufalme usioharibiwa milele, . . . utavunja vipande vipande na kuharibu falme hizi zote [za kidunia], nao utasimama milele.” Hivyo, ilitabiriwa kwamba Mungu angesimamisha Ufalme, au serikali, itakayotawala dunia. Kulingana na Ufunuo 20:4, serikali hiyo itatawala kwa miaka elfu—mileani! Fikiria tu njia fulani ambazo katika hizo hali za maisha zitafanywa kuwa bora kwa ajili ya wanadamu wote wakati wa Mileani hiyo tukufu:

Uchumi. “Watajenga nyumba, na kukaa ndani yao; na watapanda mizabibu, na watakula matunda yake: hawatajenga na mutu mwingine kukaa ndani yao; hawatapanda, na mutu mwingine kula matunda yake.”—Isaya 65:21, 22.

Afya. “Ndipo macho ya vipofu yatafunguliwa, na masikio ya viziwi yatafunguliwa. Ndipo kiwete atarukaruka kama ayala, na ulimi wa bubu utaimba.” “Wala hapana mwenyeji atakayesema, mimi ni mgonjwa.”—Isaya 33:24; 35:5, 6.

Mazingira. Mungu ‘ataharibu wale wanaoharibu inchi.’—Ufunuo 11:18, ZSB.

Uhusiano Kati ya Watu. “Hawataumiza wala kuharibu katika mulima wangu wote mutakatifu; maana dunia itajaa na kumujua BWANA.”—Isaya 11:9.

Mamilioni ya watu wana imani katika ahadi hizo za Biblia na hivyo wamepata maoni ya wakati ujao yenye kutazamia mema na yaliyo na uhakika. Kama tokeo, wanaweza kukabiliana vizuri zaidi na mikazo na matatizo ya maisha. Biblia inawezaje kuwa nguvu yenye kuongoza katika maisha yako?

Ujuzi uongozao kwenye uhai!

Nyakati nyingine, sayansi na teknolojia vinaweza kuwa vyenye kushangaza sana! Hata hivyo, ujuzi wa kibinadamu haukufanya maisha ya watu walio wengi yawe salama na yenye furaha. Habari ya ujuzi pekee unaoweza kutimiza hilo inatolewa katika Biblia kwenye Yohana 17:3, linalosema: “Hii yamaanisha uhai udumuo milele, wao kuendelea kutwaa ujuzi juu yako wewe, Mungu pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.”

Ujuzi kama huo unapatikana katika kurasa za Biblia. Ijapokuwa wengi hutoa maoni yenye nguvu kuhusu kitabu hicho kitakatifu, ni wachache tu ndio wamejichunguzia hicho wenyewe. Namna gani wewe? Bila shaka, kusoma Biblia kunaomba jitihada kubwa, lakini kunastahili jitihada hiyo. Biblia ndicho kitabu pekee “[kilicho]puliziwa na Mungu na ni [chenye] manufaa kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu.”—2 Timotheo 3:16.

Unawezaje, basi, kuanza kufahamiana na Biblia? Kwa nini usikubali msaada wa Mashahidi wa Yehova? Hao wanatoa mafundisho kwa mamilioni ya watu katika nyumba zao, bila malipo. Ili kukusaidia katika jambo hilo, wanatumia vichapo mbalimbali vyenye msingi juu ya Biblia, vichapo kama vile broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? Inatoa majibu yenye mambo mengi katika maneno machache kwa mengi ya maulizo unayoweza kuwa nayo kuhusu Biblia, maulizo kama vile: Mungu ni nani? Kusudi la Mungu kwa dunia ni gani? Ufalme wa Mungu ni nini? Biblia inaweza kukusaidiaje kufanya maisha ya familia yako yawe bora?

Ikiwa unataka mmoja wa Mashahidi wa Yehova akutembelee nyumbani kwako, tafadhali jaza kuponi iliyo hapa chini. Watakuwa wenye furaha kukutolea habari zaidi kuhusu Utawala mtukufu wa Mileani wa Ufalme wa Mungu!

[Maelezo ya chini]

a Tunazungumzia maoni ya watu wote huko Magharibi kuhusu mileani mpya. Kwa kweli, mileani mpya itaanza mnamo Januari 1, 2001.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine