Tukuze kupendezwa kulikoamshwa na Habari za Ufalme na. 36
1 Je, umemaliza kugawa furushi lako la Habari za Ufalme Na. 36? Trakti hiyo inauliza ulizo lenye kufika pa wakati wenye kufaa, ulizo ambalo wote wanapaswa kufikiria kwa uangalifu: “Mileani Mpya—Wakati Ujao Unakuwekea Nini Wewe?” Kadiri mwaka wa 2000 ulivyokaribia, matazamio kuhusu yale ambayo mileani mpya ingeleta yalitofautiana sana. Trakti Habari za Ufalme Na. 36 inazungumzia mengine ya matazamio hayo na kutukumbusha kwamba hali za ulimwengu hazitoi msingi wa kutazamia mema. Mileani moja pekee ambayo italeta amani na usalama ambao watu walio wengi hutafuta ni ule Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo Yesu. Uhakika wetu katika jambo la kwamba Ufalme wake ni halisi umetuchochea kugawa Habari za Ufalme Na. 36 kwa kila mtu iwezekanavyo.
2 Itikio mbalimbali kuelekea Habari za Ufalme: Ugawaji mbalimbali uliotangulia wa Habari za Ufalme umeonekana kuwa kichocheo bora kwetu katika kazi yetu. Kuhusu Habari za Ufalme Na. 35, ofisi ya Kanada iliandika: “Kampeni hii ya pekee ilitegemezwa kwa bidii na wahubiri na mapainia shambani, na mambo mengi yaliyoonwa yenye kutia moyo yalifurahiwa.” Bila shaka mmeonyesha bidii yenye kufanana na hiyo kwa ajili ya ugawaji wa Habari za Ufalme Na. 36.
3 Kampeni ya sasa ya Habari za Ufalme inapangwa kumalizika mnamo Novemba 17, 2000. Je, eneo lote linalotolewa kuwa mgawo kwa kutaniko lenu limetembelewa? Ikiwa sivyo, wazee wanaweza kuwaomba mwendelee na kampeni mpaka mwisho wa Novemba.
4 Mpaka sasa, watu wameitikiaje ugawaji wa Habari za Ufalme Na. 36 mahali penu? Watu wachache ndio watajaza kuponi na kuomba nakala ya broshua Anataka na/au funzo la Biblia la nyumbani. Hata hivyo, wengi wa wale ambao mwanzoni huonyesha kupendezwa na habari kuhusu mileani hiyo yaelekea hawatachukua hatua mpaka mmoja wa Mashahidi wa Yehova atakaporudi kuwatembelea. Wale wote walioonyesha kupendezwa wanapaswa kutembelewa tena. Ni wakati gani ungekuwa bora kufanya hivyo? Kufuatia mambo kunapaswa kufanywa mapema zaidi iwezekanavyo.
5 Ona mambo haya yaliyoonwa, ambayo yalitokana na kurudi baada ya kuachia watu Habari za Ufalme Na. 35. Painia mmoja katika Ireland aliacha Habari za Ufalme kwa mtu aliye na hoteli ya chakula. Ujumbe uligusa mwanamke huyo hivi kwamba alialika dada arudi. Dada akarudi baada ya siku mbili, na funzo la Biblia likaanzishwa. Katika Denmark, nakala ya Habari za Ufalme iliachwa kwenye nyumba ambako hakukuwa mtu. Siku hiyohiyo mwanamke aliyeishi hapo akatuma kuponi kwa ofisi ya tawi, ambayo ilituma kuponi hiyo kwa kutaniko la mahali hapo. Kabla ya juma kwisha, dada wawili walimtembelea mwanamke huyo, mipango kwa ajili ya funzo ikachukuliwa, naye akahudhuria mkutano wake wa kwanza kwenye Jumba la Ufalme!
6 Mambo ya kusema wakati mnaporudi: Kufanya ziara za kurudia kwa watu ambao tuliachia Habari za Ufalme ni jambo jepesi kwa njia fulani, na jambo hilo ni sehemu yenye kufurahisha ya huduma yetu. Wakati wa kufanya ziara hizo, ni vizuri zaidi kuchukua nakala ya Habari za Ufalme Na. 36, kwa kuwa huenda mwenye-nyumba hana nakala yake. Unaweza kujaribu madokezo haya.
7 Baada ya kukumbusha mwenye-nyumba wewe ni nani, unaweza kusema:
◼ “Niliacha trakti yenye kichwa ‘Mileani Mpya—Wakati Ujao Unakuwekea Nini Wewe?’ Je, halikuwa jambo lenye kutia moyo kusoma kwamba karibuni Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo Yesu utaanza, ukileta hali za Paradiso duniani? [Onyesha picha za Paradiso katika Habari za Ufalme Na. 36.] Kwenye ukurasa wa mwisho, unaalikwa kuomba nakala ya broshua Mungu Anataka Nini Kwetu?” Onyesha broshua, geuza hiyo kwenye somo 5, soma ulizo la kwanza na mafungu 1 na 2, na umwombe mwenye-nyumba atoe maelezo. Someni na kuzungumzia andiko moja au mawili. Ikiwa inawezekana, fikirieni ulizo lingine na fungu lingine, kisha mchukue mipango kwa ajili ya kurudi ili kuendeleza mazungumzo.
8 Kwa kuwa toleo la Novemba kwa ajili ya kufuatia mambo ni broshua “Anataka” au kitabu “Ujuzi,” unaweza kusema:
◼ “Wakati nilipokutembelea hivi majuzi, niliacha nakala ya ‘Mileani Mpya—Wakati Ujao Unakuwekea Nini Wewe?’ Hiyo ina pendekezo la funzo la Biblia la nyumbani bila malipo. Nimerudi kukuonyesha kichapo chenye kusaidia kwa ajili ya funzo ambacho tunatumia. [Onyesha broshua Anataka, na uigeuze kwenye ukurasa wa mwisho; au uonyeshe kitabu Ujuzi, na ukigeuze kwenye kurasa 188-9.] Ile Mileani inayozungumziwa katika Biblia italeta hali zenye kufanana na zile unazoona kwenye picha hii. Ili kustahili kuishi katika Paradiso, tunahitaji kutwaa ujuzi sahihi juu ya Mungu. Tafadhali niruhusu nikuonyeshe kwa kifupi jinsi tunavyojifunza Biblia.”
9 Ugawaji wa Habari za Ufalme Na. 36 umetuchochea kuzidisha ushiriki wetu katika huduma, ukitokeza ushahidi mkubwa. Yaelekea kwamba ugawaji huo umeamsha kupendezwa kwa watu wengi katika eneo. Kwa msaada wa Yehova, jitihada yetu yenye umoja ya kukuza kupendezwa huko itafanya tupate kwa furaha watu wengi zaidi wenye mfano wa kondoo.—Mt. 10:11; Mdo. 13:48, 49, 52.