“Mileani mpya—wakati ujao unakuwekea nini wewe?”
1 Ulizo hilo limekuwa katika akili za watu kuzunguka dunia. Ingawa wanadamu wametimiza mengi muda wa karne nyingi, watu hawadanganywi tena kwa sababu matatizo ya msingi ambayo yamesumbua wanadamu kwa mileani mingi yangali mpaka leo. (Yobu 14:1; Zab. 90:10) Wanadamu wanaweza kupata kitulizo wapi?
2 Mnamo miezi ya Oktoba na Novemba, tutakuwa na nafasi ya pekee ya kutolea majirani zetu jibu kwa ulizo hilo. Namna gani? Kupitia ugawaji wa Habari za Ufalme Na. 36. Trakti hiyo ni yenye kichwa “Mileani Mpya—Wakati Ujao Unakuwekea Nini Wewe?” Mnamo nusu ya kwanza ya Oktoba, tutatolea watu magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kisha, kuanzia Siku ya Kwanza, Oktoba 16, mpaka Siku ya Tano, Novemba 17, tutajitoa katika ugawaji mkubwa wa Habari za Ufalme Na. 36. Muda wa kampeni hiyo, tutakaza fikira juu ya kuachia watu Habari za Ufalme Na. 36 tangu Siku ya Kwanza mpaka Siku ya Tano. Kwenye miisho-juma, tutatoa trakti hiyo pamoja na magazeti ya sasa.
3 Je, utashiriki kikamili? Wazee, watumishi wa huduma, na mapainia watataka kuchukua uongozi katika kampeni hii, kwa kuwa wao ndio wako kwenye nafasi ya mbele ya kazi hii. Wahubiri wengi wamerekebisha hali zao ili kuwa mapainia wasaidizi muda wa mwezi mmoja au yote miwili ya ugawaji huo. Wengine wanapanga kupitisha katika huduma wakati mwingi zaidi kuliko kawaida.
4 Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wanaweza kusaidia kwa kutia moyo kila mshiriki wa kikundi chao ashiriki kikamili katika ugawaji wa Habari za Ufalme Na. 36. Huenda kukawa wahubiri fulani ambao wamekuwa wasiotenda katika kazi ya kuhubiri. Wazee wanapaswa kutembelea wahubiri hao ili kuona kile kinachoweza kufanywa ili kuwasaidia. Labda mipango inaweza kuchukuliwa kusudi, mnamo miezi hiyo, mhubiri mwenye ujuzi aambatane shambani na kila mtu asiyetenda. Ule utoaji mwepesi wa Habari za Ufalme Na. 36 unaweza kuwa ndilo jambo pekee linalohitajiwa ili kufanya wahubiri hao wawe wenye kutenda tena.
5 Hii itakuwa pia nafasi nzuri kwa wanafunzi wa Biblia ambao wanakaribia kumaliza kitabu Ujuzi na ambao wana sifa zenye kuwastahilisha kuwa wahubiri wasiobatizwa kuanza kushiriki katika huduma. Hata watoto wanaweza kushiriki vizuri katika kazi hii yenye kusisimua.
6 Utoaji mwepesi tu ndio unaohitajiwa. Unaweza kusema:
◼ “Nimetoa kwa kujipendea wakati wangu ili nisaidie kugawa ujumbe huu wa maana sana kwa kila familia hapa [jina la mji au nchi]. Hii ndiyo nakala yako. Tafadhali soma yenyewe.” Linaweza kuwa jambo lenye faida kutochukua mfuko wa mahubiri wakati wa kugawa Habari za Ufalme Na. 36.
7 Mikutano iliyopangwa vizuri kwa ajili ya utumishi wa shambani: Wazee wanapaswa kuangalia kwamba mipango kwa ajili ya kutoa ushahidi iwe yenye kufaa na yenye kutumika. Mwangalizi wa utumishi hasa anapaswa kuhakikisha kwamba kuna eneo la kutosha la nyumba kwa nyumba au la kibiashara kusudi kila mmoja ashiriki kikamili katika kazi hii. Mahali popote inapowezekana, mikutano kwa ajili ya utumishi inapaswa kupangwa kila siku, kuanzia Siku ya Kwanza mpaka Siku ya Tano, kwenye miisho-juma, na jioni. Kwa faida ya wanafunzi wa shule, wafanyakazi wasiokuwa na saa kamili za kazi, na wengine, mipango inaweza kuchukuliwa ili kukutana jioni inapokaribia.
8 Jambo la kufanya kuhusu wale wasiokuwako nyumbani: Mradi wetu ni kuongea na wenye-nyumba wengi zaidi iwezekanavyo. Ikiwa hakuna mtu nyumbani wakati wa ziara yako, andika anwani hiyo na uje pa wakati tofauti wa mchana. Ikiwa mpaka juma la mwisho la kampeni haukufanikiwa kukutana na wenye-nyumba hao, unaweza kuwaachia nakala ya Habari za Ufalme Na. 36 mahali pasipoonwa na wapita-njia. Huenda wazee wa mahali penu wakaagiza kutaniko kuacha nakala ya Habari za Ufalme Na. 36 kwa wale wasiokuwako nyumbani kwenye ziara ya kwanza wakati wa kutumika katika maeneo ya vijijini au mahali ambako kuna eneo kubwa kuliko lile linaloweza kutembelewa muda wa kampeni.
9 Acheni tuharakishe kazi! Makutaniko yanapaswa kujitahidi kumaliza eneo layo mbele ya kampeni kumalizika mnamo Novemba 17. Ikiwa eneo lenu ni kubwa sana, wahubiri fulani wanaweza kutumika peke yao mahali ambapo hilo ni jambo lenye kufaa na lenye usalama. Mpango kama huo utafanya iwe vyepesi zaidi kufikia watu wenye kupendezwa wengi zaidi iwezekanavyo. Hakikisheni kwamba mnalinda maandishi mazuri kuhusu kupendezwa kokote kulikopatikana.
10 Wazee wanapaswa kukadiria kimbele ni magazeti mangapi ya ziada ambayo kutaniko litahitaji na kufanya ombi kupatana na jambo hilo. Hakuna uhitaji wa kutoa ombi la Habari za Ufalme Na. 36, kwa kuwa furushi litatumwa kwa kila kutaniko. Mapainia wa pekee, wa kawaida, na wasaidizi watapokea kila mmoja nakala 200 za kugawa, huku wahubiri wa kutaniko wakipewa nakala 50 kila mmoja. Kwa hiyo, je, nyinyi ni tayari na wenye hamu ya kuharakisha kazi katika utendaji huu wa pekee? Sisi ni wenye kupendelewa kama nini kujulisha majirani zetu wote yale ambayo Mungu ameahidi kwa ajili ya wakati ujao ulio karibu!